Zanzibar wanafuga kuku wengi kuliko bara...?

Mpaka Kieleweke

JF-Expert Member
Feb 27, 2007
4,132
1,571
Soma hotuba ya kambi ya upinzani hapa ujionee maajabu ya Tanzania; kwa wanaojua mahesabu wanaweza kufanya na kuonyesha hizo ni sawa na kuku ngapi ili kupata tani 100.


4.0 Vibali vya Uagizaji wa Nyama ya Kuku toka Njeya Nchi

Mheshimiwa Spika, taarifa ya Hali ya Uchumi kwa mwaka 2011 imeonyesha kuwa nchi yetu ina kuku takribani 58 milioni ambao wanafugwa hapa nchini mwetu.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuku wote hao bado wizara hii inaendelea kutoa vibali ya kuagiza nyama ya kuku kutoka Brazili, jambo ambalo ni kinyume cha sheria zetu na matamko mbalimbali ambayo yamekuwa yakitolewa na serikali hapa Bungeni mara kwa mara.

Mheshimiwa Spika, mnamo tarehe 05.04.2012 Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Mifugo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Dr. E. J. Sekidio) alitoa kibali cha kuagiza nyama ya kuku kutoka nchini Brazili kwa kampuni ya Frostan Ltd, ya Jijini DSM kibali chenye namba 000551 cha kuagiza kiasi cha kilo27,100 au tani 27.1 ya nyama zakuku.

Mheshimiwa Spika, mnamo tarehe 20.07.2012 Mkurugenzi Mkuu huyo huyoalitoa kibali kingine chenye namba 00000409 na code namba 0655 kwa kampuni ya MALIK FARAJ CO.LTD cha kuagiza nyama ya kuku kutoka Zanzibar kiasi cha katoni 10,000 zenye kilo 10 kwa kila katoni moja na hivyo ni sawa na kuagiza kilo 100,000 au tani 100 za nyama ya kuku kwa ajili ya migodi ya kuchimba madini ya Barrick.

Kambi Rasmi ya upinzani inataka kupata majibu ya kina kuhusiana na vibali hivi na kama ni sahihi kuendelea kuagiza nyama ya kuku kutoka nje wakati wapo wafugaji wa kuku hapa nchini. Aidha, tunataka kujua nyama za kuku kiasi cha tani 100 zilizoagizwa kutoka Zanzibar ni kutoka nchi gani? Au ni kutoka Zanzibar? Na kama ni kutoka Zanzibar wanahitaji kibali cha kusafirisha nyama kuja bara?
 
Kule Zanzibar ni. Free port ya vitu vingi na si kuku pekeyake. Na ndiyo maana TRA hawapendwi kama sumu Zanzibar. Ubaya zaidi tunaweza letewa kuku kutoka tusipokujua wakapitia Zanzibar na wakatusababishia madhara makubwa kwa afya zetu na mifugo yetu pia, mfano virus cya mafua ya ndege
 
hii inataka kufanana na ile ya nguzo za Tanesco kutoka Africa kusini ,kumbe ni za mufindi!
 
Hata KILA Mazanzibari akifuga kuku 10 kila mmoja(kitu ambacho Wazenj hawakijui) bado wataagiza kuku toka Tangayika.
 
Hata KILA Mazanzibari akifuga kuku 10 kila mmoja(kitu ambacho Wazenj hawakijui) bado wataagiza kuku toka Tangayika.
Kushapigwa na akili zako na chuki binafsi dhidi ya Wazanzibari, utawaona hivohivo lakini chuki zako hazitosaidia kudumaza mawazo yao ya kudai nchi yao.
 
kule zanzibar ni. Free port ya vitu vingi na si kuku pekeyake. Na ndiyo maana tra hawapendwi kama sumu zanzibar. Ubaya zaidi tunaweza letewa kuku kutoka tusipokujua wakapitia zanzibar na wakatusababishia madhara makubwa kwa afya zetu na mifugo yetu pia, mfano virus cya mafua ya ndege

hivi vitu ninanyovitumia hapa bara na vingi vina mazara kwetu! Na tbs wanavialalisha mbona hatuvitazami! Je hivi vinavyo tengenezwa hapa? Nyama tunayokula unaijua usalama wake? Hata huku ndo kubaya kabisa na vitu vinaingia kwa ushuru tena mkubwa na bado ni feki na vinamazara
 
Kushapigwa na akili zako na chuki binafsi dhidi ya Wazanzibari, utawaona hivohivo lakini chuki zako hazitosaidia kudumaza mawazo yao ya kudai nchi yao.

