Balantanda (PhD)!
By virtue of the authority vested in me by JF, I hereby confer upon you the Honorary Degree of Doctor of Music.
Congratulations!
Si wewe tu mkuu wangu,kila mtu akizikumbuka bendi kama Marquis(wana sendema,zembwela n.k),Sambulumaa,Vijana Jazz(pambamoto),Washirika Tanzania Stars(watunjatanjata,njata one),Tancut Almas(wana fimbo lugoda,kinyekinye kisonzo tisa kumi mangala),JKT Mafinga(kimulimuli),JKT Kimbunga stereo,Ngorongoro Heroes Band(sukuma push),Kurugenzi Jazz,Six Manyara,Bima Lee(Magnet tingisha),Super Matimila(Bongo beats,talakaka),Zaita Musica(wana zuke muselebende),MK Group(wana Ngulupa tupatupa dansi),MK Beats(wana tukunyema,wowowo),MK Sound,OSS(wana masantula ngoma mpwita,dukuduku,ndekule,power Iranda,rashikanda wasaa),MCA Internationa(wana munisandesal,Orch. Makassy,Magereza Jazz(Mkote Ngoma),Bicco Stars(wana kindumbwe ndumbwe),Super Rainbow,Bantu Group Band(wana kasimbagu kaabuka),Legho Stars(wana sopabango),Afriso International ya Lovy Longomba na nyingine nyingi lazima utatokwa chozi mkuu,kifo cha bendi hizi ndio kifo cha muziki wetu ule mtamu tulioupenda,haupo tena.......Nyingi kati ya bendi hizi zimekufa na zilizopo zinajikongoja........Natamani kuurudisha wakati nyuma aisee....
Kuhusu Super Stereo Hassan Rehani Bitchuka,kwa sasa yupo Mlimani Park orch wana Sikinde ambako alihamia akitokea Msondo Ngoma....
Dr. Balantanda amenikumbusha mbali. Miongoni mwa nyimbo nazopenda sana ni "Ni wewe pekee" wa Nguza Viking/Marquis na Jack wa Nico Zengekala. Nikisikiliza nyimbo hizi nahisi mapigo ya moyo yanabadilika.
Single ya Alikiba, "Usinisemee kama napenda kula" tutaisikiliza kweli?
Dr. Balantanda amenikumbusha mbali. Miongoni mwa nyimbo nazopenda sana ni "Ni wewe pekee" wa Nguza Viking/Marquis na Jack wa Nico Zengekala. Nikisikiliza nyimbo hizi nahisi mapigo ya moyo yanabadilika.
Single ya Alikiba, "Usinisemee kama napenda kula" tutaisikiliza kweli?
Aah, Jackie, mtoto wa Nairobi.
Mkuu zile zilikuwa nyimbo bwana.
Sio haya mabongo fleva, vijana wanajaza majina ya wauza chips kwenye wimbo mzima. Ha ha ha.
Kulikuwepo na Orchestra Tomatoma, walikuwa na kibao cha "Mwanaidi" nao walikuwa wametulia, sijui hata walifia wapi.
Nakumbuka kulikuwa na bendi ya Chezimba ilikuwa inapiga Twiga Hotel samora...wimbo wao maarufu "Kijongoo sina nyumba..."
Then kulikuwa na bendi nyingine ikiitwa Bene Bene, Jambo Stars....Of course Tanzanites na wimbo wao "KIdude"
Pia ilikuwepo bendi ya Tancut Almasi,bendi hii ilikuwa inamilikiwa na kiwanda cha kukata almasi kilichokuwa mkoani Iringa na ilikuwa ni mojawapo ya bendi za mikoani zilizokuwa na makali kweli(kama jirani zao wa JKT Mafinga wana Kimulimuli chini ya Zahir Ally Zorro na Kurugenzi ya Arusha).....Tancut Almasi walikuwa wakitumia mtindo wa Fimbo Lugoda na Kinye kinye Kisonzo,tisa kumi Mangala.......
Bendi hii ilitamba na nyimbo kama Samahani ya uongo,Pili wangu,Butinini,Ngoma za Afrika,Helena mtoto wa Arusha,Masikitiko,Lutandila,Safari siyo kifo na nyingine nyingi tu tamu...
Bendi hii iliundwa na wanamuziki kama Kalala Mbwembwe,Nanah Njige,Nuru Mhina,Kawalee Mutimwana,Kyanga Songa,Kasaloo Kyanga,Mafumu Bilali 'Bombenga',Shaban Yohana 'Wanted',John Kitime,Akuliake Saleh 'King Maluu',Ray Mlangwa,Mohammed Shaweji,Kibambe Ramadhan,Bakari Buhero,Bdul Mngatwa,Hashim Kassanga na wengine wengi......Bendi hii ilikuwa na hazina ya vipaji kwa kweli.......
Bendi hii ilitamba sana kabla ya kuanza kusambaratika baada ya wanamuziki wake tegemeo akiwemo Kalala Mbwembwe,Kyanga Songa na Kasaloo Kyanga kuanzisha bendi nyingine hapohapo Iringa ya Ruaha International ambayo ilitamba sana na wimbo wa Lutandila namba 2 Safari (Safari safari safari kweli tabu,naomba kwa Mungu baba nifike salama,safari yangu mieee,safari ya Zimbabweee............ulikuwa wimbo mtamu kweli jamani).....
Kulikuwepo na Orchestra Tomatoma, walikuwa na kibao cha "Mwanaidi" nao walikuwa wametulia, sijui hata walifia wapi.
Mkuu Mzee Marijani (RIP) alikuwa nio kichwa haswa! Moja ya nyimbo nilizotokea kuzipenda ni Mayasa.Vipi kuhusu Dar International Orchestra wana Super Bomboka chini yake Jalbali la Muziki Marijan Rajab..... Kuna anayewajua hawa?,na atujuze basi.......
Mkuu Mzee Marijani (RIP) alikuwa nio kichwa haswa! Moja ya nyimbo nilizotokea kuzipenda ni Mayasa.. Mayasa mbona wanichana mbavu bibie, Sura yako mbona sasa imekuwa hivyo, Nakuuliza mbona hata kunijibu hutaki, Umenikasirikia kama mimi ndio nilikutuma, Sura yako mbona inatisha mama eh, Sio mimi wazidi kunichana mbavu Mayasa oooh...