Zitto akataa posho ya mil. 238

Zitto akataa posho ya mil. 238

Dah zitto kaka umewashika watu pabaya jamaa wana chuki lkn umewaacha kilimetre mia
 
Wapi alipokataa? Yeye ni sawa na anayesema hali nguruwe ila mchuzi wake tu. Chichidodo!
 
Bavicha kwakujitoa ufaham bwana!
Posho hizo ni kwa mujibu wa sheria so atapokea maana ni mafao kwa mujibu wa sheria ......awadanganye wajinga , zile za posho alisema hatapokea mara atapelekea kwenye NGO yake huko Kigoma , muulizeni ziko wapi ? NGO yake ilipokea ngapi? Mnafiki sana huyu ....
 
Zitto, anasema atachukua zile anazostahili kwa mujibu wa sheria , sasa yeye ambazo hastahili ni ngapi? Vipi kuhusu posho ya kukaa ambayoalisema aliacha kuchukua , mbona aliendelea kuchukua ?
acha chuki binafsi mkuu iyo posho una ushahidi anachukua, mbona rahisi kujua anazo stahli ni zile za mwanzo alipojiuzuru ubunge hizi 230 zinazotaka kusainiwa ndo atapeleka aliposema. HUYU NDO MZALENDO WA KWELI.
 
This is very Personal to me,
Binafsi nimekuwa nikimkubali ZZK,he has always been and will always remain my Political hero.Lakini katika hili haitoshi tu kutuambia kitakachozidi utakipeleka huko ulikosema,tunahitaji baada ya malipo kufanyika uje na ushahidi ulio wazi kama sera ya ACT inavosema ambayo utaonyesha Transaction zote zilivofanyika kuhusu hiyo hela iliyozidi na ulivyoipeleka kusaidia hizo sehemu husika na uzisimamie zitumike kwa malengo uliyoyasema,kinyume na hivi ndugu ZZK utakuwa sawa na Mbowe ambaye ameichukua na kula Kimya.
 
Hayo ndio majibu ya Zitto tunaemjua,sio yale majibu yakupikwa na Bavicha!Huyu Zitto mungu hatomwacha daima kwakuwa sio mnafiki kama wakina Mbowe aliojifanya wanakana gari la KUB but mpaka sasa anatesea na vimada wake!
By Zitto,

Juzi nilipokuwa jijini Mbeya niliulizwa na wananchi iwapo nami nitachukua kiinua mgongo cha tshs 238 milioni kitakacholipwa kwa wabunge. Nimewajibu kuwa msimamo wangu upo wazi kwenye masuala haya.

Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua. Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka kusaidia ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi Shule ya Buhangija na Hospitali ya Saratani ya Ocean Road. Buhangija nilitembelea mwezi Aprili na kukuta watoto wanalala kwa shida sana.

Niliamua kusaidia juhudi zinazofanywa na Miss. Tanzania Briggite Alfred ambaye anajenga Bweni pale. Ocean Road ni mchango wangu katika kusaidia wagonjwa wa saratani, ugonjwa uliomchukua mama yangu Hajjat Shida Salum.

Source: His facebook page.

Huyu Zitto kweli ni akili kubwa. Muda si mrefu wanafiki na wapenda sifa nao wataanza kumuiga, japo moyoni hawapendi kuachia hiyo mihela.

 
Masikin Bavichaa mwaka huu mnalo!
Aseme anazostahili kwa mujibu wa sheria ni ngapi? Mbona yeye analipwa wakati alifukuzwa kwenye chama chake na kuukosa Ubunge ? Mbona mpaka leo akina Danny Makanga na Erasto Tumbo , tangu walipofukuzwa UDP hawajawahi kulipwa mafao yao ? yeye analipwakwa utaratibu upi?
 
huo sio uzalendo, ni kuwapumbaza wasioelewa siasa anazofanya, yeye anapokea pesa nyingi Zaidi ya hizo, ukweli utakuja julikana tu ngoja tusubiri, ila kama ni pesa kwa mujibu wa sharia siwezi kumlaumu anayepokea, ni pesa halali kisheria.
 
Zitto anapenda sana kujadiliwa...

Iwe kwa baya au zuri....

Ndio sababu ana msururu wa ID mbalimbali anazotumia kuanzisha maada kila baada ya masaa kadhaa...

Sasa katika bandiko lake hilo wapi amesema hatachukua hiyo pesa??

Huyu mtu ndio sababu Muhongo alimtaja kama kijana mmoja mlafi sana wa sifa na rushwa...
 
