Zitto anafahamika kwa biashara ya siasa

Zitto anafahamika kwa biashara ya siasa

Albert Einstein

JF-Expert Member
Joined
Aug 24, 2017
Posts
394
Reaction score
583
Wasalaam

Na Galila Wabanh'u

Nimesoma makala ya Mhe Zitto Zubeir Kabwe mbunge wa Kigoma mjini akipotosha juu ya mradi wa bandari ya Bagamoyo kama moja ya mradi unaopaswa kutekelezwa katika eneo hilo pamoja na ujenzi wa reli yetu ya kisasa ya SGR.

Kwa wasiofahamu Ndugu Zitto anajulikana kwa kufanya “biashara” ya siasa. Yeye hulipwa ili kuwasemea “wanufaika” wa wanaotaka au wanaotekeleza miradi mbalimbali ya Serikali kwa ubia au wao wenyewe.

Tabia yake hii ameifanya kwenye kutoa taarifa za uongo kwa mataifa ya nje yenye nia isiyo ya wazi juu ya Taifa letu. Pia Ndugu Zitto akishirikiana na wenzake wa aina yake waliungana na kampuni iliyokuwa inayasimamia makampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Bulyanhulu, North Mara na Pangea (Buzwagi). Watu hawa walijaribu kumtisha Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwa uthubutu wake wa kuamua kuchunguza mikataba ya madini utalipelekea Taifa letu kushtakiwa na kuishia kulipa pesa nyingi, kufukuza wawekezaji na kugombana na mataifa makubwa na taasisi za kimataifa.

Waliyasema hayo hayo Mhe Rais Magufuli alipoagiza mapitio na uboreshaji wa mikataba ya kampuni ya mawasiliano ya Airtel, TICTS iliyopo bandarini, nk. Hata hivyo, mafanikio yaliyopatikana kwa uamuzi huu na hatimaye mapitio ya mikataba yote yamewaacha na aibu kubwa Zitto na kundi lake wanaomtumia.

Zitto huyu huyu na wenzake bila aibu wamekuwa pia wakitumika na makampuni ya kuchapisha noti duniani kuzunguka na kutoa rushwa ili wapate tenda mbalimbali kwenye benki kuu katika mataifa ya Afrika Mashariki.

Aidha, ni bahati mbaya kuwa Zitto na wenzake wanaendelea kutumika na wanyonyaji wa raslimali za nchi bila kung’amua kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli katika uchunguzi wa mikataba mbalimbali imegundua uchafu na madhaifu mengi ya kimikataba ambayo ndiyo iliyoifanya Serikali ya Awamu ya Tano “kushtuka” kuhusu rasimu ya mkataba wa Uendelezaji wa Eneo Maalum la Kiuchumi (Special Economic Zone - SEZ) pale Bagamoyo inayojumuisha ujenzi wa Bandari. Mradi huu uliokuwa utekelezwe na kampuni ya China Merchant Port ya jijini Shenzhen nchini China wakishirikiana na Mfuko wa Wakfu wa Oman.

Vipengele vilivyopendekezwa kwenye rasimu ya mkataba vingi ni vya kinyonyaji. Serikali imewaambia wawekezaji hawa kuwa vipengele vyenye ukakasi viondolewe ili mkataba uwe utakaowanufaisha pande zote mbili kwa maana ya mwekezaji na Taifa kama dhamira bado wanayo ya kutaka kushiriki kwenye mradi huo mkubwa wa Serikali vinginevyo haiwezekani.

Ni wenye nia ovu tu ndio wanaweza kubeza na kuona kuwa uamuzi huu wa serikali wa kusimamia raslimali za Taifa kwa maslahi ya wananchi wetu ni uamuzi mbaya usiofaa.

Ndugu Zitto amejaribu kueleza uamuzi wa baadhi ya nchi jirani kutekeleza baadhi ya miradi aliyoianisha ila ni muhimu kumkumbusha na kuwakumbusha watanzania kuwa tunaweza pia kujifunza kuwa sio maamuzi yote yanayofanywa na nchi jirani zetu au hata nchi nyinginezo ni uamuzi sahihi.

