View attachment 3659469Unaambiwa misimamo ya Dkt. Mwigulu Nchemba, ambayo inaendana na baadhi ya misimamo ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, ndiyo iliyomuibua Ndejembi.
Ni dhahiri kuwa Dkt. Nchimbi angeweza kufukuzwa uanachama kutokana na kukosa uwajibikaji wa pamoja, yaani kuishambulia Serikali ambayo na yeye ni sehemu yake.
Katika mchakato wa kumpata mrithi wake, magenge na makundi mbalimbali yalionya kuwa Mwigulu asipandishwe, wala asifikiriwe kwenye ndoto yake ya 2030, kwa sababu kumpeleka juu huyu ni sawa na kumrudisha Dkt. John Pombe Magufuli.
Kimahesabu, kuletwa kwa Makamu kijana kunaweza kuwa sehemu ya mkakati huo. Za chini chini zinasema kwamba wapo wengine wawili wanaoandaliwa.
Kimahesabu, hii ni mikakati ya kumzuia Dkt. Magufuli huyu mpya.
Watanzania, kama tunataka kumpata Magufuli tena, basi tuziangalie hesabu hizi kwa umakini.