Kashaijabutege
JF-Expert Member
- Oct 20, 2010
- 2,696
- 740
Kusema ukweli sasa, inakuwa ni vigumu kumpata mchumba umpendaye wa kabila lako; hasa baada ya watu wengi kuhamia mijini na kwenda walikozaliwa kwa matembezi tu (au kugombea ubunge); ni baada ya utandawazi.
Watoto tunaowazaa wanakuwa ni wa 'mjini' na kwa nadra wanaweza kuongea lugha za makabila yetu. Nachelea kusema, huenda baada ya miongo fulani, lugha zetu za asili zitakuwa zimetoweka katika uso wa dunia. Haidhuru basi, watoto wangeweza kuokoteza neno moja moja kutoka kwa lugha za wazazi wao, lakini na hilo haliwezekani kwa sababu wazazi wenyewe hawasikilizani kwa vile ni makabila tofauti.
Mbali na lugha, watoto wanashindwa kupata mila ya kufuata. Wanabaki kati kati, kwa baba hawapo na wala hawapo kwa mama.
Hakika, Mungu alikuwa na makusudi kumuumba kila mtu katika kabila lake au taifa lake (Mtikila, 1995). Pamoja na mazuri ya utandawazi wa kuoa au kuolewa katika makabila tofauti, binafsi, naona hasara ni nyingi kuliko faida.
WanaJF mnasemaje?
Watoto tunaowazaa wanakuwa ni wa 'mjini' na kwa nadra wanaweza kuongea lugha za makabila yetu. Nachelea kusema, huenda baada ya miongo fulani, lugha zetu za asili zitakuwa zimetoweka katika uso wa dunia. Haidhuru basi, watoto wangeweza kuokoteza neno moja moja kutoka kwa lugha za wazazi wao, lakini na hilo haliwezekani kwa sababu wazazi wenyewe hawasikilizani kwa vile ni makabila tofauti.
Mbali na lugha, watoto wanashindwa kupata mila ya kufuata. Wanabaki kati kati, kwa baba hawapo na wala hawapo kwa mama.
Hakika, Mungu alikuwa na makusudi kumuumba kila mtu katika kabila lake au taifa lake (Mtikila, 1995). Pamoja na mazuri ya utandawazi wa kuoa au kuolewa katika makabila tofauti, binafsi, naona hasara ni nyingi kuliko faida.
WanaJF mnasemaje?