Mfano, Wakati nchi jirani ilipoamua kujenga reli ya kisasa ya kiwango cha SGR walijikuta wameingia mkataba mbovu ambao gharama za ujenzi ni kubwa sana karibu mara mbili za ujenzi ukilinganisha na SGR ya Tanzania, SGR yao ni ya kutumia mafuta aina ya Diesel, SGR yao treni inakimbia spidi ya kilomita 120 kwa saaukilinganisha na SGR ya Tanzania ambayo treni yake itatembea spidi ya kilomita 160 kwa saa nk.

Hivyo ni vizuri ndugu Zitto akaanzishe rasmi kampuni ya kibiashara itakayomuwezesha kufanya udalali wa kibiashara aachane na siasa au utumishi wa wananchi.

Siamini kama wananchi wa Kigoma anaowawakilisha wamemtuma kuhujumu Taifa badala ya kuungana na Serikali ya Awamu ya Tano kuwaletea maendeleo ya haraka wananchi wake wakiwemo wana-Kigoma La sivyo, wananchi wanaweza kukiona Chama cha ACT-Wazalendo kama mrija tu unaotumika kupitisha madili ya kiongozi wake bila wanachama wake kujua kuwa wanatumika kwa maslahi ya watu wachache.

#MimiNiMshindi
 
Huu muda watu wangetumia kufanya maendeleo au kuelezea nini kifanyike na sio fulani alichosema kifanyike ametumwa.., au fulani ni muongo bila kuweka uongo huo wazi.., tungekuwa mbali sana kama taifa..

Yaani fulani akiwa tofauti anahujumu Taifa.., na nyie msio hujumu mnafanya nini cha manufaa zaidi ya kuwa cheer leaders, lets talk about issues na sio people behind the issues...
 
Wanahitajika watu kama zitto au Tundu Lissu sana kwenye siasas...

Siyo wale wa ndiyo mzee peke yake....


Cc: mahondaw
 
Huna akili za Huyo uliyeiba jina.Kwanza huna uthibitisho wowote kuwa zitto anatumika.Kwanza umeandika mipasho huna hoja yoyote yaani wewe ni loser.

Zitto alitoa maoni yake kuhusu hiyo bandari na wewe ulipaswa kuja na hoja kupinga zile za zitto.Si kila mtu akitoa mawazo tofauti basi anatumiwa na mabeberu.

Kama hujui hata magufuli anaweza kuwa pandikizi la mabeberu wanaotumika kutunyonya ila kama huna jicho la tatu huwezi kuona hayo.

HAKUNA mwenys uhakika ikiwa SGR itazaa kile tulichokitarajia au ule mradi wa umeme rufiji.,kama tuliaminishwa kuwa gesi ni mkombozi wetu na hadi leo hatujakomboka bado tuko kwenye umaskini kosa ni la nani?

Kwa kukosa diplomasia imara ina maana hao wajenzi wameshindwa kukaa meza na serikali?

Itakuwaje kama bandari ya Lamu ikashika hatamu EA coast na bandari ya Dar ikafa kifo cha mende nani alaumiwe?Mi nasubiri mafanikio ya bandari ya Lamu kisha nione kweli aliyoongea zitto ni kweli au ni uongo
 
*ZITTO ANAFAHAMIKA KWA BIASHARA YA SIASA*

Na Galila Wabanh'u

nimesoma makala ya Mhe Zitto Zubeir Kabwe mbunge wa Kigoma mjini akipotosha juu ya mradi wa bandari ya Bagamoyo kama moja ya mradi unaopaswa kutekelezwa katika eneo hilo pamoja na ujenzi wa reli yetu ya kisasa ya SGR.

Kwa wasiofahamu Ndugu Zitto anajulikana kwa kufanya “biashara” ya siasa. Yeye hulipwa ili kuwasemea “wanufaika” wa wanaotaka au wanaotekeleza miradi mbalimbali ya Serikali kwa ubia au wao wenyewe.

Tabia yake hii ameifanya kwenye kutoa taarifa za uongo kwa mataifa ya nje yenye nia isiyo ya wazi juu ya Taifa letu. Pia Ndugu Zitto akishirikiana na wenzake wa aina yake waliungana na kampuni iliyokuwa inayasimamia makampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Bulyanhulu, North Mara na Pangea (Buzwagi). Watu hawa walijaribu kumtisha Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwa uthubutu wake wa kuamua kuchunguza mikataba ya madini utalipelekea Taifa letu kushtakiwa na kuishia kulipa pesa nyingi, kufukuza wawekezaji na kugombana na mataifa makubwa na taasisi za kimataifa.

