ZILIPENDWA: Wanamuziki, nyimbo na mitindo yao

Bila kuwasahau Bima Lee Orchestra....Bendi hii ilikuwa ikimilikiwa na Shirika la Bima la Taifa.....Iliimarika zaidi mwaka 1984 baada ya kuwapata wanamuziki kutoka bendi tofauti tofauti walipoletwa kwenye bendi hii kwa lengo la kuiimarisha....Wanamuziki hao ni Shaban Dede,Jerry Nashon 'Dudumizi',Joseph Mulenga,Abdalaah Gama na Athuman Momba....Bendi hii ilikuwa ikitumia mtindo wa Magnet 84 na baadae uliboreshwa ukawa Magnet ndele Tingisha.....

Bendi hii ilitamba na nyimbo kama Neema,Shangwe ya harusi,Makulata,Linalonisibu,Milionea wa mapenzi,Linalonisibu,Siri yako,Visa vya mesenja,Uzuri ni tabia,Dunia ni upepo,Busu pande tatu,Ndoa fungo la hiyari,Penzi dawa ya chuki,Samaki baharini,Baba Shani,Shakaza na nyingine nyingi....

Bendi hii iliundwa na wanamuziki kama Shaban Dede,Athuman Momba,Joseph Mulenga,Abel Barthazar,Abdallah Gama,Belesa Kakere,Maxmilillian Bushoke,Jerry Nashon,Coumson Mkomwa,Eddy Sheggy,Fresh Jumbe na wengine wengine

Hapa mkuu umenikumbusha mbali hii bendi niliipenda sana,na nimejaribu kutafuta nyimbo zake bila mafanikio. Kama kuna link naweza pata nyimbo zake plz iweke hapa.

shangwe ya harusii imekuwa kitendawili kilichokosa mfumbuuzi jamaaniee,

furaha yoyooo imegeuka maachozi niiliyemtegemea kanisalitii! kaniumbuaae.


www.Muziki.net hapa zipo nyingi lakini za bima lee sijaziona
 
bendi hizi hazina mfano.inasikitisha mno.maana nyimbo zilijaa mafunzo bila kusahau burudani.ukichanganya na wale watangazaji walizoziendesha,ilikuwa raha tele.kwa hivi sasa hamna kitu.fujo moja kwa moja
 
hapamtani umenikumbusha mbali wacha na mie niendelee ''' sijaona manowari eeh ikipita barabarani, fimbo ooh fimbo mkononi.....


dah haka kawimbo kalikuwaga katamu sana mi huwa najiuliza ukienda RTD oops sorry TBC Taifa, huwezi pata hizi nyimbo?

Ngoja na mimi niendeleze...
wanawake wa kitanga, ukicheza uta-tangatanga
hata maji ya kuoga, huchanganywa na hiliiiiki
Na mdalasini, ua waridi......

Jamani huu wimbo nimeutafuta mpaka basi, atakayeupata tafadhali atuwekee hapa.
 
Kuna huu wimbo wa Fanta pia niliupenda sana, hivi uliimbwa na nani?

Fanta wangu
Uliamua
Kuniacha peke yangu mama kwa ajili ya pesa aah
Mwenye pesa, kanipora nawe eeh
 
Kuna huu wimbo wa Fanta pia niliupenda sana, hivi uliimbwa na nani?

Fanta wangu
Uliamua
Kuniacha peke yangu mama kwa ajili ya pesa aah
Mwenye pesa, kanipora nawe eeh

Fanta Wangu uliimbwa na Hayati Kalala Mbwembwe .....Haukupigwa na bendi yoyote bali uliimbwa kwa mtindo wa Zingzong ambapo Mbwembwe aliwakusanya wanamuziki kutoka bendi tofauti na kurekodi kibao hiki cha FantaWangu ambacho kwa hakika kilitamba sana enzi hizo.....Wimbo huu Kalala Mbwembwe alikuwa akiuaimba katika bendi zote alizokuwa akiziimbia kabla hajaaga dunia... Bendi hizo ni pamoja na TanCut Almas ya Iringa, Ruaha International ya Iringa na baadae Vico Stars pia ya Iringa......

Wimbo huu ulikuja kurudiwa na kijana Papii Nguza ambaye alijitahidi kuutendea haki.......Aliutoa wimbo pamoja na nyimbo za Seya, Moyo na Salima....
 
Balantanda, thank for this great thread, angalau nimepata nafasi ya kukumbuka nyimbo zetu za ujanani. Hivi kuna mtu anaweza kuwa na lyrics ya wimbo: Mazoea yananikondesha? Nimeona mtu mmoja humu amejaribu kuuandika lakini ameishia njiani. I would real like to get it. Thanks wakuu!
 
