Zamani ilikuwa raha


Hapo kwenye red ulionjapo mtete wa Msukuma?
 
Hapo kwenye red ulionjapo mtete wa Msukuma?

Tulilala ndani ya basi hadi asubuhi......na baridi la moshi na vimini vyetu.....mijamaa ikawa inarandaranda nje ya basi...tukabaki tunakodoleana mimacho tu mpaka asubuhi......ngoma bila bila, unacheza na ulinzi wa walimu wa zamu wa siku hizo nini??? Ukileta mchezo ni nyumbani tu...si kuchekewachekewa kama wanavyofanya ktk shule za sasa!
 
Siku hizi ndo hamna raha wakati huo kila kitu kilikuwa kinasisimua kwani havikuwa vinapatikana kila mahali kama leo. Wali wa maharage ulikuwa mtamu kuliko chipis mayai/kuku leo, hata uji usio na chochote ulikuwa mtamu kuliko uji wa asali leo

Wali maharage bado vipo kila mahali, utamu ni hisia tu na vinginevyo. Kwa maelezo haya dhaifu, nahisi zamani ndo hii ya leo, labda tu facebook, twitter na whatsapp zimeongezeka
 
Duh, foleni za sukari saa tisa za usiku, ikifika asubuhi unapewa betri za Panasonic badala ya sukari nayo ilikuwa raha?
 
Tuliapishwa bila kujua ule wimbo wa-NAAPA NAAHIDI MBELE YA CHAMA;PINDUZI NITAKULINDA MPAKA KUFA najuta sana leo

Wale wote wavuta bangi ccm, wafundishe waelewe vuta sigara, naapa naahidi mbele ya chama mapinduzi nitakulinda mpaka kufa,
 
Mkuu shairi la karudi baba mmoja nililiimba nikiwa darasa la 4 mwaka 2000 ila shairi la sizitaki hizi mbichi sikubahatika emu weka mistari yake!

Dah la 4 juzi mwaka 2000? Mbona juzi tu kaka??? Ila hata hivyo miaka inakimbia mimi hayo mashairi pendwa sana niliyaimba 1992-1993.
 
Udini haukuwepo, Watanzania walipendana na kusaidiana kwa hali na mali bila kujali huyu muislam au mkristo. Hakukuwepo na mafisadi kama ilivyo sasa. Viongozi walikuwa wanaheshimika kwa sababu badala ya kukwapua kwa ajili ya matumbo yao wengi wao walikuwa wanawatumikia Watanzania kwa faida yao na Tanzania. Wauza unga walikuwa hawapo tulikuwa tunasikia tu kwenye taarifa ya habari kuhusu wauza unga wa nchi za nje ambazo zote zilikuwa ni nje ya Afrika. Ikulu iliheshimika na Watanzania sio kama ilivyo sasa imegeuzwa kuwa danguro la mafisadi wanagawana pesa za umma walizokwapua ndani ya Ikulu.
 

- CCM day 5/2 gwaride la chipukizi na kuimba kwaya
- Tarehe 9 mwezi 9 saa 9 dkk 9 sek 9 usiku: kukata form one mikia!
 
Saa hizi Raha..hata hufikiri sana,una-Google tu....hatutoi copy,tunapiga picha na smart phones!!
 
Watu wa zamani mlipata shida sana. Sijui hata mlikuwa mnatongozaje wakati kulikuwa hakuna simu... Inawezekana pia mlikuwa mnachapiana sana.. Na ndio pengine mkafikia hatua ya kutunga ule msemo kuwa "kuchapiwa ni siri ya ndani"
 
Zamani mlikuwa mnasema, Albino hawafi eti wanapotea tuu...kumbe mnawaua..
 
Reactions: awp
waliofeli ndio walienda private schools, ilikuwa aibu mtu kusoma pte school. leo ni sifa kusoma au kusomesha pte schools.

Hii ya juzi hapo 90 huyu mleta mada kwa namna alivyoandika yeye ni miaka ya mwisho ya 80 kurudi nyuma kwa Mwl Nyerere. Kipindi hicho hata private schools sidhani kama zilikuwepo na mara nyingi ilikuwa ukifeli ndio basi tena labda ukarudie darasa sehemu nyingine.
 

Four years!! Mkuu watu wame-date toka shule ya msingi hadi chuo kikuu na hawaoni ndani. Mchezo wanakuja kupewa siku ya ndoa (of coz hizi ni zile extreme cases lakini zilikuwepo za kutosha tu)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…