Zifahamu tofauti kati ya Chui na Duma

Zifahamu tofauti kati ya Chui na Duma

CHUI-LEOPARD


View attachment 435663

Ana umbo nene na lenye madoa ya mviringo ni mnyama anayewinda kimya kimya kwa kunyatia.

DUMA-CHEETER

Ni aina ya jamii ya paka, mwenye ngozi ya manjano inayoelekea kwenye rangi ya udongo iliyopambwa kwa madoa meusi. Ndiye mnyama anayekimbia kwa mwendo kasi zaidi kuliko wanyama wengine wote watembeao hukimbia kilometa 113 kwa saa.

View attachment 435664

TIGER-SIMBA MARARA

Huyu ni jamii ya Simba na sio chui kama wengi wazaniavyo, Anaitwa Simba marara kutokana na ile milia yake inavyoonekana na Ana nguvu na Speed kuliko Simba wa kawaida.
Ndo hawa wanapanda miti?
Ref:Manyara nationa park
 
1479406155057.jpg

Nimefanikiwa kupata hiyo picha
 
Ndg chui ni mfupi, na makazi yake asilimia kubwa ni juu ya miti hii niliona ngorongoro. Duma in English Cheater huyu ni mrefu ,na mwembamba kidogo na ndie myama anaekimbia speed kubwa kuliko wote. hukimbia KLM 100 kwa SAA moja. Tiger huyu ni mnene ana miraba karibu kama pundamilia ana hasira sana huyu hupigana na simba huweza hata kupata point katika mapambano hayo .
Hivi mkuu ndege ni mnyama ? Kama ndio duma hawezi kuwa mnyama anayekimbia kuliko wote labda kama unaongelea wanyama watembeao juu ya ardhi

Ila kiumbe kinachokimbia kuliko wote ni Peregrine Falcon anakimbia 200 Mph

Sijui kwa kiswahili ndio anaitwa kipanga
 
Sawa ndg Mimi labda sikupambanua vizuri kwamba Duma anakimbia kuliko wanyama hawa wawindao wakiwamo king lion chui, fisi ect.
 
Kwa ukubwa anaanza Tiger(wamebaki Asia tu), Lion, Leopard na wamwisho ambae ni mnyonge sana porini kiasi kwamba wakiwa wawili wanamkimbia fisi moja ni Cheetah.
 
Kwa ukubwa anaanza Tiger(wamebaki Asia tu), Lion, Leopard na wamwisho ambae ni mnyonge sana porini kiasi kwamba wakiwa wawili wanamkimbia fisi moja ni Cheetah.
Hawa Cheetah wako Tz?
Kuna wale unawakuta kwenye baadhi ya Nyumba za wasanii wakubwa wakubwa ndo nani wale
 
Hawa Cheetah wako Tz?
Kuna wale unawakuta kwenye baadhi ya Nyumba za wasanii wakubwa wakubwa ndo nani wale
Cheetah wapo wengi Tanzania na Afrika kwa ujumla. Nikweli wasanii na watu wenye fedha wanapenda kufuga Cheetah na Lion.
 
Wakati nipo darasa la sits nilikuwa napenda kuwinda, kutumia mbwa, mkuki, na mishale, na Mara nyingine tulikuwa kukitumia miguu pekee, silaha yetu ilikuwa mbio tuu, kipindi cha mvua wanyama wengi kwato zao huoza, sass tulikuwa tukitumia udhaifu huo wakakimbiza hadi kuwakamata, maana wakifika ktk ardhi yenye changarawe wanaumia na speed hupungua, sasa kuna siku tulimuona huyo kiumbe Duma, jirani kwa wale wanaopajua Wami mbigiri /ukimbizini...si tukamuungia hatukumuona vizuri? Mmmh alikimbia kidogo alafu kulikuwa na mti flani akapanda hapo akageuka kutuangalia ndio tukamuona vizuri , tulikimbia, mom nilifika nyumbani miguu imechanika kwa kuchanwa na miiba, kucha mbili sina miguuni na nilikuwa nimevaa vile viatu vya kutengeneza kwa matair ya magari (nga'ati) kipo kimoja mguuni kingine hata kilipovukia sikufahamu , huyu mdudu anatisha kuliko Sura yake kwanza anamlio flani kama paka kimburu na yale macho yake eeh Mungu nashuru tulikuna na huyu angekuwa mkuu wa pori tusingefika nyumbani salama.
 
Ningeomba kujulishwa tofauti ziliyopo kati ya wanyama hawa wawili;

CHUI NA DUMA.

NA JE HUYO DUMA NDO TIGER AU CHEETAH?

Au kuna tofauti nyingine tena kati ya Tiger na Cheetah?

