Josh Michael
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,523
- 77
Sawa kabisa mzee maana PM wako siku hizi kauli zake zina utata mkubwa sana, tunashindwa kumuelewa hata kidogo, maana hata aseme vipi bado tunaendelea kuona kuwa CCM wanabaka demokrasia Tanzania
Mkuu huko kubandikwa jina "mtoto wa mkulima" unadhani ni kwa sababu gani? Si kwa sababu waziri mkuu aliyetoka Edward Lowassa alikuwa na skendo kibao na kila mtu alikuwa anajua ni tajiri sana. Sasa kumchagua Pinda ili kumtofautisha na EL ndiyo hiyo kupachikwa "mtoto wa mkulima" ili watu waone nae ni mwananchi wa kawaida. Kwa mshahara wa wabunge na mirupurupu mingine unadhani kuna mtoto wa mkulima mule? Yote ilikuwa tu politics ya kumuuza Pinda kwa wananchi.
Hujanielewa ambaye hashauriki ni Zito siyo waziri mkuu huyo Zito wenu ameisha sema kuwa anamheshimu Pinda kifaa bwana acha majungu
Miye nadhani huyu Zitto anapewa umaarufu ambao hata haumstahili. Zitto amepewa kichwa tu kutokana na kuwa msemaji kwa jazba ndani ya Bunge etc lakini hana upeo wowote mkubwa kisiasa kuweza kumjibu Waziri Mkuu kama ilivyoelezwa na mwandishi wa habari hiyo!
Eti:
Kuhusu Pinda kunishambulia bungeni jana kauli yangu ni hii. Ninamheshimu sana Pinda na sitaki malumbano nae. Namshauri atazame kauli zake maana zinapelekea watu makini waanze kuhoji uelewa wake wa demokrasia, alisema Zitto.
Hivi kweli kati ya Pinda na Zitto nani anayeelewa zaidi demokrasia kuzidi mwenziwe?!
Hilo lekundu sio kweli. Hayo mengine ni mawazo yako na ninayaheshimu.