Tofauti za haraka haraka ni:1.Chui ni mnene kuliko duma kwa umbo
2.Chui ana kichwa kipana kilichounganika sambamba na shingo yake wakati duma ana kichwa kidogo kinachoendana na shingo yake nyembamba
3.Chui ana nguvu kuliko duma
4.Chui hupandisha mzoga wake mtini na kula hukohuko wkt duma hula windo lake ardhini
5.chui ana mbio lakini duma ana mbio kuliko chui pia ndio mnyama wa ardhini mwenye mbio kuliko wote
6.Madoa ya chui ni makubwa wkt madoa ya duma ni madogo madogo
7.Duma ana michirizi myeusi inayoelekea chini kwenye macho yake wkt chui hana hiyo michirizi
8.Chui ana mkia mpana wkt duma ana mkia mwembamba na mrefu kuliko wa chui
9.Chui mwili wake mpana kuanzia kifuani mpaka kiunoni wkt duma ni mpana kifuani lkn kiuno ni chembamba!
10. Chui huwinda mnyama kwa kumnyemelea mpaka umbali mfupi ndo humkimbiza lkn duma anaweza kukimbiza windo lake tokea umbali mrefu na akafanikiwa kukamata.
Picha mbili za mwanzo ni duma na mbili za mwisho ni chui