Kakke
JF-Expert Member
- Dec 4, 2010
- 1,883
- 1,482
Wakati umefika wa kila mtu kujitegemea au kujihami mwenyewe kwa lolote lile kwani kwa hali inavyokwenda Zanzibar hapana usalama wa Raia tena! Serikali iliopo imeshindwa na wao binafsi ndio chanzo cha matatizo Zanzibar.
Nasema hivi kwa mantiki ya kwamba Viongozi na Serikali ya Mapinduzi imeshindwa kulinda usalama wa Raia wake matokeo yake wao binafsi wamekuwa ni maadui wa Raia zao, kuwatesa na kuwatupa Magerezani bila hoja na sababu za msingi.
Ushahidi upo kwamba wao ndio wanaoandaa mipango hii yote.
Lengo ni kuifanya Zanzibar kuwa na mtafaruku wa wenyewe kwa wenyewe ili malengo ya Wahafidhina yatimie.
Uamsho ni kisingizio tu lakini kiini cha matatizo haya ni Viongozi wa serikali ya Zanzibar kushikwa shemere na Tanganyika.
Rais ameshindwa kuendesha Serikali badala yake amekuwa ni mshika usukani tu!usukani tu! ambao unaendeshwa kila upande hata kama gari itaingia shimoni,msingini yeye hana habari, alimradi yeye amepinda kona tu.
Nchi kama Nchi haiwezi kuongozwa kwa fitina na majungu kila uchao. Rais Shein Baraza la Mapinduzi na Viongozi wenzake wanashindwa kuelewa kwamba wanawaongoza binaadamu na sio wanyama wana fikra na maarifa yao.
Matukio yote ambayo yanatokea Zanzibar ni njama zilizopangwa na Tanganyika na kupata baraka zote za Wahafidhina ambao hawapo Zanzibar kwa maslahi ya Wananchi bali wapo kwa maslahi yao binafsi. Na yote haya yamekuja kutokana na Wazanzibar kupinga dhulma ya kuporwa kwa Nchi yao.
Wazanzibar wamechoka kutawaliwa na Tanganyika hivi kwa nini hawaachiwi Wazanzibar nnchi yao wakaendesha mambo yao wenyewe?
Viongozi wa juu wa C.C.M wana kila sababu ya kuwadhulumu Wazanzibar kwa vile wao hawana uchungu na Nchi wala na Raia wa zanzibar, Na hao viongozi wengi wao hawana asili ya Zanzibar wamepandikizwa kwa maslahi ya Tanganyika.
Viongozi hao wanafaidika na jasho la Wazanzibari ndio maana Tanganyika kwa kupitia maajenti wao wanafanya kila kinachowezekana kuikaba roho Zanzibar hata kama damu ikimwagika basi wako tayari kwa hilo.
Tukimuangalia Rais wetu tokea hapo awali hakuwa na mvuto lakini pia hao C.C.M wenyewe Zanzibar hawakumpa baraka zao. Kilichotokea ni mabavu na kuwekwa kinguvu na Tanganyika hichi kitu kila mtu anaelewa. Watanganyika walielewa kwamba kazi waliompa Dr Shein ataifanya vilivyo. Wazanzibar kuna mengi bado yanakuja kupitia bwana huyu Mungu tuweke hai tumuone.
Kama ni hivyo sisi kama Wazanzibar tutegemee nini kwa mtu ambae nafasi aliyonayo ni hidaya tu kutoka kwa Mtawala Tanganyika ! Shein kama Shein yupo kwenye kiti kama Punda na hatamu aliebeba mzigo anafuata ,hawashi wala hazimi.
Tumuangalie Seif Iddi naamini hata hilo jina ni la kupanga kwani yeye binafsi hana hata hisia wala maji ya Uzanzibar. Amewekwa pale kuwa kama ni usalama na balozi ambae anaiwakilisha Tanganyika na kutoa Taarifa mihimu kwa Tanganyika. Hapa ndio kiukioni mwa fitina na unyanyasaji kwa upande wa Wazanzibar.
