Zitto akataa posho ya mil. 238

Zitto akataa posho ya mil. 238

By Zitto,

Juzi nilipokuwa jijini Mbeya niliulizwa na wananchi iwapo nami nitachukua kiinua mgongo cha tshs 238 milioni kitakacholipwa kwa wabunge. Nimewajibu kuwa msimamo wangu upo wazi kwenye masuala haya.

Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua. Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka kusaidia ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi Shule ya Buhangija na Hospitali ya Saratani ya Ocean Road. Buhangija nilitembelea mwezi Aprili na kukuta watoto wanalala kwa shida sana.

Niliamua kusaidia juhudi zinazofanywa na Miss. Tanzania Briggite Alfred ambaye anajenga Bweni pale. Ocean Road ni mchango wangu katika kusaidia wagonjwa wa saratani, ugonjwa uliomchukua mama yangu Hajjat Shida Salum.

Source: His facebook page.

Huyu Zitto kweli ni akili kubwa. Muda si mrefu wanafiki na wapenda sifa nao wataanza kumuiga, japo moyoni hawapendi kuachia hiyo mihela.

Nadhani mtu huyu ni mjanja wakisiasa mpaka unaweza ukafikiri ana uzalendo wowote.Nijuavyo mimi he is in a process of fighting for his political life.Yuko katika hali ya kumalizika kisiasa kabisa muoneeni huruma
 
Mpuuzi kabis huyu ZZK. ili azigawe huko ocean rd na kwenye ujenzi wa hilo bweni la wasichana si lazima azipokee??
Kawadanganye shangazi zako wa mwandiga na sio hapa.
 
Zitto kwa hili nitakupongeza bila kujali mapungufu yako au makosa yako na wala sitasubiri mpaka siku utangulie mbele ya haki ndio niseme.

Hata hivyo,huna budi kututhibitishia ni kiasi gani umechukua na kiasi gani umepeleka kusaidi hizo huduma za jamii.Ukishindwa kuthibitisha hili ujue utaendelea kujimaliza kisiasa na itakuwa ni bora kama ungekaa kimya tu.
 
By Zitto,

Juzi nilipokuwa jijini Mbeya niliulizwa na wananchi iwapo nami nitachukua kiinua mgongo cha tshs 238 milioni kitakacholipwa kwa wabunge. Nimewajibu kuwa msimamo wangu upo wazi kwenye masuala haya.

Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua. Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka kusaidia ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi Shule ya Buhangija na Hospitali ya Saratani ya Ocean Road. Buhangija nilitembelea mwezi Aprili na kukuta watoto wanalala kwa shida sana.

Niliamua kusaidia juhudi zinazofanywa na Miss. Tanzania Briggite Alfred ambaye anajenga Bweni pale. Ocean Road ni mchango wangu katika kusaidia wagonjwa wa saratani, ugonjwa uliomchukua mama yangu Hajjat Shida Salum.

Source: His facebook page.

Huyu Zitto kweli ni akili kubwa. Muda si mrefu wanafiki na wapenda sifa nao wataanza kumuiga, japo moyoni hawapendi kuachia hiyo mihela.


Nimesoma hii habari mara mbili. Sijaona aliposema hatapokea kiinua mgongo cha Tshs. 238 milion. Alichokisema ni kwamba anafikiri hastahili kula (kufanyia mambo yake binafsi) hiyo hela. Hivyo, ataipokea hiyo pesa na kuitoa kama mchango wake (hili ni jambo lake binafsi kwa kuwa ata claim mchango huo katoa yeye) kwa Shule ya Walemavu wa Ngozi na Hospitali ya Saratani Ocean Road.
 
Zito! Zito! Muogope Mungu! Zile ulizoenda kuchukua CRDB zilikuwa halali yako? Zile za kigeni zilizopelekwa ujermani ktk a/c ya yule dada je zilikuwa halali yako? acha hizo ndugu ni aibu kwako kudanganya umma!
 
By Zitto,

Juzi nilipokuwa jijini Mbeya niliulizwa na wananchi iwapo nami nitachukua kiinua mgongo cha tshs 238 milioni kitakacholipwa kwa wabunge. Nimewajibu kuwa msimamo wangu upo wazi kwenye masuala haya.

Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua. Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka kusaidia ujenzi wa Bweni la wanafunzi wenye ulemavu wa ngozi Shule ya Buhangija na Hospitali ya Saratani ya Ocean Road. Buhangija nilitembelea mwezi Aprili na kukuta watoto wanalala kwa shida sana.

Niliamua kusaidia juhudi zinazofanywa na Miss. Tanzania Briggite Alfred ambaye anajenga Bweni pale. Ocean Road ni mchango wangu katika kusaidia wagonjwa wa saratani, ugonjwa uliomchukua mama yangu Hajjat Shida Salum.

Source: His facebook page.

Huyu Zitto kweli ni akili kubwa. Muda si mrefu wanafiki na wapenda sifa nao wataanza kumuiga, japo moyoni hawapendi kuachia hiyo mihela.


Zitto,

Kama kawaida yake hapa amejaribu kutumia lugha ya kilagai kama ilivyokawaida yake katika kukwepa ukweli,Mkuu Haki sawa Upo sahihi.
 
Last edited by a moderator:
Zito! Zito! Muogope Mungu! Zile ulizoenda kuchukua CRDB zilikuwa halali yako? Zile za kigeni zilizopelekwa ujermani ktk a/c ya yule dada je zilikuwa halali yako? acha hizo ndugu ni aibu kwako kudanganya umma!