Hatuwezi kuwachukia Wazanzibari bwana , Zanzibar ni nchi atii!
Twasubiri tu biashara ya kuuza kuku kwa dola nchini kwenu.
 
Kushapigwa na akili zako na chuki binafsi dhidi ya Wazanzibari, utawaona hivohivo lakini chuki zako hazitosaidia kudumaza mawazo yao ya kudai nchi yao.

unataka kusema huyo jamaa chuki zake haziwezi kuwadumaza wazanzibari mawazo yao kwa mara ya pili? maana kila mtu anajua kuwa wazenji tayari mawazo yao yashadumaa especially kwa kulalamikia mambo yasiyo na msingi.
 
hii ni rushwa dhahiri. Ukienda wizarani pale wanakuambia hairuhusiwi kuimport kuku sasa vibali vilitolewaje? waziri na kajibu kisanii sana
 
ni ngumu, hizo statistics wanapata wapi?Wapo watu kibao wana kuku kibao tuu hakuna nayehesabu,ila hawa jamaa wanakuja na data zao kimeo.Tatizo ni distribution ya hizo kuku huku bara na consumer kuwa wengi sana.Zenji ni wachache na wana pia mazao ya bahari, huku wengine wakiwa na pato dogo sana kiasi cha kuwafanya wasiwe watumiaji wazuri wa kuku kama si wafugaji.

Hao jama wanaoingiza kuku wana uwanja mpana kama wanaleta kuku ambao ni genetically modified na wanatoak katika nchi ambazo watu wanawafyatua kama kuzalisha nyanya.Bei itakuwa chini sana na pengine wanapewa bei sawa na bure kama kuna mkono wa watafiti ambao hawajapata pa kufanyia huo utafiti.
 
Wote hao wanatoka Brazil lakini wizara ilishasema imesimamisha uagizaji wa kuku kutoka nje ya nchi sasa hivi vibali vilitolewa vipi tena. Pia kama umepata bahati ya kuona hao kuku huwa wanauza 4000 - 5000 na mostly ni majunk. This will definitely killl our Poultry Farming in TZ which has recently employed a lot of Tanzanians.Serikali inatakiwa kulitizama hili swala kwa jicho la tatu na waache Kudanganyika na vijirushwa mbuzi. Huyo Dr Sekidio aweke uzalendo mbele na sio masilahi binafsi.
Waziri nae anasubiri hadi yasemwe Bungeni ndo anatuambia kibali kilikua feki??? what a nonses
 
Soma hotuba ya kambi ya upinzani hapa ujionee maajabu ya Tanzania; kwa wanaojua mahesabu wanaweza kufanya na kuonyesha hizo ni sawa na kuku ngapi ili kupata tani 100.


4.0 Vibali vya Uagizaji wa Nyama ya Kuku toka Njeya Nchi

Mheshimiwa Spika, taarifa ya Hali ya Uchumi kwa mwaka 2011 imeonyesha kuwa nchi yetu ina kuku takribani 58 milioni ambao wanafugwa hapa nchini mwetu.

Mheshimiwa Spika, pamoja na kuku wote hao bado wizara hii inaendelea kutoa vibali ya kuagiza nyama ya kuku kutoka Brazili, jambo ambalo ni kinyume cha sheria zetu na matamko mbalimbali ambayo yamekuwa yakitolewa na serikali hapa Bungeni mara kwa mara.

Mheshimiwa Spika, mnamo tarehe 05.04.2012 Mkurugenzi mkuu wa Idara ya Mifugo, Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Dr. E. J. Sekidio) alitoa kibali cha kuagiza nyama ya kuku kutoka nchini Brazili kwa kampuni ya Frostan Ltd, ya Jijini DSM kibali chenye namba 000551 cha kuagiza kiasi cha kilo27,100 au tani 27.1 ya nyama zakuku.