Seif Iddi hayupo Zanzibar kama kiongozi lakini yupo kwa kufanya kazi kama ajenti na Muwakilishi wa Tanganyika. Wazanzibar wasishangae na matusi wala fitina za Balozi huyu kwani yeye hana hasara hata mukichinjana yeye hajali wakati majumba yake ya fahari yako kwao Bara Zanzibar yuko kibaruani tu!
Mukitaka kujua udhaifu na unafiki wa Kiongozi huyu muangalieni kwenye uchaguzi mdogo uliopita pale Bububu jinsi ya hisia zake,alishindwa kujizuia na kutoa yale ambayo yamo kwenye moyo wake,chuki na fitina kwa Wazanzibar.
Kiongozi ambae anashindwa kufuata maadili ya uongozi na badala yake anawachochea Raia zake kufanya fujo na kupigana huku anapongeza na kuwapa baraka zote Wahusika, kweli huyu ni kiongozi muadilifu? Kweli kama si ajenti ni nani twambieni?
Lakini pia hata Elimu yake haifanani na cheo chake. Inakuwaje yeye kama Makamo wa Rais shughuli za Serikali ya Zanzibar azifanyie Tanganyika kwenye Majumba yake binafsi pale Dar na nyingine kule Dodoma, Jee hakuna ofisi Zanzibar kwa Wageni kufikia na kupanga mipango ya Nchi?
Hii ni kuonesha jeuri na ulwa alionao lakini akumbuke ya kwamba iko siku ataulizwa na ajiandae na majibu hivi sasa. Sote tunaelewa kwamba uongozi ni dhamana lakini pia hakuna refu lisilo na mwisho . Viongozi wengi kama yeye wamepita na hivi leo hawatajwi tena ila kilichobaki katika nafsi yao ni majuto na huzuni tu kwa yale walioyafanya.
Tujiulize kiongozi kama huyu ambae ana raslimali chungu mbovu kule Tanganyika ambako ni kwao, kweli atawatetea Wazanzibar wanyonge wanaodai haki zao hapa Zanzibar? Hivi kila siku tutapangiwa Maajenti na Tanganyika na kutunyanyasa mpaka lini na kutuharibia udugu wetu wa asili, hawa akina Seif Iddi ndio wanaoleta ubaguzi Zanzibar.
Angalieni michango ya maafa iliochangiwa ni Mzanzibar gani aliefaidika? Mtu kafiliwa na familia mzima anaenda kupewa ubani laki moja wakati michango ya mabilioni imetolewa, hivi pesa hizi zimetumikaje! Ndio maana Balozi huyu akawa na jeuri kwani mifuko yake imetuna, kwa maana hiyo ana kila sababu kuwagombanisha Wazanzibar.
Tumuangalie Waziri Mohamed Aboud ameingia katika medali ya siasa baada ya kupata ngekewa ya vita vya panzi kupigana, yeye kama Kunguru Rais Karume akampa nafasi. Mheshimiwa huyu hakufanya kosa akatia fitina na baadae kujipendekeza Tanganyika. Kiongozi kama huyu lazima aabudu na asujudu kwa mabwana zake,sishangai kuona anawachukia hata wale watetezi wa uislamu na nchi yetu, analipa fadhila.
Mheshimiwa Mohamed Aboud hana Elimu na ni dhahiri kwamba alifoji hata Elimu yake na hili lipo wazi na ndio sababu hata ya kukosa nafasi ya kupigania kiti cha Urais Zanzibar. Kama sio kashifa hii kuwa wazi wazi basi leo hii Mohammed Aboud angekuwa ameshasimbikwa Urais kwani hapa petu hatuchagui, tunasimbikiwa kutoka Tanganyika tu.
Lakini hili limefumbiwa macho na Tanganyika, kwa sababu Watanganyika lengo lao sio mtu mwenye Elimu Zanzibar akawahangaisha bali wanahitaji mapocho wenye kupenda posho huku Tanganyika ikiendelea na biashara yake "as usual".
