Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Kuna habari za kutatanisha kuwa tayari baraza la wawakilishi la Zanzibar au tunaweza pia kuliita Bunge la Zanzibar wanavutana kuhusu kuvunja Muungano na kundi linaloelekea kushinda ni lile linalotaka iitishwe kura ya maoni kuhusu hatma ya Muungano ,likidai wananchi waliowatuma wanahitaji kura ya maoni kuhusu Muungano ,ili ipatikane ridhaa yao.
Wengine walifika kuhoji mbona Tanzania haijatia saini kuhusu muungano wa East Africa hadi leo ? Wanaogopa kitu gani ?
Pia kuna tetesi kuwa umoja wa serikali ya kitaifa huenda ukavunjika muda si mrefu ,kuna upande utawasilisha na kuanzisha mvutano huo wa kura ya maoni na hapo ndipo tishio la kuvunjika kwa Muungano huo wa GNU.
Kwa kweli WaZanzibari wengi wamechoshwa na Muungano, kwani kuna wastaafu wengi wa kutoka JWTZ ambao nao wameonekana kupanda kwenye viriri wakisema hawalipwi mafao yao na hawana pa kuyadai ,serikali ya Muungano imewatelekeza na kuwatupa.
Kuna tetesi zingine zinasema Maalim Seif atamshauri Dr Shein na pia kuishauri serikali kuitisha kutangaza mgogoro wa Muungano na kuitaka kuitisha kura ya maoni ,ikiwa hoja yake itakataliwa basi atakuwa hana faida ya kubakia hapo alipo kama makamo wa Raisi kwani ni kuwasaliti wananchi.
Wananchi walio wengi wanasikika wakiitajataja hoja ya G55 wakidai kama wao wana makosa basi wale wa G55 nao wafikishwe mahakamani la si hivyo hoja ile itaendelezwa hadi kieleweke ,wengine walihoji kwa nini wabara(TZ) wanaona hayana aibu kuidai au kuishi kama Tanganyika, kwa nini wanaidharau Nchi yao.
Hivi ni WaZanzibari tu ndio wanahamu na kuwa na Taifa lao na kutunza itikadi na silka zao ukichanganyishwa na utamaduni wao ,hawa WaTanganyika wao vipi ? Mbona wanaing'ang'ania Zanzibar na wengine wanafika hata kufurahi unapowaita kuwa wao ni WaZanzibari na kunakuwa na mbinde ukimwita kuwa ni m'bongo ,huku ni kupotoka kwa mtu kudharau chake.
Wengine walifika kuhoji mbona Tanzania haijatia saini kuhusu muungano wa East Africa hadi leo ? Wanaogopa kitu gani ?
Pia kuna tetesi kuwa umoja wa serikali ya kitaifa huenda ukavunjika muda si mrefu ,kuna upande utawasilisha na kuanzisha mvutano huo wa kura ya maoni na hapo ndipo tishio la kuvunjika kwa Muungano huo wa GNU.
Kwa kweli WaZanzibari wengi wamechoshwa na Muungano, kwani kuna wastaafu wengi wa kutoka JWTZ ambao nao wameonekana kupanda kwenye viriri wakisema hawalipwi mafao yao na hawana pa kuyadai ,serikali ya Muungano imewatelekeza na kuwatupa.
Kuna tetesi zingine zinasema Maalim Seif atamshauri Dr Shein na pia kuishauri serikali kuitisha kutangaza mgogoro wa Muungano na kuitaka kuitisha kura ya maoni ,ikiwa hoja yake itakataliwa basi atakuwa hana faida ya kubakia hapo alipo kama makamo wa Raisi kwani ni kuwasaliti wananchi.
Wananchi walio wengi wanasikika wakiitajataja hoja ya G55 wakidai kama wao wana makosa basi wale wa G55 nao wafikishwe mahakamani la si hivyo hoja ile itaendelezwa hadi kieleweke ,wengine walihoji kwa nini wabara(TZ) wanaona hayana aibu kuidai au kuishi kama Tanganyika, kwa nini wanaidharau Nchi yao.
Hivi ni WaZanzibari tu ndio wanahamu na kuwa na Taifa lao na kutunza itikadi na silka zao ukichanganyishwa na utamaduni wao ,hawa WaTanganyika wao vipi ? Mbona wanaing'ang'ania Zanzibar na wengine wanafika hata kufurahi unapowaita kuwa wao ni WaZanzibari na kunakuwa na mbinde ukimwita kuwa ni m'bongo ,huku ni kupotoka kwa mtu kudharau chake.