Zitto aiteta CHADEMA

Zitto aiteta CHADEMA

Robethn

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2015
Posts
2,103
Reaction score
354
CHAMA cha ACT-Wazalendo kimezidi kutamba kwamba ndicho chama pekee cha upinzani kinachoweza kuzungumzia ufisadi ambao ni tatizo kubwa la maendeleo nchini mbele ya wananchi.

Akihutubia katika mikutano ya hadhara kwa nyakati tofauti mkoani , Kiongozi Mkuu wa chama hicho, Zitto Kabwe alisema vyama takribani vyote vya siasa sasa vimechafuka kwa sababu vimekumbatia mafisadi na hivyo hawawezi tena kukemea ufisadi.

Zitto alisema mgombea urais kwa tiketi ya Chadema ambaye anawakilisha vyama vinavyounda umoja wa Ukawa, Edward Lowassa, kabla hajahama Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), chama hicho pamoja na vyama shiriki waliueleza umma wa watanzania kuwa ni fisadi lakini sasa wamempokea na kumpendekeza kugombea nafasi ya urais, jambo ambalo limeua hoja ya ufisadi na chadema kuendelea kukumbatia mafisadi.
 
Issue si Kuzungumza Kwani Hata CCM Wenyewe Wanauzungumza Ufisadi Tena kwa Kutetemeka.Issue ni kukosekana Kwa Nia ya Dhati na Mfumo Mbovu wa CCM Wa Kulindana Kifisadi.

Wananatuita Malofa Kwa Sababu wanaona Tunakwenda Kubomoa Mfumo wao Wa Kujilimbikizia.
 
Alisema serikali inapaswa kukiri kwamba, kuna Watanzania wengi waliomaliza darasa la saba, kidato cha nne na cha sita, walioko mitaani hawana ajira. Tusipoangalia watakuja kula sahani moja na sisi. Tusipowashughulikia," alitahadharisha Lowassa.

Kadhalika, alisema mipango mingi ya maendeleo nchini imekuwa haifanikiwi kutokana na serikali kutokuwa na msimamo wa kufanya maamuzi magumu

"Tatizo la nchi hii mnazungumza mambo hakuna utekelezaji. Tunazungumza, lakini discipline (nidhamu) ya (nchi ya) Malaysia na hapa (Tanzania) ni tofauti. Hapa kuna uswahili mwingi wa kukaa bila kutekeleza mambo, mnaamua hamtekelezi," alisema Lowassa


Alishauri kuwapo na chombo, ambacho kinaweza kufanya maamuzi magumu na yakawa magumu yanayotekelezeka kweli kweli.
Alisema tabia ya kujivika joho la kufanya maamuzi ya utekelezaji, lakini bila kufanya, ni kazi bure

"Tukikubaliana mambo yafanyike. Haiwezekani katika nchi kila mtu akawa analalamika. Kiongozi analalamika, mwananchi analalamika, haiwezi ikawa ni jamii ya kulalamika lalamika. Awepo mtu mmoja anayefanya maamuzi na anayechukua hatua," alisema Lowassa
 
Safi sana Zitto, umeonyesha ukomavu wa kisiasa
 
Watakuja hapa na matusi chungu nzima
Lakin all in all zito kasema la maana hapa

Wasituletee mambo ya kwenye stand ya chato (uharo)

Viva zzk
 
Aache uhuni uyo..; Kwani hajasikia measure ya kuwa na mahakama special itakayohusika na Ufisadi??
# shkamoo Magufuli my president!!
HAPA KAZI TU!
 
Magufuli ndo kura yangu zitto angekua lowassa CCM ningemchagua mgombea wa ACT
 
Iwapo act_wasaliti kikiingia ikulu basi bwana zitto atakuwa ndo firstlady.
 
Twaweza imeonyesha ACT ya Zitto itapata 0% ya kura zote ikifika Octoba 25.
 
Yeye mwenyewe fisadi...kwani ukibaraka huku ukilipwa sio ufisadi. Kwanini aliwasaliti Chadema. Aende zake huko asitufanye mabwege
 
Zitto yupo sahihi, chadema hawana hoja ya ufisadi
 
Huu ni ukweli japo ni mchungu.
Magufuli na Lowasa hakuna tofauti, ni ccm ileile.
 
Back
Top Bottom