Waliyasema hayo hayo Mhe Rais Magufuli alipoagiza mapitio na uboreshaji wa mikataba ya kampuni ya mawasiliano ya Airtel, TICTS iliyopo bandarini, nk. Hata hivyo, mafanikio yaliyopatikana kwa uamuzi huu na hatimaye mapitio ya mikataba yote yamewaacha na aibu kubwa Zitto na kundi lake wanaomtumia.

Zitto huyu huyu na wenzake bila aibu wamekuwa pia wakitumika na makampuni ya kuchapisha noti duniani kuzunguka na kutoa rushwa ili wapate tenda mbalimbali kwenye benki kuu katika mataifa ya Afrika Mashariki.

Aidha, ni bahati mbaya kuwa Zitto na wenzake wanaendelea kutumika na wanyonyaji wa raslimali za nchi bila kung’amua kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli katika uchunguzi wa mikataba mbalimbali imegundua uchafu na madhaifu mengi ya kimikataba ambayo ndiyo iliyoifanya Serikali ya Awamu ya Tano “kushtuka” kuhusu rasimu ya mkataba wa Uendelezaji wa Eneo Maalum la Kiuchumi (Special Economic Zone - SEZ) pale Bagamoyo inayojumuisha ujenzi wa Bandari. Mradi huu uliokuwa utekelezwe na kampuni ya China Merchant Port ya jijini Shenzhen nchini China wakishirikiana na Mfuko wa Wakfu wa Oman.

Vipengele vilivyopendekezwa kwenye rasimu ya mkataba vingi ni vya kinyonyaji. Serikali imewaambia wawekezaji hawa kuwa vipengele vyenye ukakasi viondolewe ili mkataba uwe utakaowanufaisha pande zote mbili kwa maana ya mwekezaji na Taifa kama dhamira bado wanayo ya kutaka kushiriki kwenye mradi huo mkubwa wa Serikali vinginevyo haiwezekani.

Ni wenye nia ovu tu ndio wanaweza kubeza na kuona kuwa uamuzi huu wa serikali wa kusimamia raslimali za Taifa kwa maslahi ya wananchi wetu ni uamuzi mbaya usiofaa.

Ndugu Zitto amejaribu kueleza uamuzi wa baadhi ya nchi jirani kutekeleza baadhi ya miradi aliyoianisha ila ni muhimu kumkumbusha na kuwakumbusha watanzania kuwa tunaweza pia kujifunza kuwa sio maamuzi yote yanayofanywa na nchi jirani zetu au hata nchi nyinginezo ni uamuzi sahihi.

Mfano, Wakati nchi jirani ilipoamua kujenga reli ya kisasa ya kiwango cha SGR walijikuta wameingia mkataba mbovu ambao gharama za ujenzi ni kubwa sana karibu mara mbili za ujenzi ukilinganisha na SGR ya Tanzania, SGR yao ni ya kutumia mafuta aina ya Diesel, SGR yao treni inakimbia spidi ya kilomita 120 kwa saaukilinganisha na SGR ya Tanzania ambayo treni yake itatembea spidi ya kilomita 160 kwa saa nk.

Hivyo ni vizuri ndugu Zitto akaanzishe rasmi kampuni ya kibiashara itakayomuwezesha kufanya udalali wa kibiashara aachane na siasa au utumishi wa wananchi.

Siamini kama wananchi wa Kigoma anaowawakilisha wamemtuma kuhujumu Taifa badala ya kuungana na Serikali ya Awamu ya Tano kuwaletea maendeleo ya haraka wananchi wake wakiwemo wana-Kigoma La sivyo, wananchi wanaweza kukiona Chama cha ACT-Wazalendo kama mrija tu unaotumika kupitisha madili ya kiongozi wake bila wanachama wake kujua kuwa wanatumika kwa maslahi ya watu wachache.


C&P
 
Wasalaam

Na Galila Wabanh'u

Nimesoma makala ya Mhe Zitto Zubeir Kabwe mbunge wa Kigoma mjini akipotosha juu ya mradi wa bandari ya Bagamoyo kama moja ya mradi unaopaswa kutekelezwa katika eneo hilo pamoja na ujenzi wa reli yetu ya kisasa ya SGR.

Kwa wasiofahamu Ndugu Zitto anajulikana kwa kufanya “biashara” ya siasa. Yeye hulipwa ili kuwasemea “wanufaika” wa wanaotaka au wanaotekeleza miradi mbalimbali ya Serikali kwa ubia au wao wenyewe.

