Zanzibar strikes again !

Haya kuna ile hadithi ya punda aliyetaka kwenda njia mbili,akaishia kufa.Sasa sijui hawa wenzetu wanataka nini?Wakija bara serikali mbili,wakiondoka serikali tatu.Mh!:shock:😕

Miaka 47 sasa hawatoa Mchango kugharamia Muungano , kumbe pesa wanayo? Kama pesa ipo Mbona hawalipi mishahara watumishi wao?hata posho Zimewashinda? Kila kitu Tanganyika ndio analipia ! Pesa za zenji wamehifadhi kwa ajili ya kununulia dhana za kivita kisha wazitumie kudai Uhuru wa kujitenga.
 
Kumbe Zenji ni wajanja saana wao wanabania pesa Yao kwa na kutumia za Tanganyika zao wanatunza kwa ajili ya kununulia Bunduki ili baadae waje kuzitumia kudai Nchi Yao ! Tanganyika sasa amekuwa buzi anachunwa pasipo kujielewa .
 
Uzuri/ubaya wa haya yote wanayasemea wakiwa Mchambawima, lakini wakifika Dodoma wanaufyata. Hizo kelele za Mchambawima ambazo hata mwangi wake haufika Chumbe, hazitunyimi usingizi.
 
Keissy aliwaambi nji nyeupee, jhakuna aliyetoka mjengo! Ungewauliza waikuwa wanasubiri nini, na je walihitaji nguvu za kutoka mjengoni kuelekea bandarini.
 
Wazanzibar ni wazuri sana wa kuongea. Badala ya kununua silaha tungependa wasema, ulinzi na usalama si jambo la muungano. Hapo tungewaelewa. Halafu silaha hazinunuliwi na wabunge, ni dalili za kubweka tu. Lini ulisikia ndani ya bunge la JMT wakitangaza vifaa vyao. Hapa hamuoni kuna kubweka tu siku ipite.

Kuhusu Uraia, hili ni zuri sana. Kwanza wanatakiwa wamwambie Seif na wenzake waliokuja Karimjee kurudisha viyambulisho vya NIDA. Halafu watengeneze vyao. Hilo halina shida.

Hata huko nyuma walikuwa na passport, sijui walitupa wapi.
Hakuna aliyewashia bunduki, walizutupa baharini wenyewe.
Waje KIUTA wachapishe mpya, kila la heri.
 
Zanzibar inawatu wenye msimamo na wanajitambua..
 
Wizara hiyo ina wafanyakazi hewa wanaochukua mishahara tu na wasiijuwa kazi zao, wengi sana
 
Mkuu Mwiba, asante kwa hii!.

Maadam hayo ni maoni tuu ya Wawakilishi, yataendelea kubaki ni maoni tuu!.

Maadamu wamezungumzia kwa mujibu wa sheria!, nashauri anzeni na sheria kwanza ndipo utekelezaji ufuate!.

Kwa mujibu wa sheria, Jeshi ni la JMT!, hao wa huko Zanzibar ni vikosi tuu kama migambo au Ultlmate security, mwisho wa uwezo wao kisheria ni kumili silaka ndogo za kujilinda na sio silaha za vita!. Kama mnataka kuvibadili vikosi vigeuke jeshi, anzeni na kuibadili sheria kuwa Zanzibar nayo iwe na jeshi lake!.

Vivyo hivyo kwenye uraia, uraia bi wa Nchi, JMT!, huko Zanzibar ni ukaazi tuu!. Maadam Mwakilishi katamka vizuri, "huwezi kuwa na nchi bila kuywa na raia!", Zanzibar sio nchi, ni sehemu ya JMT hivyo haiwezi kuwa na raia wake!, raia wote ni wa JMT!, ili Zanzibar iweze kuwa na raia wake, inabisi kwanza iwe nchi!m ndipo ipate raia lakini sivyo kama ilivyo sasa ni "nchi jina tuu!" lakini sii nchi lolote!, sii nchi chochote!, ila kama shida yenu ni jina tuu!, then naiwe!, kitambulisho cha ukaazi wa Zanzibar kiitwe "Kitambulisho cha Raia Wa Nchi ya Zanzibar!", kama tulivyokupeni bendera si mnapeperusha!, na wimbo wa taifa si mnapiga!, kujiita raia wa Zanzibar ruksa, ila vifaru, RPG, mizinga ya kujiandaa kupigana vita na nani?.

Enyi waume mnaomiliki silaha!, inapotokea mkeo nae anaomba na yeye amiliki silaha! na nyite mlale nazo chini ya mito kuna usalama kweli hapo?!.

Mke kazi yake ni kula bure, kulala bure, kuvishwa, kupendezeshwa, umeme bure!, mishahara bure na asilimia 4.5 % ya misaada yote bure na nimesikia sasa ajira ni asilimia 21!%, Mungu akupe nini tena!.

Hongereni!.

Pasco
 
Watanunua na nini hiyo mixinga wakati tunawalipia mishahara ya wafanyakazi SMZ na kuwalipia umeme!
Tatizo Wazenj hawajijui kuwa wameolewa ndani ya muungano mapembe ya kumtishia nani?
 
Hata Asha Bakari akiwa Zanzibar anadai uhuru wa Zanzibar, ila akiwa Dodoma, ujasiri wote unaisha!
 
Keissy aliwaambi nji nyeupee, jhakuna aliyetoka mjengo! Ungewauliza waikuwa wanasubiri nini, na je walihitaji nguvu za kutoka mjengoni kuelekea bandarini.

Kutoka bungeni na kielekea bandarini bado wazanzibar hawajajitoa kwenye himaya ya Tanganyika, kujitoa ni kuvunja muungano huu wa kidhalim ambapo Kessy na Lukuvi walienda makanisani wakasema haiwezekani Zanzibar kupatiwa mamlaka yao, kwa lugha nyengine Tanganyika hawataki Zanzibar iwe huru. Tanganyika ndio kikwazo hamtaki kutuacha munatungangania.
 
Pasco unasemaje? mwanamke inabidi atunzwe.. huyu mke tumemchoka.. tumempa yote lakini bado anataka apewe na silaha.. mdau mmoja kasema ako ka bil 700 kanampa kibri..
 
Last edited by a moderator:

mbona mnafurahia kung'ang'aniwa.. mnapenda sana umeme wa bwelele.. tulia mpate vya bure..ila msilalame hiyo ndio impact ya vya bwelele..
 

hehehe wazenjy bwana kwa kuongea tu hamjambo
 
Ng'ombe tumempa mashudu kwa muda mlefu sana, wacha tumkamue maziwa.. japo ng'ombe mwenyewe kakonda kabaki mifupa mitupu lakini lazima maziwa tuyakamue na yatoke tena yakutosha..
 
mbona mnafurahia kung'ang'aniwa.. mnapenda sana umeme wa bwelele.. tulia mpate vya bure..ila msilalame hiyo ndio impact ya vya bwelele..

Zanzibar ndio nchi pekee ulimwenguni inayonunua umeme ghali kutoka Tanga ambapo huduma hiyo ata nchi za Kenya na nyengine za jirani tungeipata kwa unafuu mara 2 zaidi.,
 

Mkuu zanzibar haijafikisha miaka hamsin ya uhuru bali zanzibar ilikua huru kwa miez mitatu tu. Yaan january to april 1964 kisha ikarud kutawaliwa mpaka leo hii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…