Zijue aina kuu 2 za misukule

Mimi mbona nashindwa kuamini mambo haya
Na akili za kiccm huwezi kuelewa kamwe
Misukule aina ya nne ni wapiga kura wa chama chakavu!
Ahaaa misukule ya ccm. Na watu wanafikiri ni utani. Nimewahi kusikiliza ushuhuda ya mchawi lakini alikuwa zaidi ya mchawi tuseme ni "freemason" kwa jinsi watu wanavyoelewa, anasema watu wengi hulogwa wakati wa kupiga kura na pale maelfu ya majini yanapoachiliwa ili kupumbaza watu na hujikuta wakipiga kura bila kuwa na akili zao wenyewe. Akasema amefanya kazi nyingi kwa viongozi wa siasa waliopo leo na alikuwa analipwa mamilioni. Leo ameokoka na enaendelea kufichua siri nyingi sana. Hivyo misukule ya ccma ni kweli ipo manake huwezi kuamini kwanini watu wanaendekeza chama chenye zaidi ya miaka 60 sasa katika hali kubwa ya umaskini.
 
Hivi siku mtu akichukuliwa msukule hakuna hata mtu mmoja anaekuja kwenye msiba hashtukii mchezo uliofanyia,au wachawi,waganga na wenye makarama huwa wanashirikiana ?
 
Haya sasa wenye fani zao wameamua kutufundisha..😂
Mkuu samahani lakini hivi unaujua hata ujasiliamali..??

Ni swali tu tusifikishane mbali..🙏🙏😅
Ujasiriamali gani tena wakati tayari ameshauelezea ujasiriamali wake? Kazi ya manabii, wachungaji feki, mitume feki na waganga wa kienyeji ndiyo hii i.e. kukujaza hofu na pale unapokuwa na hofu ''wanakupiga'' kama hawana akili nzuri. Simulizi za uchawi zimekuwa nyingi sana siku hizi kwani wajanja wanataka kuwajaza watu hofu na wakishajaa hofu wanapigwa!
 
Usalama upo kwa Yesu, walozi ni viumbe wa hovyo....wanatoa kafara hadi watoto wao wa kuwazaa..
 
Kwa hiyo mkuu, msukule wa nje anakuwa anaishi kama binadamu wengine ila maisha yake yanakuwa yamefungwa? yaani hafanikiwi kwa lolote...
 
Nduguyangu unalolisema nisahihi kabisa, mwaka jana mdogowangu kabisa alifariki sasa baada ya muda amekuwa akinitokea analia kabisa.
 
Hivi siku mtu akichukuliwa msukule hakuna hata mtu mmoja anaekuja kwenye msiba hashtukii mchezo uliofanyia,au wachawi,waganga na wenye makarama huwa wanashirikiana ?
Wataalam wenyewe wanajua hili changa la macho, ila kile ni chama chao hawawezi muumbua memba. Kuna wengine kukataa unafiki huwa hawaendi kuzika
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…