Tabia yake hii ameifanya kwenye kutoa taarifa za uongo kwa mataifa ya nje yenye nia isiyo ya wazi juu ya Taifa letu. Pia Ndugu Zitto akishirikiana na wenzake wa aina yake waliungana na kampuni iliyokuwa inayasimamia makampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Bulyanhulu, North Mara na Pangea (Buzwagi). Watu hawa walijaribu kumtisha Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwa uthubutu wake wa kuamua kuchunguza mikataba ya madini utalipelekea Taifa letu kushtakiwa na kuishia kulipa pesa nyingi, kufukuza wawekezaji na kugombana na mataifa makubwa na taasisi za kimataifa.

Waliyasema hayo hayo Mhe Rais Magufuli alipoagiza mapitio na uboreshaji wa mikataba ya kampuni ya mawasiliano ya Airtel, TICTS iliyopo bandarini, nk. Hata hivyo, mafanikio yaliyopatikana kwa uamuzi huu na hatimaye mapitio ya mikataba yote yamewaacha na aibu kubwa Zitto na kundi lake wanaomtumia.

Zitto huyu huyu na wenzake bila aibu wamekuwa pia wakitumika na makampuni ya kuchapisha noti duniani kuzunguka na kutoa rushwa ili wapate tenda mbalimbali kwenye benki kuu katika mataifa ya Afrika Mashariki.

Aidha, ni bahati mbaya kuwa Zitto na wenzake wanaendelea kutumika na wanyonyaji wa raslimali za nchi bila kung’amua kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli katika uchunguzi wa mikataba mbalimbali imegundua uchafu na madhaifu mengi ya kimikataba ambayo ndiyo iliyoifanya Serikali ya Awamu ya Tano “kushtuka” kuhusu rasimu ya mkataba wa Uendelezaji wa Eneo Maalum la Kiuchumi (Special Economic Zone - SEZ) pale Bagamoyo inayojumuisha ujenzi wa Bandari. Mradi huu uliokuwa utekelezwe na kampuni ya China Merchant Port ya jijini Shenzhen nchini China wakishirikiana na Mfuko wa Wakfu wa Oman.

Vipengele vilivyopendekezwa kwenye rasimu ya mkataba vingi ni vya kinyonyaji. Serikali imewaambia wawekezaji hawa kuwa vipengele vyenye ukakasi viondolewe ili mkataba uwe utakaowanufaisha pande zote mbili kwa maana ya mwekezaji na Taifa kama dhamira bado wanayo ya kutaka kushiriki kwenye mradi huo mkubwa wa Serikali vinginevyo haiwezekani.

Ni wenye nia ovu tu ndio wanaweza kubeza na kuona kuwa uamuzi huu wa serikali wa kusimamia raslimali za Taifa kwa maslahi ya wananchi wetu ni uamuzi mbaya usiofaa.

Ndugu Zitto amejaribu kueleza uamuzi wa baadhi ya nchi jirani kutekeleza baadhi ya miradi aliyoianisha ila ni muhimu kumkumbusha na kuwakumbusha watanzania kuwa tunaweza pia kujifunza kuwa sio maamuzi yote yanayofanywa na nchi jirani zetu au hata nchi nyinginezo ni uamuzi sahihi.

Mfano, Wakati nchi jirani ilipoamua kujenga reli ya kisasa ya kiwango cha SGR walijikuta wameingia mkataba mbovu ambao gharama za ujenzi ni kubwa sana karibu mara mbili za ujenzi ukilinganisha na SGR ya Tanzania, SGR yao ni ya kutumia mafuta aina ya Diesel, SGR yao treni inakimbia spidi ya kilomita 120 kwa saaukilinganisha na SGR ya Tanzania ambayo treni yake itatembea spidi ya kilomita 160 kwa saa nk.

Hivyo ni vizuri ndugu Zitto akaanzishe rasmi kampuni ya kibiashara itakayomuwezesha kufanya udalali wa kibiashara aachane na siasa au utumishi wa wananchi.

