Ziara ya Trump huko Qatar ni kufuru!

Ziara ya Trump huko Qatar ni kufuru!

Limashaona China imemshinda linataka kuspin issues.

Hilo ni lirahisi HEWA kuwahi kutokea America.
 
Wamefanya homework yao vizuri sana.

Yaani hapo Trump anaweza hata akawapa zile B-52s bure kabisa.
Hivyo ndio inatakiwa, hiyo ndio ile huitwa kunyenga huku mtaani kwetu, kwahiyo jamaa wameanza kumnyenga nyenga raisi wa Dunia kabla hawajaanza kuweka ajenda zao😂😂😂
 
Kuna kuwa na uchumi mkubwa, halafu kuna kuwa na cash ya kutosha ndani..ikiwa una walau idea ya uchumi ni nini
Hebu nipe elimu kidogo hapa hasa ukiangalia hizi nchi mbili.
Maana Marekani wana uchumi mkubwa ila sidhani kama timu zake za mpira wa miguu zaweza shindano na Waarabu kwenye usajili wa wachezaji na matumizi ya fedha.
 
AIPAC, hakuna zaidi
Hii nayo ni moja ya mambo yanayofanya ile hoja yako ya utani ya mwanzo isiwe na nguvu, ofcoz ulirelate ya kwamba nao wakianza kufadhili wagombea but haiwezi kuwa rahisi kiasi hiko AIPAC nadhani imeshajihakikishia uwepo wa kudumu.
 
Nina mwanangu anafanya kazi huko.
Anasema Qatar wanapenda showoff sana tena sana.

Yaani kila ugomvi yeye anataka awapatanishe.

Wewe pigana tu na mimi kesho tunaitwa Qatar kwa gharama zao

Yaishe yasiishe wote tunapewa makazi ya kudumu bure, ila unaondoka na funguo zako
Siku ukija unakuta nyumba yako inakusubiri

Sitanii ni ukweli kabisa
Mr Slim na hasimu wake wa DRC walialikwa na wote wana mijengo yao sasa
Hata Taliban wana ubalozi na nyumba zao pia
Al shabab wapo hata Hamas wana makazi pia
Cheza na Qatar wewe
Hata Trump anaweza kupewa nyumba ya kifahari hapo bila hiyana

Kama ni hela mabilioni yanaingia

Unaweza kuamini hasara waliyoipata kwenye world cup ni mabilioni ya $$$
Ila wanasema faida ilipatikama 22b ila hasara ni mara 10 kwa serikali

Hao ndio Qatar sasa
Wao hela ni mapambo tu
Nilienda mwaka jana
Wametengeneza kisiwa artificial island mjini Doha
Yaani ka mji kadogo ila kamejaa hela
 
Hebu nipe elimu kidogo hapa hasa ukiangalia hizi nchi mbili.
Maana Marekani wana uchumi mkubwa ila sidhani kama timu zake za mpira wa miguu zaweza shindano na Waarabu kwenye usajili wa wachezaji na matumizi ya fedha.
Uchumi ni uzalishaji mali kwa ujumla na mgawanyo wake, marekani ndiyo ana uzalishaji mali mkubwa kuliko waarabu,lakini pesa zipo miongoni mwa raia, ndiyo maana serikali ya marekani inadaiwa matrilioni ya dola,wakati waarabu Wana cash ndani
 
Limashaona China imemshinda linataka kuspin issues.

Hilo ni lirahisi HEWA kuwahi kutokea America.
Well said. Kajirahisisha sana huyu mzee kuzururia vinchi vidogo kisa hongo ndogo ndogo. Hilo tumba la dege ambalo Qatar wanataka kumpa kama zawadi limeshazua mjadala huko Marekani.
 
Air Force One kabla haijatua Qatar, ilisindikizwa na F-15 za Qatar.

Walipotua, msafara wa magari uliongozwa na Cybertrucks nyekundu.

Ongezea na askari waliopanda ngamia.

Hawa Qatar naona wanamjua vizuri Trump maana hayo ndo mambo anayoyapenda.

Ukiongeza na lile dege wanalotaka kumpa bure, hawa Qatar wana lao jambo.

Hawafanyi haya mambo yote bila kutegemea chochote toka kwa Trump!


View: https://youtu.be/OSgYXH3Ra7g?si=IEwoXt4e3aQiXGuE

Bila Marekani si watafurushwa bado kuja kumtembelea mheshimiwa rais daktari profesa Samia Suluhu Hassan
 
Hii nayo ni moja ya mambo yanayofanya ile hoja yako ya utani ya mwanzo isiwe na nguvu, ofcoz ulirelate ya kwamba nao wakianza kufadhili wagombea but haiwezi kuwa rahisi kiasi hiko AIPAC nadhani imeshajihakikishia uwepo wa kudumu.
AIPAC hufanya lobbying kwa ajili ya israel,na nguvu yao ni kuwafadhili wagombea wakati wa kampeni, JFK alitaka AIPAC ifutwe,wakamng'oa
 
Qatar Wana buy influence kwa marekani naona Israel wamemind sana uhusiano unaondelea kwa sasa wa marekani na Qatar. Pesa ina nguvu sanaa
 
Qatar Wana buy influence kwa marekani naona Israel wamemind sana uhusiano unaondelea kwa sasa wa marekani na Qatar. Pesa ina nguvu sanaa
Al-Jazeera inamilikiwa na serikali ya Qatar.

Ukitaka kujua misimamo ya serikali ya Qatar basi tazama Al-Jazeera.

Qatar na Hamas lao moja.
 
Back
Top Bottom