Zitto aonyesha vitabu anavyosoma


Shule zikufunguliwa hakikisha hukosi kipindi cha English.
 

Kama ww unapenda mambo mapya unakitafuta cha nn hicho kitabu au ndo unataka uanzishe na ww cristo state au ccm state? Acha uongo kama hujasoma njoo shule……
 

Huo ni unafiki kk ww mbona unatuma hii txt kwenye mitandao ya kijamii unata tujue kama unatumia? Kama huelew unako enda na hutofika kama utafika bas kwa kuchelewa mno
 
Mwenye/ungekuwa na mawazo chanya ungeanza kuappreciate kabla ya kublame na kutoa ushauri na ndio maana nikakuambia una wivu.


Sikuanza na appreciation kwa kuwa hiyo ya kusoma vitabu vingi si habari kwangu kwa kuwa zitto mwenyewe amewahi kulizungumza hili kuwa muda mwingi anajisomea.Alieleza pia baadhi ya vitabu hivyo si jambo jipya jipya ni hizo picha ambazo zinaeleza hayo aliyowahi kueleza.Wakati mwingine huwa ananukuu statement za waandishi ama viongozi aliopata kuwasoma. Labda la muhimu ni kufahamu kuwa zito napenda challenge ingalikuwa ni yeye aliyesoma reply yangu asingalikuja na matusi angalileta argument au ku-appreciate challenge.Zitto ana ambition kubwa kuwa siku za baadae awe raisi wetu which is very good ,jukumu letu ni kumuandaa kwa kumkosoa bila unafiki nashukuru umri wake haukuruhusu kugombea uraisi hivyo kumpa nafasi zaidi ya kubadilika na atabadilika kwa kukosolewa. Mbowe alipokuwa anaomba kura kuwa raisi wa jamhuri mwaka 2010 nilimkosoa kwa kuongea kwa jazba bila vituo ila imechukua muda hadi kwa kiwango flani anaweza kutoa hoja na kumfanya msikilzaji aisikie vizuri na kuijadili.Dr Slaa ni mtu mzima kidogo hutegemewi kumbadili kirahisi lakini udhaifu wake upo kwenye attitude anahamaki ,pia si mtu nayeweza kucheza na fikra za anaowahutubia anashindwa ku relax hivyo kuwatia hofu baadhi ya wasikilizaji maana wanawaza huyu bwana akiwa amiri jeshi mkuu itakuwaje? Uchaguzi wa 2010 Jakaya Kikwete raisi wa sasa hali ilishamuwia ngumu yeye na chama chake ila wakabadilisha mfumo wa kampeni kwa namna ya maongezi jukwaani akishirikisha wagombea wa ngazi za chini mgombea ubunge na diwani. Mbunge na diwani wakitaja kero za mahala husika nae JK kwa ku relax japo moyoni alijua mwenyewe uwezekano mdogo wa utekelezaji akawa anatoa ahadi huku akiwa mpole anacheka anasisitiza inawezekana .Ni wachache walioelewa kuwa imekuwa hivyo kwa sababu gani.na leo utakuwa shaidi yangu juu ya hizo ahadi.Kwa hiyo ndugu yangu mi ni analyst tu si mshabiki najiweka huru ki fikra kama huyo zitto mwenyewe
 

Kwa sababu watanzania wengi sio wasomaji vitabu.
 
Eti vitabu anavyosoma.... So what??????!!!!!!

Hakuna kitu debe tupu haliachi kutika. Kwani kusoma vitabu na issue. Apeleke huko u bisho wake.

Hivi Sugu na Lema wanasoma vitabu gani?

... Kwani nani ambaye hasomi vitabu? Mwishowe mtatuonyesha hata choo anachokatia gogo

Sijaona hata kimoja chenye maana. Vyote ni history.Angejisomea tu " The Secrte"The master Key System nungemwelewa.Otherwise anakopi na kupaste mafanikio na makosa wengine Ulayani, Asia na Uislam

SUGU hana muda mchafu wa kusoma vitabu, yeye na GANJA, ganja na yeye.

Kwa jinsi hiyo mnavyo msifia mme wenu hata akionyesha choo anachotumia kunyea mtatuletea hapa ili tujadili jf


Hawa wanaosoma vitabu vingi ndo wanatuharibia nchi

Acheni wivu wa kike jamani!! si mzuri kwa afya zenu!! na kwenye ukweli tuseme ukweli... anastahili pongezi!!
 