Siamini kama wananchi wa Kigoma anaowawakilisha wamemtuma kuhujumu Taifa badala ya kuungana na Serikali ya Awamu ya Tano kuwaletea maendeleo ya haraka wananchi wake wakiwemo wana-Kigoma La sivyo, wananchi wanaweza kukiona Chama cha ACT-Wazalendo kama mrija tu unaotumika kupitisha madili ya kiongozi wake bila wanachama wake kujua kuwa wanatumika kwa maslahi ya watu wachache.

#MimiNiMshindi
Hii story ndefu lakini ya kijinga jinga na mwandishi ni mtu mwenye upeo mdogo IQ ndogo sana, kaa ukijua kuwa watanzania wapo makini wanajua ukweli wote wanajua mabaya yenu na huu ujinga mnaofanya, hakuna mtu mwenye Uelewa wa kutosha anaweza kukaa kusoma ulivyoviandika kisha aviweke kichwani, vyote ubakie navyo na wajinga wenzako lakini wenye kujielewa wanajua Profesa Assad alikuwa mwiba mchungu dhidi ya ufisadi unaofanywa na wanaojiita wazalendo, mshukuru mungu Assad kaondoka pasipo kuikagua wizara ya miundo mbinu maana pengine angekagua mahesabu yao ingekuwa Aibu ya karne,
 
Huu muda watu wangetumia kufanya maendeleo au kuelezea nini kifanyike na sio fulani alichosema kifanyike ametumwa.., au fulani ni muongo bila kuweka uongo huo wazi.., tungekuwa mbali sana kama taifa..

Yaani fulani akiwa tofauti anahujumu Taifa.., na nyie msio hujumu mnafanya nini cha manufaa zaidi ya kuwa cheer leaders, lets talk about issues na sio people behind the issues...
Nchi hii imekosa maendeleo kwa kuukumbatia ujinga mwingi usio na kikomo, mleta mada ni mmojawapo wa wajinga wanaoamini kila kitokacho kwa magufuli hutoka mwa mungu na magufuli ni malaika mtakatifu halosei
 
*ZITTO ANAFAHAMIKA KWA BIASHARA YA SIASA*

Na Galila Wabanh'u

nimesoma makala ya Mhe Zitto Zubeir Kabwe mbunge wa Kigoma mjini akipotosha juu ya mradi wa bandari ya Bagamoyo kama moja ya mradi unaopaswa kutekelezwa katika eneo hilo pamoja na ujenzi wa reli yetu ya kisasa ya SGR.

Kwa wasiofahamu Ndugu Zitto anajulikana kwa kufanya “biashara” ya siasa. Yeye hulipwa ili kuwasemea “wanufaika” wa wanaotaka au wanaotekeleza miradi mbalimbali ya Serikali kwa ubia au wao wenyewe.

Tabia yake hii ameifanya kwenye kutoa taarifa za uongo kwa mataifa ya nje yenye nia isiyo ya wazi juu ya Taifa letu. Pia Ndugu Zitto akishirikiana na wenzake wa aina yake waliungana na kampuni iliyokuwa inayasimamia makampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Bulyanhulu, North Mara na Pangea (Buzwagi). Watu hawa walijaribu kumtisha Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwa uthubutu wake wa kuamua kuchunguza mikataba ya madini utalipelekea Taifa letu kushtakiwa na kuishia kulipa pesa nyingi, kufukuza wawekezaji na kugombana na mataifa makubwa na taasisi za kimataifa.

Waliyasema hayo hayo Mhe Rais Magufuli alipoagiza mapitio na uboreshaji wa mikataba ya kampuni ya mawasiliano ya Airtel, TICTS iliyopo bandarini, nk. Hata hivyo, mafanikio yaliyopatikana kwa uamuzi huu na hatimaye mapitio ya mikataba yote yamewaacha na aibu kubwa Zitto na kundi lake wanaomtumia.

Zitto huyu huyu na wenzake bila aibu wamekuwa pia wakitumika na makampuni ya kuchapisha noti duniani kuzunguka na kutoa rushwa ili wapate tenda mbalimbali kwenye benki kuu katika mataifa ya Afrika Mashariki.

Aidha, ni bahati mbaya kuwa Zitto na wenzake wanaendelea kutumika na wanyonyaji wa raslimali za nchi bila kung’amua kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli katika uchunguzi wa mikataba mbalimbali imegundua uchafu na madhaifu mengi ya kimikataba ambayo ndiyo iliyoifanya Serikali ya Awamu ya Tano “kushtuka” kuhusu rasimu ya mkataba wa Uendelezaji wa Eneo Maalum la Kiuchumi (Special Economic Zone - SEZ) pale Bagamoyo inayojumuisha ujenzi wa Bandari. Mradi huu uliokuwa utekelezwe na kampuni ya China Merchant Port ya jijini Shenzhen nchini China wakishirikiana na Mfuko wa Wakfu wa Oman.