Zitto Anadhani Watanzania wote wana fkra Butu kama wale wafuasi wake.
 
Last edited by a moderator:
..Chochote ambacho sio haki yangu sitachukua.
Hii sawa

..Fedha yote ya ziada ya kile ninachostahili kwa mujibu wa sheria nitapeleka ...
Sasa hapa fafanua vizuri, utapeleka bila kuchukua? Au utachukua na kisha uamue cha kufanyia (sehemu ya kupeleka)? Kama ni hivyo ina tofauti gani na wanasiasa wengine ambao pia watachukua? Tukiwauliza watasema wamesaidia majimboni mwao.

Kama upo serious, acha tu usichukue kabisa....tutakuelewa.
 
Zito ana akili gani? ni zinga la msanii acha wewe! kwa akili zako za kuazima toka kwa mkeo ndio maana unaona zitoan akili! Polle sana na nakushauri uwe unatumia akili zako japo ndogo.

Ukiwa mfuasi wa ma criminal na wewe unakuwa na majibu ya ma criminal, sasa matusi ya kazi gani humu!?
 
Hii sawa

Sasa hapa fafanua vizuri, utapeleka bila kuchua? Au utachukua na kisha uamua cha kufanyia (sehemu ya kupeleka)? Kama ni hivyo inatofauti gani na wanasiasa wengine ambao pia watachukua? Tukiwauliza watasema wamesaidia majimboni mwao.

Kama upo serious, acha tu usichukue kabisa....tutakuelewa.
Ndugu Huyu Zitto hana Ubavu huo,Hapa anachotafuta ni Misifa ya kipuuzi.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: SMU
Aseme anazostahili kwa mujibu wa sheria ni ngapi? Mbona yeye analipwa wakati alifukuzwa kwenye chama chake na kuukosa Ubunge ? Mbona mpaka leo akina Danny Makanga na Erasto Tumbo , tangu walipofukuzwa UDP hawajawahi kulipwa mafao yao ? yeye analipwakwa utaratibu upi?
taratibu mkuu zitto hakufukuzwa, zitto alijiuzuru hivyo malipo ni halali yake. kama nahisi alifukuzwa leta ushahidi
 
Kumbuka hakustahili kupata hata senti moja huyo bwana baada ya kujitoa chadema na kuaga bungeni . hana haki ya senti tano acheni kuchezeshwa nahuyu bwana muongo . Ni rahisi kuwadanganya wabunge si wananchi huku uraiani.Mpendazoe alipewa sh ngapi? mbona yeye kwakuwa pro-CCM wamemuahidi kumpa wakati hayupo bungeni? Ndio maana CCM wanatuchezea watanzania hatuko critical ni kushangilia na kucheza ngoma basi. Zitto anakuambia tusiamini wanasiasa anajijua. Kama kuna vijana hawawajui wanasiasa jifunzen kwa mrema
 
ataje zilizo sahihi ni zipi na zisizo sahihi ni zipi coz hiz hela hapewi mkononi bali zitaingia kwa benki na hatutojua wal kuziona.
 
Uchaguzi Ukipita Act Itakuwa Na Mbunge 1 Na Zitto Attakuwa Kwenye Kaputaka (dastbin) Tayar Kwenda Chomwa Dampo
 
Zito! Zito! Muogope Mungu! Zile ulizoenda kuchukua CRDB zilikuwa halali yako? Zile za kigeni zilizopelekwa ujermani ktk a/c ya yule dada je zilikuwa halali yako? acha hizo ndugu ni aibu kwako kudanganya umma!
hapa ndo huwa nachoka kabisa, nani aliwahi jitokeza kusema hili kwa uwazi kama msemaji wa chama bwana mnyika alisema huo waraka hautambui na haujatolewa na kamati kuu wewe unauamini vipi. hapa wewe ndo ulidanganywa na unatia aibu kuja na maneno ya kutunga.
 
Zitto kwa hili nitakupongeza bila kujali mapungufu yako au makosa yako na wala sitasubiri mpaka siku utangulie mbele ya haki ndio niseme.

Hata hivyo,huna budi kututhibitishia ni kiasi gani umechukua na kiasi gani umepeleka kusaidi hizo huduma za jamii.Ukishindwa kuthibitisha hili ujue utaendelea kujimaliza kisiasa na itakuwa ni bora kama ungekaa kimya tu.

aliagize bunge lipeleke huko kwa wenye mahitaji maalumu.
 
Kumbuka hakustahili kupata hata senti moja huyo bwana baada ya kujitoa chadema na kuaga bungeni . hana haki ya senti tano acheni kuchezeshwa nahuyu bwana muongo . Ni rahisi kuwadanganya wabunge si wananchi huku uraiani.Mpendazoe alipewa sh ngapi? mbona yeye kwakuwa pro-CCM wamemuahidi kumpa wakati hayupo bungeni? Ndio maana CCM wanatuchezea watanzania hatuko critical ni kushangilia na kucheza ngoma basi. Zitto anakuambia tusiamini wanasiasa anajijua. Kama kuna vijana hawawajui wanasiasa jifunzen kwa mrema
sema hauko critical wewe sio wote, kwa nini hastahili kupewa hata senti tano ili hali amejiuzuru
 
Back
Top Bottom