Tuangalieni viongozi wengi katika Baraza la kutunga sheria wengi wao hawana Elimu inayohitajika kwa nafasi walizopewa,inakuwaje mtu kujifurahisha na kujitapa na Cheti cha ubaharia, hivi ubaharia na utungaji wa sheria ni wapi na wapi? Yote haya yamepangwa hayakuja kibahati mbaya, Tanganyika wanaelewa wanachokifanya.
Kweli kiongozi kama huyo atakuwa na uwezo wa kuitetea Zanzibar na Wananchi wake au atakuwa yupo kwa maslahi yake binafsi huku akiitikia hewala bwana,alimradi posho inaingia. Hawa ndio wengi wa viongozi wetu wanaoendesha Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Hivi Wananchi wategemee nini kutoka kwao isipokuwa matusi tu na kuiuza Nchi?
Kiongozi kama huyo kweli ataitetea Zanzibar awaudhi mabwana zake walio mchagua na kumpa uwakala wa kuichuuza Zanzibar? hilo haliwezekani abadani! na hawa ndio wengi wao viongozi wetu ndani ya Chama changu nikipendacho cha C.C.M walivyo.
Suala la mageuzi kwao ni mwiko hata kama Zanzibar itaharikishwa na sababu kuwa ni wao basi wako tayari kwa hilo.
Tumtupie macho Dk. Mwinyihaji na udokta wake na vikosi vyake anavyo ongoza.
Kwa kweli ni jambo la kushangaza kuona kwamba mawazo yake na Elimu yake ni vitu tofauti, Anachojali ni maslahi binafsi yeye na familia yake lakini uzalendo wa NCHI yeye hana kabisaa.
Zanzibar ni Visiwa vidogo sana lakini ina vikosi vya ulinzi hata hayo Mataifa makubwa Duniani hayana, hii inakuwaje lengo hapa ni dhulma tu.
Inapofika wakati ukaamrisha vikosi vyako vya ulinzi kuwashambulia Raia wako wewe kama kiongozi unaipeleka Nchi yako wapi? Kimawazo yangu ni kwamba unazidisha uhasama ndani ya jamii,lakini pia wewe kama kiongozi na kiongozi wa Serikali utegemee kuona kama hichi kinachotokea hivi sasa Zanzibar,Vurugu na watu kuteswa bila sababu kosa eti hawautaki Muungano sio haki!
Kinachoendelea hivi sasa Zanzibar ni mipango mahususi ilioandaliwa na yeye akiwa ni muandaaji mkuu wa hayo. Elimu yake ni sawa na punda aliebeba vitabu lakini maskini kilichoandikwa hakijui. Lakini pia cheo na umri wake naona unamkanganya,anahisi ataishi milele,basi sheikh wangu hukumbuki hata akhera yako! mwisho wa yote ni wapi? Hao makachero uliwaleta kutoka Bara ni bure tu Wazanzibar wataendelea kudai haki yao "for sure"
Sasa tuelekee kwa Waimarishaji wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar,hawa ni akina Borafya,Shamte na wenzake hawana hata chembe ya imani,ubinaadam,uungwana nathubutu kusema kwamba ni kondoo waliopotea,hawana huruma kama wao ni miongoni mwa jamii watu. Maisha yao yote ni hasadi,fitina na majungu huku wakifanya dhulma ya kuwafitinisha Wazanzibar.
Umri wangu sio mdogo lakini tokea kuwa na akili yangu timamu sijawahi kuona viongozi wa chama kufanya mikutano na kutukana matusi ya nguoni bila kisisi chochote huku televisheni na vyombo vya habari vikionyesha na kutoa habari hizo. Serikali ina washauri hivi kazi yao hao washauri ni nini? maanake ni dhahiri huku tunakoelekea kwa mtindo wa kina Borafya ni kuelekea Jahhanam.
Hizi sio silka na tamaduni za Wazanzibar na mtu yeyote ambae utamuona anafanya vitendo kama hivyo basi ujue huyo sio Mzanzibar bali ni mtu wa kuja Visiwani na ana lake jambo, kufitinisha na kugombanisha kwa maslahi maalumu au ametumwa kufanya hivyo kwa dhana na malengo maalum,Wazanzibar tusikubali kuelekea huko, tupambane kiume.
Kamishina wa Polisi Zanzibar, Waswahili wana msemo unasema mcheza kwao hutuzwa. Kamishina ni mtu ambae hajui hata uongozi ni kitu, hajui baya wala jema,ni muongo na mnafiki hata sura yake tu ukimuona basi utajua ni mtu wa aina gani? Anashindwa hata kupanga uongo wenye muelekeo. Nilitegemea kuona kiongozi kama huyu anaheshimu cheo chake kama mlinda usalama wa Raia lakini yeye amekuwa msimamiaji wa sera za akina Borafya ndani ya C.C.M.
Kamishina huyu ni bendera inafuata upepo licha ya kufanya kazi kisayansi lakini ni dhahiri kwamba kichwa chake kina uhaba wa Elimu! Elimu yake na majukumu alopewa ni sawa na mbingu na ardhi kwa maana hiyo sishangai sana na jinsi anavyowadhalilisha Wazanzibar wenzake.
Anachojaribu kukifanya ni kujikweza ili aweze kubakia kwenye nafasi aliyopo kwani bila kuwa Mdhabi-dhabina na mnafiki kwenye Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ile ya Tanganyika basi wewe huna nafasi hili linaeleweka.
Nimalizie kwa kusema kwamba Mchimba kisima huingia mwenyewe, Viongozi wa c.c.m na Serikali yetu ya Mapinduzi, imechimba Visima ihakikishe kwamba ikiwa haitakuwa makini basi wataingia wenyewe kwani Wazanzibar wameshachoka na dhulma Zao. Uvumilivu una mwisho wake, hivi sasa Zanzibar imegeuka Paka alofungiwa kwenye chumba na ameshajua kwamba anakufa kwa mateso,hana budi na yeye kujihami kwa njia yeyote ile.
Kutokana na hili ilivyo ikiwa Dokta Shein ataendelea kuongozwa na Tanganyika(Bara) kufuata ushauri wa Wahafidhina kama hivi anavyowafanyia Wazanzibar Muda huu wote, basi na aelewe wazi kwamba atayarishe mageraza mengi kama Firaun na serikali zake lakini Wazanzibar hawatorudi nyuma tena kupigania haki yao ya msingi, Na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar kwanza.
Nasema hivi kwa mantiki ya kwamba Viongozi na Serikali ya Mapinduzi imeshindwa kulinda usalama wa Raia wake matokeo yake wao binafsi wamekuwa ni maadui wa Raia zao, kuwatesa na kuwatupa Magerezani bila hoja na sababu za msingi.
Ushahidi upo kwamba wao ndio wanaoandaa mipango hii yote.
Lengo ni kuifanya Zanzibar kuwa na mtafaruku wa wenyewe kwa wenyewe ili malengo ya Wahafidhina yatimie.
Uamsho ni kisingizio tu lakini kiini cha matatizo haya ni Viongozi wa serikali ya Zanzibar kushikwa shemere na Tanganyika.
Rais ameshindwa kuendesha Serikali badala yake amekuwa ni mshika usukani tu!usukani tu! ambao unaendeshwa kila upande hata kama gari itaingia shimoni,msingini yeye hana habari, alimradi yeye amepinda kona tu.
Nchi kama Nchi haiwezi kuongozwa kwa fitina na majungu kila uchao. Rais Shein Baraza la Mapinduzi na Viongozi wenzake wanashindwa kuelewa kwamba wanawaongoza binaadamu na sio wanyama wana fikra na maarifa yao.
Matukio yote ambayo yanatokea Zanzibar ni njama zilizopangwa na Tanganyika na kupata baraka zote za Wahafidhina ambao hawapo Zanzibar kwa maslahi ya Wananchi bali wapo kwa maslahi yao binafsi. Na yote haya yamekuja kutokana na Wazanzibar kupinga dhulma ya kuporwa kwa Nchi yao.
Wazanzibar wamechoka kutawaliwa na Tanganyika hivi kwa nini hawaachiwi Wazanzibar nnchi yao wakaendesha mambo yao wenyewe?
Viongozi wa juu wa C.C.M wana kila sababu ya kuwadhulumu Wazanzibar kwa vile wao hawana uchungu na Nchi wala na Raia wa zanzibar, Na hao viongozi wengi wao hawana asili ya Zanzibar wamepandikizwa kwa maslahi ya Tanganyika.
Viongozi hao wanafaidika na jasho la Wazanzibari ndio maana Tanganyika kwa kupitia maajenti wao wanafanya kila kinachowezekana kuikaba roho Zanzibar hata kama damu ikimwagika basi wako tayari kwa hilo.
Tukimuangalia Rais wetu tokea hapo awali hakuwa na mvuto lakini pia hao C.C.M wenyewe Zanzibar hawakumpa baraka zao. Kilichotokea ni mabavu na kuwekwa kinguvu na Tanganyika hichi kitu kila mtu anaelewa. Watanganyika walielewa kwamba kazi waliompa Dr Shein ataifanya vilivyo. Wazanzibar kuna mengi bado yanakuja kupitia bwana huyu Mungu tuweke hai tumuone.
Kama ni hivyo sisi kama Wazanzibar tutegemee nini kwa mtu ambae nafasi aliyonayo ni hidaya tu kutoka kwa Mtawala Tanganyika ! Shein kama Shein yupo kwenye kiti kama Punda na hatamu aliebeba mzigo anafuata ,hawashi wala hazimi.
Tumuangalie Seif Iddi naamini hata hilo jina ni la kupanga kwani yeye binafsi hana hata hisia wala maji ya Uzanzibar. Amewekwa pale kuwa kama ni usalama na balozi ambae anaiwakilisha Tanganyika na kutoa Taarifa mihimu kwa Tanganyika. Hapa ndio kiukioni mwa fitina na unyanyasaji kwa upande wa Wazanzibar.
Seif Iddi hayupo Zanzibar kama kiongozi lakini yupo kwa kufanya kazi kama ajenti na Muwakilishi wa Tanganyika. Wazanzibar wasishangae na matusi wala fitina za Balozi huyu kwani yeye hana hasara hata mukichinjana yeye hajali wakati majumba yake ya fahari yako kwao Bara Zanzibar yuko kibaruani tu!
Mukitaka kujua udhaifu na unafiki wa Kiongozi huyu muangalieni kwenye uchaguzi mdogo uliopita pale Bububu jinsi ya hisia zake,alishindwa kujizuia na kutoa yale ambayo yamo kwenye moyo wake,chuki na fitina kwa Wazanzibar.
Kiongozi ambae anashindwa kufuata maadili ya uongozi na badala yake anawachochea Raia zake kufanya fujo na kupigana huku anapongeza na kuwapa baraka zote Wahusika, kweli huyu ni kiongozi muadilifu? Kweli kama si ajenti ni nani twambieni?
Lakini pia hata Elimu yake haifanani na cheo chake. Inakuwaje yeye kama Makamo wa Rais shughuli za Serikali ya Zanzibar azifanyie Tanganyika kwenye Majumba yake binafsi pale Dar na nyingine kule Dodoma, Jee hakuna ofisi Zanzibar kwa Wageni kufikia na kupanga mipango ya Nchi?
Hii ni kuonesha jeuri na ulwa alionao lakini akumbuke ya kwamba iko siku ataulizwa na ajiandae na majibu hivi sasa. Sote tunaelewa kwamba uongozi ni dhamana lakini pia hakuna refu lisilo na mwisho . Viongozi wengi kama yeye wamepita na hivi leo hawatajwi tena ila kilichobaki katika nafsi yao ni majuto na huzuni tu kwa yale walioyafanya.
Tujiulize kiongozi kama huyu ambae ana raslimali chungu mbovu kule Tanganyika ambako ni kwao, kweli atawatetea Wazanzibar wanyonge wanaodai haki zao hapa Zanzibar? Hivi kila siku tutapangiwa Maajenti na Tanganyika na kutunyanyasa mpaka lini na kutuharibia udugu wetu wa asili, hawa akina Seif Iddi ndio wanaoleta ubaguzi Zanzibar.