Vipengele vilivyopendekezwa kwenye rasimu ya mkataba vingi ni vya kinyonyaji. Serikali imewaambia wawekezaji hawa kuwa vipengele vyenye ukakasi viondolewe ili mkataba uwe utakaowanufaisha pande zote mbili kwa maana ya mwekezaji na Taifa kama dhamira bado wanayo ya kutaka kushiriki kwenye mradi huo mkubwa wa Serikali vinginevyo haiwezekani.

Ni wenye nia ovu tu ndio wanaweza kubeza na kuona kuwa uamuzi huu wa serikali wa kusimamia raslimali za Taifa kwa maslahi ya wananchi wetu ni uamuzi mbaya usiofaa.

Ndugu Zitto amejaribu kueleza uamuzi wa baadhi ya nchi jirani kutekeleza baadhi ya miradi aliyoianisha ila ni muhimu kumkumbusha na kuwakumbusha watanzania kuwa tunaweza pia kujifunza kuwa sio maamuzi yote yanayofanywa na nchi jirani zetu au hata nchi nyinginezo ni uamuzi sahihi.

Mfano, Wakati nchi jirani ilipoamua kujenga reli ya kisasa ya kiwango cha SGR walijikuta wameingia mkataba mbovu ambao gharama za ujenzi ni kubwa sana karibu mara mbili za ujenzi ukilinganisha na SGR ya Tanzania, SGR yao ni ya kutumia mafuta aina ya Diesel, SGR yao treni inakimbia spidi ya kilomita 120 kwa saaukilinganisha na SGR ya Tanzania ambayo treni yake itatembea spidi ya kilomita 160 kwa saa nk.

Hivyo ni vizuri ndugu Zitto akaanzishe rasmi kampuni ya kibiashara itakayomuwezesha kufanya udalali wa kibiashara aachane na siasa au utumishi wa wananchi.

Siamini kama wananchi wa Kigoma anaowawakilisha wamemtuma kuhujumu Taifa badala ya kuungana na Serikali ya Awamu ya Tano kuwaletea maendeleo ya haraka wananchi wake wakiwemo wana-Kigoma La sivyo, wananchi wanaweza kukiona Chama cha ACT-Wazalendo kama mrija tu unaotumika kupitisha madili ya kiongozi wake bila wanachama wake kujua kuwa wanatumika kwa maslahi ya watu wachache.


C&P
Haya yako hayana uhusiano na huu ujinga aliofanyiwa CAG, point je? Alichofanyiwa CAG ni sawa? Kumtoa mtu ofisini kisa aliwaumbua juu ta tr 1.5 na kumuumbua Ndungai kwa ufujaji ofisi bunge vina uhusiano gani na Zito? Acheni uongo Dunia hii ya sasa kila mmoja anajua kupima mabaya na mazuri
 
Wasalaam

Na Galila Wabanh'u

Nimesoma makala ya Mhe Zitto Zubeir Kabwe mbunge wa Kigoma mjini akipotosha juu ya mradi wa bandari ya Bagamoyo kama moja ya mradi unaopaswa kutekelezwa katika eneo hilo pamoja na ujenzi wa reli yetu ya kisasa ya SGR.

Kwa wasiofahamu Ndugu Zitto anajulikana kwa kufanya “biashara” ya siasa. Yeye hulipwa ili kuwasemea “wanufaika” wa wanaotaka au wanaotekeleza miradi mbalimbali ya Serikali kwa ubia au wao wenyewe.

Tabia yake hii ameifanya kwenye kutoa taarifa za uongo kwa mataifa ya nje yenye nia isiyo ya wazi juu ya Taifa letu. Pia Ndugu Zitto akishirikiana na wenzake wa aina yake waliungana na kampuni iliyokuwa inayasimamia makampuni ya uchimbaji madini ya dhahabu ya Bulyanhulu, North Mara na Pangea (Buzwagi). Watu hawa walijaribu kumtisha Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kuwa uthubutu wake wa kuamua kuchunguza mikataba ya madini utalipelekea Taifa letu kushtakiwa na kuishia kulipa pesa nyingi, kufukuza wawekezaji na kugombana na mataifa makubwa na taasisi za kimataifa.

