Zitto atua Dodoma kuinadi ACT

Zitto atua Dodoma kuinadi ACT

comment yako inaonesha hujasoma hata thread yenyewe. ukisoma utalazimika ku-edit maana unajidhalilisha.

Watanzania wanataka kusikia habari ya Katiba mpya kama inafaa ama haifai, Tume huru ya uchaguzi, Uandikishwaji wa daftari la kudumu la wapiga kura na Uchaguzi mkuu mwezi October - sasa mtu mwingine eti anatanganza chama chake kipya!!

saccos yenu ya chagadomo imewadodea. na bado.


Teteteteh....siku hizi habari leo ina ripoti upinzani?.Si mnakatazwa kuripoti issues za upinzani?.Huyu zito mna ripoti kwa misingi gani?jibu mnalo waswahili,mafisadi.

Zitto kawashika vibaya. mmebaki kuweweseka. hiyo ni trela tu. picha yenyewe yaja.


Kwa Dodoma hawezi kutudanganya lolote aende zake Kigoma huko.dodoma hatutaki watu wanaoeneza udini na wanajisifia maisha yao.sisi na CCM au wengine UKAWA basi.
 
Usiangalie majina bali vyama hivyo vinasimamia nin?ni kweli CCM na Chadema kisera wanafanana, zinatofautiana majina tu.

Tumepata this time chama chenye misingi tofauti, ndio maana unaanza kusikia hoja zikianza kuongelewa.Ndio tunapaswa kwenda huku.

ACT ina aina ya siasa inayolifaa taifa letu, maana tukiwa na vyama uniform vinavyofanana kuna haja gan basi ya kuwa navyo?ACT kimekuja tofauti, turudi kwenye misingi.

Hakuna msing hapo bhana, msingi upi.Viongozi wote ACT yenu nini kipya wanaleta. Makaratasi sio utendaji kaka. Hapo mnashabikia matumbo yenu tu hakuna lolote fullstop
 
Maskini wee!! Too late yani.. Watu wako busy kutangaza nia sasa hivi wimbo wa kutambulisha chama hauimbiki tena
 
Kwa Dodoma hawezi kutudanganya lolote aende zake Kigoma huko.dodoma hatutaki watu wanaoeneza udini na wanajisifia maisha yao.sisi na CCM au wengine UKAWA basi.
Sema we we siyo sisi...why are you speaking before others..? Who are you?
 
Back
Top Bottom