Kwa msaada zaidi pia ningeomba kujulishwa Classification zao kuanzia;
Kingdom
Phylum
Class
Order
Family
Genus and
Species

Ntashukuru kwa msaada wenu.

Karibuni
Tofauti za haraka haraka ni:1.Chui ni mnene kuliko duma kwa umbo
2.Chui ana kichwa kipana kilichounganika sambamba na shingo yake wakati duma ana kichwa kidogo kinachoendana na shingo yake nyembamba
3.Chui ana nguvu kuliko duma
4.Chui hupandisha mzoga wake mtini na kula hukohuko wkt duma hula windo lake ardhini
5.chui ana mbio lakini duma ana mbio kuliko chui pia ndio mnyama wa ardhini mwenye mbio kuliko wote
6.Madoa ya chui ni makubwa wkt madoa ya duma ni madogo madogo
7.Duma ana michirizi myeusi inayoelekea chini kwenye macho yake wkt chui hana hiyo michirizi
8.Chui ana mkia mpana wkt duma ana mkia mwembamba na mrefu kuliko wa chui
9.Chui mwili wake mpana kuanzia kifuani mpaka kiunoni wkt duma ni mpana kifuani lkn kiuno ni chembamba!
10. Chui huwinda mnyama kwa kumnyemelea mpaka umbali mfupi ndo humkimbiza lkn duma anaweza kukimbiza windo lake tokea umbali mrefu na akafanikiwa kukamata.
de87b5b23df5d04dcab57e460b261f13.jpg
a121633eda252438a3d5e353635e1651.jpg
c3bce9eb11f94392ab735d3bba5fcfa3.jpg
f2f3f91616fb3f6e3f52cf341b0b2d58.jpg

Picha mbili za mwanzo ni duma na mbili za mwisho ni chui
 
Wakati nipo darasa la sits nilikuwa napenda kuwinda, kutumia mbwa, mkuki, na mishale, na Mara nyingine tulikuwa kukitumia miguu pekee, silaha yetu ilikuwa mbio tuu, kipindi cha mvua wanyama wengi kwato zao huoza, sass tulikuwa tukitumia udhaifu huo wakakimbiza hadi kuwakamata, maana wakifika ktk ardhi yenye changarawe wanaumia na speed hupungua, sasa kuna siku tulimuona huyo kiumbe Duma, jirani kwa wale wanaopajua Wami mbigiri /ukimbizini...si tukamuungia hatukumuona vizuri? Mmmh alikimbia kidogo alafu kulikuwa na mti flani akapanda hapo akageuka kutuangalia ndio tukamuona vizuri , tulikimbia, mom nilifika nyumbani miguu imechanika kwa kuchanwa na miiba, kucha mbili sina miguuni na nilikuwa nimevaa vile viatu vya kutengeneza kwa matair ya magari (nga'ati) kipo kimoja mguuni kingine hata kilipovukia sikufahamu , huyu mdudu anatisha kuliko Sura yake kwanza anamlio flani kama paka kimburu na yale macho yake eeh Mungu nashuru tulikuna na huyu angekuwa mkuu wa pori tusingefika nyumbani salama.
Hahahahahaha mkuu kweli mlikuwa mmchoka kuishi yaani mnamuwinda mpaka Leopard.
 
Ningeomba kujulishwa tofauti ziliyopo kati ya wanyama hawa wawili;

CHUI NA DUMA.

NA JE HUYO DUMA NDO TIGER AU CHEETAH?

Au kuna tofauti nyingine tena kati ya Tiger na Cheetah?

Kwa msaada zaidi pia ningeomba kujulishwa Classification zao kuanzia;
Kingdom
Phylum
Class
Order
Family
Genus and
Species

Ntashukuru kwa msaada wenu.

Karibuni

Tofauti zao nadhani comments zimeeleza hapo juu.
Nimejaribu kukumbuka Biology ya Form One miaka hiyo ya mid 80's na Mwl Miss Lihepanyama,alikuwa anaimba Classification of living organisim

Cheetah

Kingdom ni Animalia
Phylum ni Chordata
Class ni Mammalian
Order ni Carnivora
Family ni Felidae
Genus ni Acinonyx
Species ni Jubatus

Tiger
Kingdom ni Animalia
Phylum ni Chordata
Subphylum ni Vertebrata
Class ni Mammalia
Order ni Carnivora
Family ni Falidae
Subfamily ni Acinonychinae,Falinae na Pantherinae
Genus ni Acinonyx hii iko chini ya subfamily Acinonychinae

Kuna genus 13 chini ya subfamily Falinae
Kuna genus 3 chini ya subfamily Pantherinae
 
Back
Top Bottom