Gang Chomba
JF-Expert Member
- Feb 29, 2008
- 20,301
- 4,681
Mimi bana sikinde tuuu, jamani sikinde watani wangu msondo mtaniwia radhi. Dah kuna vibao nikivisikia mpaka natokwa na jasho kuna kitu km Duniani Kuna mambo, wikiendi nalala kwa taabu, kwa ujumla sikinde you rock my heart!! ningekuwa na pesa ninge invest trillions pale basi tu sina kitu. haya kuna hawa marques du zaire enzi za kamanyola bila jasho kuna kibao kama dola mtoto wa Dodoma( yakaa yaka eeehn mwana mama ndimandimaeee mwana mama ...... mtoto wa dodoma) kuna kinanda flani kinapigwa mle na gitaa yaani ni raha tupu!! inanikumbusha sana dada yangu marehemu Mage jamani wakati niko Sumbawanga alikuja toka Dar basi anaziimba hizi nyimbo za makwizzz aaah jamani KAMANYOLA BILA JASHO! ikaja telemuka telemuka chekechaaaaaa
Namba moja
Namba moja
Kwa waliokuwepo Mwanza 1969 tukumbuke Orchestra Super Vea. Hapo alikuwepo pia mpiga rhythm mahiri Zahir Ally (Baba yake Banana) wakati huo tunamwita Zahoro "Zorro" na alikuwa kijana mtanashati sana. Tulikuwa tukipita Social Hall, karibu na Nyakabungo njiani kuelekea Isamilo toka Chopra Sec ilikuwa ni lazima tutulie kidogo pale na kuwasikiliza Super Vea mazoezini, walitamba sana na kibao chao cha Apollo kumi na moja. Vijana waliotamba enzi hizo Mwanza walikuwemo pia Martin (mchezaji wa Pamba Sports na mfanyabiashara wa madini). Zahoro alikuwa na uwezo wa kupiga gitaa wakati amelibeba nyuma ya kichwa, staili maarufu sana wakati huo. Baadaye nilikuja kukutana na Zahoro 1974 Dar es Salaam akiwa anafanyiwa audition na Bima Lee (bendi ya Bima wakati huo) kwenye jengo jipya la Kitega Uchumi pale chini (underground floor) kulikuwa na sehemu ya mazoezi kabla haijageuzwa kuwa Chinese Restaurant. Zahir hakufanikiwa kujiunga na Bima Lee lakini baadaye aliibukia JKT Kimbunga.
Tatizo wewe Gang una mahaba ya sikinde asilimia 100.Nginde
Dunia nzima
Kama baba yako unaweza kumtusi utakuwa wewe si rizkiHuyu atakua choko
kuna ubishi wa kumbukumbu...
je kwenye wimbo Asha Bora wa sikinde solo limepigwa na nani?
1) Kasim mponda delashamshi
2) Mkanyia
Wimbo uliimbwa na Juma Ubao akiwa na Six Manyara BandWaungwana kuna mtu anaukumbuka wimbo uliopigwa na Six Manyara unaitwa Tabu, ambapo mmoja ya waimbaji wake
alikuwa Hassan Rehani Bichuka.
Asante sana mkuu BalantandaWimbo uliimbwa na Juma Ubao akiwa na Six Manyara Band
Enjoy mkuu....
Wimbo uliimbwa na Juma Ubao akiwa na Six Manyara Band
Enjoy mkuu....
Sina uhakika sana..Ila bendi zetu hizi zilikuwa na wapiga solo wawili...First solo na second solo...
Ila mpini wenyewe wa solo aliukamata Kassim Mponda 'De la Chance' (sio Delashamshi)...
Na inawezekana second solo alipiga Henry Mkanyia...
All in all Kassim Mponda ni mmojawapo wa wapiga solo bora kabisa kuwahi kutokea Tanzania...
Ukitaka uone ubora wake pia sikiliza wimbo wa 'Kiu ya Jibu' wa Nginde...
Tatizo wewe Gang una mahaba ya sikinde asilimia 100.
Nipe kisa cha Nico Zengekaya...
OSS= Ochestra safari soundMwaka 1985 muanzilishi wa bendi Abel Barthazal, Bitchuka na Ibrahim Mwinyichande nao pia walitimkia OSS
Dah! We jamaa umenikumbusha mbali sana.Nizamu ya kazi ni ushindi na mafanikio mema kazi,viongozi na wafanyakazi daima wote tuwe na nidhamu...migogoro na migongano ya kazini ni ukosefu wa nidhamu!! Aisee hapo ikiwa inapigwa hyo ngoma,mama anaunga kisamvu na ugari unanukia,hapo mshua amekalia kiti kama cha baba madenge anasoma gazeti la mzarendo...aisee mwenye nao atusaidiewadau kama kuna mtu anaufaham huu wimbo au anao.
Nidhamu ya kazi ni msingi wa mafanikio bora kazini, viongozi na wafanyakazi lazima wote muwe na nidhamu, migogoro na migongano makazini ni ukosefu wa nidhamu
Ha ha ha ha ha ha ha haaa! Kinaitwa kiti cha uvivu!Dah! We jamaa umenikumbusha mbali sana.Nizamu ya kazi ni ushindi na mafanikio mema kazi,viongozi na wafanyakazi daima wote tuwe na nidhamu...migogoro na migongano ya kazini ni ukosefu wa nidhamu!! Aisee hapo ikiwa inapigwa hyo ngoma,mama anaunga kisamvu na ugari unanukia,hapo mshua amekalia kiti kama cha baba madenge anasoma gazeti la mzarendo...aisee mwenye nao atusaidie