Waliyasema hayo hayo Mhe Rais Magufuli alipoagiza mapitio na uboreshaji wa mikataba ya kampuni ya mawasiliano ya Airtel, TICTS iliyopo bandarini, nk. Hata hivyo, mafanikio yaliyopatikana kwa uamuzi huu na hatimaye mapitio ya mikataba yote yamewaacha na aibu kubwa Zitto na kundi lake wanaomtumia.

Zitto huyu huyu na wenzake bila aibu wamekuwa pia wakitumika na makampuni ya kuchapisha noti duniani kuzunguka na kutoa rushwa ili wapate tenda mbalimbali kwenye benki kuu katika mataifa ya Afrika Mashariki.

Aidha, ni bahati mbaya kuwa Zitto na wenzake wanaendelea kutumika na wanyonyaji wa raslimali za nchi bila kung’amua kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Mhe Rais Dkt John Pombe Magufuli katika uchunguzi wa mikataba mbalimbali imegundua uchafu na madhaifu mengi ya kimikataba ambayo ndiyo iliyoifanya Serikali ya Awamu ya Tano “kushtuka” kuhusu rasimu ya mkataba wa Uendelezaji wa Eneo Maalum la Kiuchumi (Special Economic Zone - SEZ) pale Bagamoyo inayojumuisha ujenzi wa Bandari. Mradi huu uliokuwa utekelezwe na kampuni ya China Merchant Port ya jijini Shenzhen nchini China wakishirikiana na Mfuko wa Wakfu wa Oman.

Vipengele vilivyopendekezwa kwenye rasimu ya mkataba vingi ni vya kinyonyaji. Serikali imewaambia wawekezaji hawa kuwa vipengele vyenye ukakasi viondolewe ili mkataba uwe utakaowanufaisha pande zote mbili kwa maana ya mwekezaji na Taifa kama dhamira bado wanayo ya kutaka kushiriki kwenye mradi huo mkubwa wa Serikali vinginevyo haiwezekani.

Ni wenye nia ovu tu ndio wanaweza kubeza na kuona kuwa uamuzi huu wa serikali wa kusimamia raslimali za Taifa kwa maslahi ya wananchi wetu ni uamuzi mbaya usiofaa.

Ndugu Zitto amejaribu kueleza uamuzi wa baadhi ya nchi jirani kutekeleza baadhi ya miradi aliyoianisha ila ni muhimu kumkumbusha na kuwakumbusha watanzania kuwa tunaweza pia kujifunza kuwa sio maamuzi yote yanayofanywa na nchi jirani zetu au hata nchi nyinginezo ni uamuzi sahihi.

Mfano, Wakati nchi jirani ilipoamua kujenga reli ya kisasa ya kiwango cha SGR walijikuta wameingia mkataba mbovu ambao gharama za ujenzi ni kubwa sana karibu mara mbili za ujenzi ukilinganisha na SGR ya Tanzania, SGR yao ni ya kutumia mafuta aina ya Diesel, SGR yao treni inakimbia spidi ya kilomita 120 kwa saaukilinganisha na SGR ya Tanzania ambayo treni yake itatembea spidi ya kilomita 160 kwa saa nk.

Hivyo ni vizuri ndugu Zitto akaanzishe rasmi kampuni ya kibiashara itakayomuwezesha kufanya udalali wa kibiashara aachane na siasa au utumishi wa wananchi.

Siamini kama wananchi wa Kigoma anaowawakilisha wamemtuma kuhujumu Taifa badala ya kuungana na Serikali ya Awamu ya Tano kuwaletea maendeleo ya haraka wananchi wake wakiwemo wana-Kigoma La sivyo, wananchi wanaweza kukiona Chama cha ACT-Wazalendo kama mrija tu unaotumika kupitisha madili ya kiongozi wake bila wanachama wake kujua kuwa wanatumika kwa maslahi ya watu wachache.

#MimiNiMshindi
mkuu. Umeandika kitu gani ? Unamshambulia Zitto au unajibu hoja zake ? Kumshambulia Zitto kuna faida gani kwa taifa ? Kwanini usingejibu hoja zake kama ni mwongo ? Hoja ipingwe na hoja iliyo bora zaid sio bla bla bla
 
Back
Top Bottom