Mnyalu Junior
JF-Expert Member
- Oct 25, 2012
- 573
- 200
Ni matapeli hao! Usithubutu kutuma hta senti moja! Huyo unayemtaja alishanitumia email km zako hata mimi. Ukihitaji nikuforwadie nitakuforwadia. Kuna rafiki yangu pia alitumiwa email na huyu huyu anayejiita Michel. Mi nilishawajua kitambo coz sio mara ya kwanza kutumiwa email za namna hiyo. Wapo pia wanaojifanyaga wanaishi Senegal Refugee camp. Baba zao waliuawa na wakaacha pesa nyingi. Wanatumia triki ya kuwa wamefall in love na wewe. Wanakuomba uwape full details zako za bank. Baada ya hapo wanakwambia utume kiasi fulani cha pesa ili jaji aidhinishe hizo pesa ziingie kwenye account yako! Ukishatuma hizo pesa ambazo wanadai zinahitajika na Attorney General ili aidhinishe hiyo transaction WANAKATA KABISA mawasiliano na wewe unakuwa ushaibiwa!