Mpaka Kieleweke
JF-Expert Member
- Feb 27, 2007
- 4,132
- 1,571
Soma hotuba ya kambi ya upinzani hapa ujionee maajabu ya Tanzania; kwa wanaojua mahesabu wanaweza kufanya na kuonyesha hizo ni sawa na kuku ngapi ili kupata tani 100.
4.0 Vibali vya Uagizaji wa Nyama ya Kuku toka Njeya Nchi
Mheshimiwa Spika, taarifa ya Hali ya Uchumi kwa mwaka 2011 imeonyesha kuwa nchi yetu ina kuku takribani 58 milioni ambao wanafugwa hapa nchini mwetu.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kuku wote hao bado wizara hii inaendelea kutoa vibali ya kuagiza nyama ya kuku kutoka Brazili, jambo ambalo ni kinyume cha sheria zetu na matamko mbalimbali ambayo yamekuwa yakitolewa na serikali hapa Bungeni mara kwa mara.
Mheshimiwa Spika, mnamo tarehe 05.04.2012 Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Mifugo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Dr. E. J. Sekidio) alitoa kibali cha kuagiza nyama ya kuku kutoka nchini Brazili kwa kampuni ya Frostan Ltd, ya Jijini DSM kibali chenye namba 000551 cha kuagiza kiasi cha kilo27,100 au tani 27.1 ya nyama zakuku.
Mheshimiwa Spika, mnamo tarehe 20.07.2012 Mkurugenzi Mkuu huyo huyoalitoa kibali kingine chenye namba 00000409 na code namba 0655 kwa kampuni ya MALIK FARAJ CO.LTD cha kuagiza nyama ya kuku kutoka Zanzibar kiasi cha katoni 10,000 zenye kilo 10 kwa kila katoni moja na hivyo ni sawa na kuagiza kilo 100,000 au tani 100 za nyama ya kuku kwa ajili ya migodi ya kuchimba madini ya Barrick.
Kambi Rasmi ya upinzani inataka kupata majibu ya kina kuhusiana na vibali hivi na kama ni sahihi kuendelea kuagiza nyama ya kuku kutoka nje wakati wapo wafugaji wa kuku hapa nchini. Aidha, tunataka kujua nyama za kuku kiasi cha tani 100 zilizoagizwa kutoka Zanzibar ni kutoka nchi gani? Au ni kutoka Zanzibar? Na kama ni kutoka Zanzibar wanahitaji kibali cha kusafirisha nyama kuja bara?
4.0 Vibali vya Uagizaji wa Nyama ya Kuku toka Njeya Nchi
Mheshimiwa Spika, taarifa ya Hali ya Uchumi kwa mwaka 2011 imeonyesha kuwa nchi yetu ina kuku takribani 58 milioni ambao wanafugwa hapa nchini mwetu.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kuku wote hao bado wizara hii inaendelea kutoa vibali ya kuagiza nyama ya kuku kutoka Brazili, jambo ambalo ni kinyume cha sheria zetu na matamko mbalimbali ambayo yamekuwa yakitolewa na serikali hapa Bungeni mara kwa mara.
Mheshimiwa Spika, mnamo tarehe 05.04.2012 Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Mifugo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Dr. E. J. Sekidio) alitoa kibali cha kuagiza nyama ya kuku kutoka nchini Brazili kwa kampuni ya Frostan Ltd, ya Jijini DSM kibali chenye namba 000551 cha kuagiza kiasi cha kilo27,100 au tani 27.1 ya nyama zakuku.
Mheshimiwa Spika, mnamo tarehe 20.07.2012 Mkurugenzi Mkuu huyo huyoalitoa kibali kingine chenye namba 00000409 na code namba 0655 kwa kampuni ya MALIK FARAJ CO.LTD cha kuagiza nyama ya kuku kutoka Zanzibar kiasi cha katoni 10,000 zenye kilo 10 kwa kila katoni moja na hivyo ni sawa na kuagiza kilo 100,000 au tani 100 za nyama ya kuku kwa ajili ya migodi ya kuchimba madini ya Barrick.
Kambi Rasmi ya upinzani inataka kupata majibu ya kina kuhusiana na vibali hivi na kama ni sahihi kuendelea kuagiza nyama ya kuku kutoka nje wakati wapo wafugaji wa kuku hapa nchini. Aidha, tunataka kujua nyama za kuku kiasi cha tani 100 zilizoagizwa kutoka Zanzibar ni kutoka nchi gani? Au ni kutoka Zanzibar? Na kama ni kutoka Zanzibar wanahitaji kibali cha kusafirisha nyama kuja bara?