Kiongozi wenu mkuu anasoma vitabu? Upeo wa ZZK unatokana na kusoma vitabu. Hata Nyerere alikuwa bookworm. Madiba hivyo hivyo. Ukitaka kumficha kiongozi fake habari yoyote, iweke kwenye kitabu!
 
Kwa chadema hicho kitabu cha Development in Germany Politics nadhani ndicho wanachokitumia zaidi kuliko vingine vyote.Wanakisoma kukikariri na kukitumia.Ndio maana hawaishi trip za Ujerumani.
Haha! Ngoja na mimi nikisome naweza pata trip za Ujerumani
 
Sasa mna uhakika kuwa kavisoma vyote au kavipanga tu ili kujipa ujiko?
 
Kuna namna nyingi za usomaji wa vitabu kuendana na malengo kwa kila kitabu inawezekana kusma vitabu 300kwa mwaka lakini ni vizuri sana ukasoma jounals na report mbalimbali pamoja na magazeti
 
Mwaka 2014 nimesoma vitabu 53 na nimefanya uchambuzi wa vitabu 21 kupitia safu ya Kitabu na Kalamu ya gazeti la Raia Tanzania kila Jumatatu.

Tangu nimeanza utaratibu kuchapisha idadi ya vitabu nilivyosoma huu ni mwaka wa tatu sasa. Mwaka 2012 nilisoma vitabu 31, mwaka 2013 vitabu 13 na 2014 vitabu 53.

Mwaka 2014 niliuanza kwa changamoto nyingi sana katika maisha yangu ya kisiasa; kuvuliwa nyadhifa katika chama na kuwa hatarini kuvuliwa uanachama kilichopelekea kwenda mahakam
ani kutetea uanachama wangu.

Vile vile kuanzia mwezi Machi nilianza kumwuguza mama yangu mzazi mpaka mungu alipomchukua hapo mwezi Juni. Muda mwingi niliutumia kusoma vitabu kama matibabu ya msongo ( therapy ).

Mchakato wa Katiba ( ambao sikushiriki kwa sababu ya kuona dhahiri hautaleta katiba bora ) pia ulinipa muda mzuri wa kufanya jambo ninalolipenda kuliko yote - Kusoma.

Kitabu kimoja ( ADAPT ) kimenifanya kubadili kabisa mtazamo wangu wa maisha. Vitabu 2 ( Exposure na Munyakei story ) vilinitia faraja kubwa katika kazi niliyokuwa nafanya tangu mwezi Machi ( uchunguzi wa akaunti ya ‪#‎TegetaEscrow‬ ).

Kitabu kimoja ( The myth of the strong leader ) kimepanua sana uwezo wangu katika kuchambua viongozi na mafanikio yao. Vyote nilifanikiwa kuvifanyia uchambuzi katika RaiaTanzania.

Bado India imechomoza sana katika orodha yangu. Miezi 2 niliyokaa Madras kumtibu mama imechangia sana kuongeza vitabu kutoka waandishi wa India. Vingi ni fiction. India Calling kilinivutia zaidi kuliko vyote.

Mwaka 2014 nimeanza kusoma kazi za ushairi za zamani ( Classics ) ili kupata maarifa mengi yaliyojaa kwenye ushairi na kuendeleza ujuzi wa kuandika mashairi.

Kitabu kimoja nilikianza nikashindwa kukimaliza, The Capital. Mungu akipenda nitakimaliza mwaka 2015. Karibu katika orodha yangu ya vitabu mwaka 2014
 
Na hii ndio tofauti ya mtu anayesoma na kuchukua hekima za waliopita, na yule anayetumia ujanja ujanja wa kupata udokta na uprofesa bila kusoma. There is no short-cut in life!
 
Hakuna kitu hapo kwami dunia hii niyeye ndio ansoma vitabu mbona hawapati huko na huko kujitangaza. Yeye huyu bwana ni mmafiki mkubwa na bahati yao CDM angeliwasambaratisha vibaya mno.
 
Uwe na muda na kipato cha uhakika ndio unaweza kufanya hayo !

Watanzania wengi wana akili sana, tena sio za kuishia kusoma vitabu, bali kuleta ideas mpya, ila tatizo hawajawezeshwa kama Zitto
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…