Angalieni michango ya maafa iliochangiwa ni Mzanzibar gani aliefaidika? Mtu kafiliwa na familia mzima anaenda kupewa ubani laki moja wakati michango ya mabilioni imetolewa, hivi pesa hizi zimetumikaje! Ndio maana Balozi huyu akawa na jeuri kwani mifuko yake imetuna, kwa maana hiyo ana kila sababu kuwagombanisha Wazanzibar.
Tumuangalie Waziri Mohamed Aboud ameingia katika medali ya siasa baada ya kupata ngekewa ya vita vya panzi kupigana, yeye kama Kunguru Rais Karume akampa nafasi. Mheshimiwa huyu hakufanya kosa akatia fitina na baadae kujipendekeza Tanganyika. Kiongozi kama huyu lazima aabudu na asujudu kwa mabwana zake,sishangai kuona anawachukia hata wale watetezi wa uislamu na nchi yetu, analipa fadhila.
Mheshimiwa Mohamed Aboud hana Elimu na ni dhahiri kwamba alifoji hata Elimu yake na hili lipo wazi na ndio sababu hata ya kukosa nafasi ya kupigania kiti cha Urais Zanzibar. Kama sio kashifa hii kuwa wazi wazi basi leo hii Mohammed Aboud angekuwa ameshasimbikwa Urais kwani hapa petu hatuchagui, tunasimbikiwa kutoka Tanganyika tu.
Lakini hili limefumbiwa macho na Tanganyika, kwa sababu Watanganyika lengo lao sio mtu mwenye Elimu Zanzibar akawahangaisha bali wanahitaji mapocho wenye kupenda posho huku Tanganyika ikiendelea na biashara yake "as usual".
Tuangalieni viongozi wengi katika Baraza la kutunga sheria wengi wao hawana Elimu inayohitajika kwa nafasi walizopewa,inakuwaje mtu kujifurahisha na kujitapa na Cheti cha ubaharia, hivi ubaharia na utungaji wa sheria ni wapi na wapi? Yote haya yamepangwa hayakuja kibahati mbaya, Tanganyika wanaelewa wanachokifanya.
Kweli kiongozi kama huyo atakuwa na uwezo wa kuitetea Zanzibar na Wananchi wake au atakuwa yupo kwa maslahi yake binafsi huku akiitikia hewala bwana,alimradi posho inaingia. Hawa ndio wengi wa viongozi wetu wanaoendesha Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.
Hivi Wananchi wategemee nini kutoka kwao isipokuwa matusi tu na kuiuza Nchi?
Kiongozi kama huyo kweli ataitetea Zanzibar awaudhi mabwana zake walio mchagua na kumpa uwakala wa kuichuuza Zanzibar? hilo haliwezekani abadani! na hawa ndio wengi wao viongozi wetu ndani ya Chama changu nikipendacho cha C.C.M walivyo.
Suala la mageuzi kwao ni mwiko hata kama Zanzibar itaharikishwa na sababu kuwa ni wao basi wako tayari kwa hilo.
Tumtupie macho Dk. Mwinyihaji na udokta wake na vikosi vyake anavyo ongoza.
Kwa kweli ni jambo la kushangaza kuona kwamba mawazo yake na Elimu yake ni vitu tofauti, Anachojali ni maslahi binafsi yeye na familia yake lakini uzalendo wa NCHI yeye hana kabisaa.
Zanzibar ni Visiwa vidogo sana lakini ina vikosi vya ulinzi hata hayo Mataifa makubwa Duniani hayana, hii inakuwaje lengo hapa ni dhulma tu.
Inapofika wakati ukaamrisha vikosi vyako vya ulinzi kuwashambulia Raia wako wewe kama kiongozi unaipeleka Nchi yako wapi? Kimawazo yangu ni kwamba unazidisha uhasama ndani ya jamii,lakini pia wewe kama kiongozi na kiongozi wa Serikali utegemee kuona kama hichi kinachotokea hivi sasa Zanzibar,Vurugu na watu kuteswa bila sababu kosa eti hawautaki Muungano sio haki!