Mheshimiwa Spika, mnamo tarehe 20.07.2012 Mkurugenzi Mkuu huyo huyoalitoa kibali kingine chenye namba 00000409 na code namba 0655 kwa kampuni ya MALIK FARAJ CO.LTD cha kuagiza nyama ya kuku kutoka Zanzibar kiasi cha katoni 10,000 zenye kilo 10 kwa kila katoni moja na hivyo ni sawa na kuagiza kilo 100,000 au tani 100 za nyama ya kuku kwa ajili ya migodi ya kuchimba madini ya Barrick.

Kambi Rasmi ya upinzani inataka kupata majibu ya kina kuhusiana na vibali hivi na kama ni sahihi kuendelea kuagiza nyama ya kuku kutoka nje wakati wapo wafugaji wa kuku hapa nchini. Aidha, tunataka kujua nyama za kuku kiasi cha tani 100 zilizoagizwa kutoka Zanzibar ni kutoka nchi gani? Au ni kutoka Zanzibar? Na kama ni kutoka Zanzibar wanahitaji kibali cha kusafirisha nyama kuja bara?
Kama mh.alisema kwa usahihi,natilia mashaka hivyo vibali kwenye red,kibali cha tarehe 05/04/2012 ni na.0000551 na cha tarehe 20/07/2012 ni na.0000409,wapi na wapi hizo serial numbers?
 
Wazanzibar wengi wanachukia TRA kwa sababu imegundua janja yao ya kupitisha mizigo kinyemela halafu wanaingizia bara kuna kipindi wakati Nahodha akiwa waziri kiongozi alikuwa na mazungumzo na mabalozi wa Tanzania nje ya nchi na moja ya mambo waliyomuulizia ni kuhusu kuifanya Zanzibar kuwa free port alichowajibu hata Zanzibar ikiwa Free port bado soko lao kubwa linategemea bara.Kwa taarifa hiyo utaona Wazanzibar ndio wanatuhujumu kwa kiasi kikubwa na kwa sababu juzi wamepiga marufuku chakula kuletwa bara nategemea pia watapiga marufuku na hao kuku wasiletwe kwani kama walivyosema serikali yao inajitahidi kuleta chakula kwa bei nafuu lakini wafanyabiashara wanakivusha huku
 
Wazanzibar wengi wanachukia TRA kwa sababu imegundua janja yao ya kupitisha mizigo kinyemela halafu wanaingizia bara kuna kipindi wakati Nahodha akiwa waziri kiongozi alikuwa na mazungumzo na mabalozi wa Tanzania nje ya nchi na moja ya mambo waliyomuulizia ni kuhusu kuifanya Zanzibar kuwa free port alichowajibu hata Zanzibar ikiwa Free port bado soko lao kubwa linategemea bara.Kwa taarifa hiyo utaona Wazanzibar ndio wanatuhujumu kwa kiasi kikubwa na kwa sababu juzi wamepiga marufuku chakula kuletwa bara nategemea pia watapiga marufuku na hao kuku wasiletwe kwani kama walivyosema serikali yao inajitahidi kuleta chakula kwa bei nafuu lakini wafanyabiashara wanakivusha huku
dawa ni kuuvunja muungano.
 
Mkuu rodrick alexander enzi za mzee Ruksa waZanzibar walitugeuza sisi wabara soko lao ndiyo maana leo unasikia kelele nyingi za kutaka rais ajaye atoke Zanzibar ili watunyonye tena.

Wazanzibar wengi wanachukia TRA kwa sababu imegundua janja yao ya kupitisha mizigo kinyemela halafu wanaingizia bara kuna kipindi wakati Nahodha akiwa waziri kiongozi alikuwa na mazungumzo na mabalozi wa Tanzania nje ya nchi na moja ya mambo waliyomuulizia ni kuhusu kuifanya Zanzibar kuwa free port alichowajibu hata Zanzibar ikiwa Free port bado soko lao kubwa linategemea bara.Kwa taarifa hiyo utaona Wazanzibar ndio wanatuhujumu kwa kiasi kikubwa na kwa sababu juzi wamepiga marufuku chakula kuletwa bara nategemea pia watapiga marufuku na hao kuku wasiletwe kwani kama walivyosema serikali yao inajitahidi kuleta chakula kwa bei nafuu lakini wafanyabiashara wanakivusha huku
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom