Ziara ya Trump huko Qatar ni kufuru!

Ziara ya Trump huko Qatar ni kufuru!

Well said. Kajirahisisha sana huyu mzee kuzururia vinchi vidogo kisa hongo ndogo ndogo. Hilo tumba la dege ambalo Qatar wanataka kumpa kama zawadi limeshazua mjadala huko Marekani.
Atasaini biashara ya $600+b, unafikiri anazurura bure,nipe nikupe hapo
 
Al-Jazeera inamilikiwa na serikali ya Qatar.

Ukitaka kujua misimamo ya serikali ya Qatar basi tazama Al-Jazeera.

Qatar na Hamas lao moja.
Aljazeera wanafanya kazi ya habari kama inavyopaswa na si aljazeera na Hamas lao moja, habari za uovu wa israel kabla ya mitandao ya kijamii ilikua ikifichwa na mainstream media, aljazeera hawafichi,tumia fuvu lako vizuri
 
Waarabu wanasaini mamikataba makubwa makubwa na USA, pia hizo nchi tatu anazotembelea ni kama wanashindana nani atazidi mwenzake kwenye mapokezi ya kifahari. Trump yuko kimaslahi ya US zaidi ukiangalia mikataba ilosainiwa jana na Saudi Arabia pamoja na mandege ya Boing ambayo Qatar kasaini kuyanunua leo utajua. Hapo bado UAE anafuatia
Saudia kanunua AI hardware kwa $10B toka Amd, same kwa UAE ananunua kwa Nvidia chip laki 5 kwa mwaka kila mwaka hadi 2027. Why wameruhusiwa kununua na nchi zote karibia zote wamepigwa pin kuuziwa Quantity kubwa hivyo?
 
Al-Jazeera inamilikiwa na serikali ya Qatar.

Ukitaka kujua misimamo ya serikali ya Qatar basi tazama Al-Jazeera.

Qatar na Hamas lao moja.
Najua . Israel anachokasirika ni kuona kama marekani atarubuniwa na pesa za Qatar na kuyumbishwa kuhusu misimamo yake dhidi ya Israel. Kumbuka Israel ana ushawishi mkubwa marekani kwa sababu ya pesa za wayahudi wa Marekani. Nilisoma sehemu kumbe Qatar Wana sponsor fedha nyingi kwenye vyuo vikuu vya marekani Hali iliyopelekea maandamano makubwa ya kuipinga Israeli vita yake dhidi ya Gaza. Nilishangaa sanaa
 
AIPAC hufanya lobbying kwa ajili ya israel,na nguvu yao ni kuwafadhili wagombea wakati wa kampeni, JFK alitaka AIPAC ifutwe,wakamng'oa
Na haiwezi kufutwa hiyo... 74yrs na bado itaendelea kuwa na miaka tele huko mbele😅
 
Air Force One kabla haijatua Qatar, ilisindikizwa na F-15 za Qatar.

Walipotua, msafara wa magari uliongozwa na Cybertrucks nyekundu.

Ongezea na askari waliopanda ngamia.

Hawa Qatar naona wanamjua vizuri Trump maana hayo ndo mambo anayoyapenda.

Ukiongeza na lile dege wanalotaka kumpa bure, hawa Qatar wana lao jambo.

Hawafanyi haya mambo yote bila kutegemea chochote toka kwa Trump!


View: https://youtu.be/OSgYXH3Ra7g?si=IEwoXt4e3aQiXGuE

Trump anafanya kama wanavyofanyaga Marais wetu...stroking their egos is the name of the game...
 
Najua . Israel anachokasirika ni kuona kama marekani atarubuniwa na pesa za Qatar na kuyumbishwa kuhusu misimamo yake dhidi ya Israel. Kumbuka Israel ana ushawishi mkubwa marekani kwa sababu ya pesa za wayahudi wa Marekani. Nilisoma sehemu kumbe Qatar Wana sponsor fedha nyingi kwenye vyuo vikuu vya marekani Hali iliyopelekea maandamano makubwa ya kuipinga Israeli vita yake dhidi ya Gaza. Nilishangaa sanaa
Israel haina ushawishi mkubwa kwa Marekani kuzidi ushawishi ambao Marekani inao kwa Israel.

Marekani ikiacha kuifadhili Israel inaweza kufutika katika uso wa dunia.

Marekani ina uwezo wa kumwambia Netanyahu aache kuishambulia Gaza na akaacha kweli.

Bila vifaa vya kijeshi vya Wamarekani, Qatar na Israel hamna kitu.

Marekani ndo mwenye upper hand ikija kwenye bilateral relations na hizo nchi.
 
Waarabu wameanza kuiingilia marekani kama AIPAC,muda si muda ngoma droo,au mwarabu atakua na nguvu zaidi,pesa si ipo
Inaweza kuja kutokea kwa maana naona nao wanachanga karata zao vizuri sana, lakini hata wakifanikiwa ni kama hawatoifaidi vizuri Marekani kwa maana utaona kwamba kitu kikubwa ambacho Trump anakipigania hivi sasa ni kuirudisha heshima ile ambayo walikua nayo duniani kote.

Lakini sasa hivi ni kama nguvu imepungua na kadri siku zinavyokwenda wanazidi kuonekana wa kawaida.
 
Inaweza kuja kutokea kwa maana naona nao wanachanga karata zao vizuri sana, lakini hata wakifanikiwa ni kama hawatoifaidi vizuri Marekani kwa maana utaona kwamba kitu kikubwa ambacho Trump anakipigania hivi sasa ni kuirudisha heshima ile ambayo walikua nayo duniani kote.

Lakini sasa hivi ni kama nguvu imepungua na kadri siku zinavyokwenda wanazidi kuonekana wa kawaida.
MBS kaweka mrija china, urusi na marekani, yaani anakaa kitaalam zaidi, trump anataka economic power tu, USA haiwezi kurudi ilikokua
 
Hivyo ndio inatakiwa, hiyo ndio ile huitwa kunyenga huku mtaani kwetu, kwahiyo jamaa wameanza kumnyenga nyenga raisi wa Dunia kabla hawajaanza kuweka ajenda zao😂😂😂
Unaelewa maana ya kunyenga?
 
MBS kaweka mrija china, urusi na marekani, yaani anakaa kitaalam zaidi, trump anataka economic power tu, USA haiwezi kurudi ilikokua
Basi mudi anachanga karata zake vizuri kama ndio hivyo... Yeah ni ngumu kurudi ilikotoka ila ukishakua na economic power tayari unaweza kufanya lolote duniani kwa maana economic power ndio ambayo imeiweka Marekani kuwa namba moja siku zote.

Nadhani nchi ambayo inampa challenge Marekani kwa sasa hivi ni China.
 
MBS kaweka mrija china, urusi na marekani, yaani anakaa kitaalam zaidi, trump anataka economic power tu, USA haiwezi kurudi ilikokua
MBS ana akili sana anajua jinsi ya kucheza na mataifa makubwa kiuchumi kwenye geopolitics na geoeconomics.

Anazichanga karata zake kwa umakini sana
 
Basi mudi anachanga karata zake vizuri kama ndio hivyo... Yeah ni ngumu kurudi ilikotoka ila ukishakua na economic power tayari unaweza kufanya lolote duniani kwa maana economic power ndio ambayo imeiweka Marekani kuwa namba moja siku zote.

Nadhani nchi ambayo inampa challenge Marekani kwa sasa hivi ni China.
Shida kuna wahuni wanakuja vibaya kiuchumi,teknolojia etc, yaani mambo yamebadilika
 
Nina mwanangu anafanya kazi huko.
Anasema Qatar wanapenda showoff sana tena sana.

Yaani kila ugomvi yeye anataka awapatanishe.

Wewe pigana tu na mimi kesho tunaitwa Qatar kwa gharama zao

Yaishe yasiishe wote tunapewa makazi ya kudumu bure, ila unaondoka na funguo zako
Siku ukija unakuta nyumba yako inakusubiri

Sitanii ni ukweli kabisa
Mr Slim na hasimu wake wa DRC walialikwa na wote wana mijengo yao sasa
Hata Taliban wana ubalozi na nyumba zao pia
Al shabab wapo hata Hamas wana makazi pia
Cheza na Qatar wewe
Hata Trump anaweza kupewa nyumba ya kifahari hapo bila hiyana

Kama ni hela mabilioni yanaingia

Unaweza kuamini hasara waliyoipata kwenye world cup ni mabilioni ya $$$
Ila wanasema faida ilipatikama 22b ila hasara ni mara 10 kwa serikali

Hao ndio Qatar sasa
Wao hela ni mapambo tu
Nilienda mwaka jana
Wametengeneza kisiwa artificial island mjini Doha
Yaani ka mji kadogo ila kamejaa hela
🙋🙋 Salute kwa Quatar
 
Inaweza kuja kutokea kwa maana naona nao wanachanga karata zao vizuri sana, lakini hata wakifanikiwa ni kama hawatoifaidi vizuri Marekani kwa maana utaona kwamba kitu kikubwa ambacho Trump anakipigania hivi sasa ni kuirudisha heshima ile ambayo walikua nayo duniani kote.

Lakini sasa hivi ni kama nguvu imepungua na kadri siku zinavyokwenda wanazidi kuonekana wa kawaida.
😳😳
 
Back
Top Bottom