Kinachoendelea hivi sasa Zanzibar ni mipango mahususi ilioandaliwa na yeye akiwa ni muandaaji mkuu wa hayo. Elimu yake ni sawa na punda aliebeba vitabu lakini maskini kilichoandikwa hakijui. Lakini pia cheo na umri wake naona unamkanganya,anahisi ataishi milele,basi sheikh wangu hukumbuki hata akhera yako! mwisho wa yote ni wapi? Hao makachero uliwaleta kutoka Bara ni bure tu Wazanzibar wataendelea kudai haki yao "for sure"
Sasa tuelekee kwa Waimarishaji wa Chama cha Mapinduzi Zanzibar,hawa ni akina Borafya,Shamte na wenzake hawana hata chembe ya imani,ubinaadam,uungwana nathubutu kusema kwamba ni kondoo waliopotea,hawana huruma kama wao ni miongoni mwa jamii watu. Maisha yao yote ni hasadi,fitina na majungu huku wakifanya dhulma ya kuwafitinisha Wazanzibar.
Umri wangu sio mdogo lakini tokea kuwa na akili yangu timamu sijawahi kuona viongozi wa chama kufanya mikutano na kutukana matusi ya nguoni bila kisisi chochote huku televisheni na vyombo vya habari vikionyesha na kutoa habari hizo. Serikali ina washauri hivi kazi yao hao washauri ni nini? maanake ni dhahiri huku tunakoelekea kwa mtindo wa kina Borafya ni kuelekea Jahhanam.
Hizi sio silka na tamaduni za Wazanzibar na mtu yeyote ambae utamuona anafanya vitendo kama hivyo basi ujue huyo sio Mzanzibar bali ni mtu wa kuja Visiwani na ana lake jambo, kufitinisha na kugombanisha kwa maslahi maalumu au ametumwa kufanya hivyo kwa dhana na malengo maalum,Wazanzibar tusikubali kuelekea huko, tupambane kiume.
Kamishina wa Polisi Zanzibar, Waswahili wana msemo unasema mcheza kwao hutuzwa. Kamishina ni mtu ambae hajui hata uongozi ni kitu, hajui baya wala jema,ni muongo na mnafiki hata sura yake tu ukimuona basi utajua ni mtu wa aina gani? Anashindwa hata kupanga uongo wenye muelekeo. Nilitegemea kuona kiongozi kama huyu anaheshimu cheo chake kama mlinda usalama wa Raia lakini yeye amekuwa msimamiaji wa sera za akina Borafya ndani ya C.C.M.
Kamishina huyu ni bendera inafuata upepo licha ya kufanya kazi kisayansi lakini ni dhahiri kwamba kichwa chake kina uhaba wa Elimu! Elimu yake na majukumu alopewa ni sawa na mbingu na ardhi kwa maana hiyo sishangai sana na jinsi anavyowadhalilisha Wazanzibar wenzake.
Anachojaribu kukifanya ni kujikweza ili aweze kubakia kwenye nafasi aliyopo kwani bila kuwa Mdhabi-dhabina na mnafiki kwenye Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na ile ya Tanganyika basi wewe huna nafasi hili linaeleweka.
Nimalizie kwa kusema kwamba Mchimba kisima huingia mwenyewe, Viongozi wa c.c.m na Serikali yetu ya Mapinduzi, imechimba Visima ihakikishe kwamba ikiwa haitakuwa makini basi wataingia wenyewe kwani Wazanzibar wameshachoka na dhulma Zao. Uvumilivu una mwisho wake, hivi sasa Zanzibar imegeuka Paka alofungiwa kwenye chumba na ameshajua kwamba anakufa kwa mateso,hana budi na yeye kujihami kwa njia yeyote ile.
Kutokana na hili ilivyo ikiwa Dokta Shein ataendelea kuongozwa na Tanganyika(Bara) kufuata ushauri wa Wahafidhina kama hivi anavyowafanyia Wazanzibar Muda huu wote, basi na aelewe wazi kwamba atayarishe mageraza mengi kama Firaun na serikali zake lakini Wazanzibar hawatorudi nyuma tena kupigania haki yao ya msingi, Na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar kwanza.