Last edited by a moderator:
Hivi Mbunge aliyefukuzwa ubunge anasitahili kupata kiinua mgongo cha ubunge in the first place?

Maana huenda hata hicho kidogo anachodai huenda hasitahili, anasitahili kupata ZERO SHILINGI.

I reckon Mpendazoe alipoacha ubunge 2010, hakupewa kiinua mgongo. Inakuwaje Zitto yeye apewe. Kama ni suala la sheria na principle Zitto anatakiwa kukataa hata kidogo hicho atakachochukua.

Kwani Zitto anafahamu fika kwamba ma-CCM YAMEPINDISHA SHERIA kumpatia kiinua mgongo wakati hasitahili kwa mujibu wa sheria.
 
Hilo unalijua ww mkuu! Mbowe na Lissu hawalijui hilo bali wanachekelea tu mihela!
Kwa nini walipwe mahela mengi namna hiyo?

Kwa nini hayo mahela yasitumiwe kwenye mambo mengine yaliyo muhimu zaidi kuliko matumbo ya hao wabunge?
 
Hivi Mbunge aliyefukuzwa ubunge anasitahili kupata kiinua mgongo cha ubunge in the first place?

Maana huenda hata hicho kidogo anachodai huenda hasitahili, anasitahili kupata ZERO SHILINGI.

I reckon Mpendazoe alipoacha ubunge 2010, hakupewa kiinua mgongo. Inakuwaje Zitto yeye apewe. Kama ni suala la sheria na principle Zitto anatakiwa kukataa hata kidogo hicho atakachopewa.

Kwani Zitto anafahamu fika kwamba ma-CMM YAMEPINDISHA SHERIA kumpatia kiinua mgongo wakati hasitahili kwa mujibu wa sheria.
Nakubaliana na wewe
 
Dah! Kwani lazima kutumia Kimombo?Lugaha za watu hizo zimekuja na majahazi msizidandie!
jamani hamjamuekewa zzt,kasema fedha zoto za ziada.
sasa kwenye hiyo amount ya 238 atuambie za ziada ni ngapi?
Au hizo 238 zote ni za ziada ??
zitto you can fool some people some time but you can't fool all the all the times.
kawadanganye mwandiga na lwiche sio humu.
 
By Zitto,

Juzi nilipokuwa jijini Mbeya niliulizwa na wananchi iwapo nami nitachukua kiinua mgongo cha tshs 238 milioni kitakacholipwa kwa wabunge. Nimewajibu kuwa msimamo wangu upo wazi kwenye masuala haya.

Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua. Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka kusaidia ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi Shule ya Buhangija na Hospitali ya Saratani ya Ocean Road. Buhangija nilitembelea mwezi Aprili na kukuta watoto wanalala kwa shida sana.

Niliamua kusaidia juhudi zinazofanywa na Miss. Tanzania Briggite Alfred ambaye anajenga Bweni pale. Ocean Road ni mchango wangu katika kusaidia wagonjwa wa saratani, ugonjwa uliomchukua mama yangu Hajjat Shida Salum.

Source: His facebook page.

Huyu Zitto kweli ni akili kubwa. Muda si mrefu wanafiki na wapenda sifa nao wataanza kumuiga, japo moyoni hawapendi kuachia hiyo mihela.


Kwa hili nampongeza
 
Bavicha mnakazi kubwa mnooooooooooo!kila mkiona jina la Zitto hata kama mnaku.nya lazima mtaacha ili muwahi kuja kurusha ngumi JF!
Akiwa anatoa msaada atasema zimetoka wapi?Lazima atajibu kwenye mafao yangu au?Anatafuta sifa kwa fedha anazoziita haramu.

Wengine tumechoka kudanganywa.Alisema mwenyewe msituamini wanasiasa,ni kweli waongo kwa asilimia 100.
 
Kwa nini uchukue kitu ambacho ni cha ziada ...kinyume cha sheria?
 
  • Thanks
Reactions: Pai
Posho hizo ni kwa mujibu wa sheria so atapokea maana ni mafao kwa mujibu wa sheria ......awadanganye wajinga , zile za posho alisema hatapokea mara atapelekea kwenye NGO yake huko Kigoma , muulizeni ziko wapi ? NGO yake ilipokea ngapi? Mnafiki sana huyu ....
Sasa si kasema ziada hachukui au ulitaka hata haki yake agomee??!!!
 
Back
Top Bottom