Last edited by a moderator:
Abel, Mulenga, Omary na Gama, George, Kessy, Mwanyilo, Habib, Machaku

Bichuka, Gulumo, Cosmas, Hamis, bwana Ibrahim, Bony, Juma Town

King Enock, thomas, Samwel, Joseph Bernald, Juma na Kitwana
 
Wimbo wa sikinde uitwao "mfaume waniliza" ni kiboko, ulirekodiwa redio tanzania dar es salaam mwanzoni mwa miaka ya 1980.sauti za bichuka,gurumo na wengineo zilitia fora
 
Wimbo wa sikinde uitwao "mfaume waniliza" ni kiboko, ulirekodiwa redio tanzania dar es salaam mwanzoni mwa miaka ya 1980.sauti za bichuka,gurumo na wengineo zilitia fora


Ebana huo wimbo umepigwa rythim na solo ile mbaaaya.
Kisha mwisho Saxa likacharazwa sana.
 
Indeinde indemoni..inde inde kisakula inde.Kanda bongoman na ile kofia loh mnanifanya nilie.Na Yondo sister(MBUTAMUTU)
 
kampuni ya kinywaji cha konyagi imewazawadia seti kamili ya vyombo vya muziki Bendi za Msondo na Sikinde na tayari vyombo hivyo vimeanza kutumika katika maonesho mbalimbali.
 
Nani anaukumbuka Maprosoo?


MAPROSOO ni wimbo mzuri sana ulio katika mahadhi ya Rhumba......

Ulitamba sana mwishoni mwa miaka ya 90 kuelekea mwaka 2000.....Wimbo uliimbwa na kundi dogo la Jambo Survivors Band........Kundi hili liliundwa na baadhi ya wanamuziki waliojiengua kutoka bendi ya KILIMANJARO CONNECTION ya KANKU KELLY....

Kundi hili liliundwa na wanamuziki wanne ambao ni Hassan Shaw, Ramadhani Kinguti maarufu kama Kinguti System, Burhan Muba na mwanadada pekee Mlasi Feruzi (Dada yake Ferooz Mrisho).........Mlasi ndiye aliimba wimbo huu wa Maprosoo....

Kundi hili la Jambo Survivors lilikuwa likifanya muziki wake kwa mtindo wa Sequencer Keyboards.......Kundi hili bado lipo na linafanya muziki wake zaidi katika nchi za Asia kama Thaiiand, Malaysia, Singapore n.k.......


patong-jambo-survivors.jpg
 
Last edited by a moderator:
MAPROSOO ni wimbo mzuri sana ulio katika mahadhi ya Rhumba......

Ulitamba sana mwishoni mwa miaka ya 90 kuelekea mwaka 2000.....Wimbo uliimbwa na kundi dogo la Jambo Survivors Band........Kundi hili liliundwa na baadhi ya wanamuziki waliojiengua kutoka bendi ya KILIMANJARO CONNECTION ya KANKU KELLY....

Kundi hili liliundwa na wanamuziki wanne ambao ni Hassan Shaw, Ramadhani Kinguti maarufu kama Kinguti System, Burhan Muba na mwanadada pekee Mlasi Feruzi (Dada yake Ferooz Mrisho).........Mlasi ndiye aliimba wimbo huu wa Maprosoo....

Kundi hili la Jambo Survivors lilikuwa likifanya muziki wake kwa mtindo wa Sequencer Keyboards.......Kundi hili bado lipo na linafanya muziki wake zaidi katika nchi za Asia kama Thaiiand, Malaysia, Singapore n.k.......


patong-jambo-survivors.jpg

walikuwa noma kweli....mimi huu mwimbo high school rafiki yangu fulani roby ndo akawa anauimba ndo nikaumbuka..hadi leo sijahusahau..una sauti fulani hivi ambayo inakufanya uupende kichizi..kuna huu na Tupendane wa kilimanjaro band.
 
Wakuu naomba msaada, kwenye nyimbo Makulata na Subiri kidogo (Mwamvua) mwanamuziki Jerry Nashon kuna lugha ameitumia na si ya kiswahili anayeifahamu naomba anijuze.
 
leo nimeisikiliza nyimbo ya Urafiki Jazz wana Chaka chuwa inasema...

''biashara ya njugu na korosho haikufai mama wee, Gezaulole mama, Gezaulole Mama wee''

Dah Juma Mrisho Ngulimba wa Ngulimba amefanya kazi sana mle...
 
Wakuu naomba msaada, kwenye nyimbo Makulata na Subiri kidogo (Mwamvua) mwanamuziki Jerry Nashon kuna lugha ameitumia na si ya kiswahili anayeifahamu naomba anijuze.

Jerry Nashon ameimba Immaculata (Makulata) kwa lugha ya Kijaluo.
 
Back
Top Bottom