ZARI: Hakuna kitu ninachokipenda katika maisha yangu kama kuzaa

Steven mushi mushi

JF-Expert Member
Jul 25, 2016
533
737
Wakati mabinti wengine wakijikita katika matumizi ya mikorogo na kukimbilia wanaume wenye pesa hali ni tofauti kwa mwanamama zari hassan (the boss lady ) ambaye amekiri wazi kuwa kitu anachopenda zaidi katika maisha yake ni kuzaa.

Zari ambaye ni mpenzi wa mwanamziki nyota Africa diamond platnumz amesema hayo ikiwa ni siku chache tangu apate mtoto wa kiume aliyezaa na diamond ambaye watu walimbeza kuwa anazaa bila mpangilio eti kiza tu alibeba ujauzito kabla ya mtoto wao wa kwanza tiffah hajatimiza mwaka mmoja.

Licha ya zari kuwa na watoto watano kwa sasa ameweka wazi kuwa kwa sasa yeye na diamond wana mpango wa kuzaa mtoto mwingine wa tatu na baada ya hapo hatozaa tena na badala yake watajikita zaidi katika kuwalea watoto wao.
 
Diamond alishasema anataka watoto wasiopungua 5 au 6... Mwakani December nadhani tutapokea mdogowake nillan..
 
Reactions: MC7
Labor wards ambassador,kuzaa sana nacho kipaji.
Mimi nimezidisha sana watatu tu.
Hongera zake.
Pole sana...
Kuna zile wanaita bahati mbaya hakutarajia..... huku wa kwanza anamiezi 6'unusu. Then Kitu na Box ya watoto pacha wanne!!.
 
Huyo nae anatumia watoto kama mtaji , chezea child support , eti anapenda kuzaa why hakuzaa na yule mwanamme wake choka mbaya mwenye sixpark?baada ya kutengana na mme wake , kabla hajampata diamond why hakuzaa na hao wanaume?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…