Haaa Bala umeturudisha kwenye mambo yetu yaleeeee,
Vijana walikuwa machachari na ndio walikuwa bendi neutral ya wapinzani wa Jadi DDC na Msondo
Umenikumbusha Dudumizi mtaalamu wa nyimbo za mapenzi
Jamaa(Jerry Nashon Dudumizi) alikuwa mtunzi kwelikweli wa nyimbo za mapenzi hasa akiwa na Bima Lee na Vijana Jazz...
Angalia kama kitu hiki kitamu hapa chini ambacho ni utunzi wake..
V.I.P-Jerry Nashon 'Dudumizi"
(Wote): Ahera hakuendeki,Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikooo,
Ahera hakuendeki Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikoooo,
(Dudumizi): Si maji wala Soda vitakavyozima kiu yangu,ila ni wewe VIP,
Si maji wala Soda vitakavyozima kiu yanguuu,iila ni weweeeee,VIP
Baada ya kazi ngumu ya kutafuta pesa,na kisirani cha kufokewa na boss,
Nahitaji VIP wa kunibembeleza,nakutaka wewe mama,unibembeleze,
Si kwa maneno ila kunitomasatomasa,kwa mikono yako laini yenye bangili,
Unipe busu mwanana la kunipumbaza wee (VIP).
Baada ya kazi ngumu ya kutafuta pesa,na kisirani cha kufokewa na boss,
Nahitaji VIP wa kunibembeleza,nakutaka wewe mama,unibembeleze,
Si kwa maneno ila kunitomasatomasa,kwa mikono yako laini yenye bangili,
Unipe busu mwanana la kunipumbaza wee (VIP)
(Wote): Ahera hakuendeki,Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikooo,
Ahera hakuendeki Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikoooo,
Ahera hakuendeki,Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikooo,
Ahera hakuendeki Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikoooo.
Dudumizi: VIP sogea karibu,ubipe busu mwanana mama
(Wote): Ahera hakuendeki,Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikooo,
Ahera hakuendeki Dunia haikaliki nimepatwa na mfadhaikoooo,
Bridge
(Wote): Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka.
Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka
Nina nia ya kuwasha moto wa mapenzi kwako,kwa uzuri ulionao VIP,
Nina nia ya kuwasha moto wa mapenzi kwako,kwa uzuri ulionao VIP
Natamani penzi live sio penzi la ndotoni,nakuomba uwe wangu VIP,
Tafadhali nakusihi, ili niondokane na ndoto za mapenzi.
(Wote): Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka.
Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka
Nina nia ya kuwasha moto wa mapenzi kwako,kwa uzuri ulionao VIP,
Nina nia ya kuwasha moto wa mapenzi kwako,kwa uzuri ulionao VIP
Natamani penzi live sio penzi la ndotoni,nakuomba uwe wangu VIP,
Tafadhali nakusihi, maaa mamaa,maaa....maaa yoooo,maa mamamaaaaaaaaaaaaaaa,
Tafadhali nakusihi, ili niondokane na ndoto za mapenzi.
Dudumizi: Ukinikubali VIP,mimi niko tayari,kubadili dini,
Ukinikubaliii VIP mimi niko tayari,kubadili dini,
Hata kama wazazi wangu hawapendi,nitafanyafanya mipango niwe na wewe sambamba(sambamba)
nitafanyafanya mipango niwe nawee sambambaaa
(Wote): Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka.
Ukinikubalii VIP,mimi niko tayari kubadili dini,
Ukinikubalii VIP,nitatoa mahaliii ya mbuzi saba,
Hata kama sina VIP,nitafanyafanya mipango niwe na wewe sambamba(sambamba) nitafanyafanya mipango niwe na wewe
sambamba.
(Wote): Binadamu hanunuliwi kama nguoo VIP,ungekuwa Dukani ningekununua nikuweke ndani,lakini nikikununua bila mapenzi yako
Utanitoroka.