Scars
JF-Expert Member
- Apr 8, 2017
- 44,401
- 105,296
Anaandika Zakazakazi,
YANGA SIYO MABINGWA MARA 29 NA SIMBA SIYO MABINGWA MARA 22
Hii ni changamoto kwa wadau wote wa soka nchini Tanzania; wachambuzi, waandishi wa habari, mamlaka za soka na serikali kwa maana ya wizara ya michezo na baraza la michezo.
Fanyeni utafiti na mje na majibu sahihi maana siku zinavyozidi kwenda, uongo unakuwa ukweli kwa sababu watu wanaamini yasiyo sahihi.
Ligi ya Tanzania ilianza mwaka 1965 ikiitwa Klabu Bingwa ya Taifa. Hadi mwaka huu, 2023, ni miaka 58. Maana yake kuna mabingwa 58 wanatakiwa kuwepo.
Sasa kama Yanga ni mabingwa mara 29, Simba mara 22 maana yake hawa wawili peke yao wamechukua ubingwa mara 51.
Katika misimu 58, imebaki misimu 7 pekee ambayo wamechukua wengine.
Hao wengine ni wafuatao.
Cosmopolitan -1 (1967)
Mseto -1 (1975)
Pan African - 1 (1982)
KMKM - 1 (1984)
Majimaji - 3 (1985, 1986 na 1998)
African Sports - 1 (1988)
Malindi - 2 (1989 na 1992)
Pamba - 1 (1990)
TZ Prisons - 1 (1999)
Azam FC - 1 (2014)
Jumla 13
Ukijumlisha na zile 51 za Yanga na Simba, unapata 64...inawezekanaje?
Ligi iliyochezwa miaka 58 inakuwaje na mabingwa 64...hesabu za wapi hizo?
Timu zilizotajwa hapo ndiyo mabingwa wa Tanzania wanaotambuliwa na CAF na FIFA, na ndiyo walioshiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika katika miaka husika.
Ndiyo maana nilianza kwa kutoa changamoto kwa wadau.
Tembeleeni tovuti za CAF na FIFA muone ni timu zipi ziliiwakilisha Tanzania kwenye Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika kuanzia 1965.
UKWELI
Yanga ni mabingwa mara 22 na Simba mara 21.
22+21= 43 - Yanga na Simba
43+13=56 - Jumla (kati ya 58)
NB: Kuna misimu miwili (1970 na 2003) Tanzania hakukuwa na bingwa.
Ndiyo maana unapata mabingwa 56 katika misimu 58.
Itaendelea...
Soma sehemu ya pili hapa
Soma sehemu ya tatu hapa
Soma sehemu ya nne hapa
Soma sehemu ya tano hapa
Soma sehemu ya sita hapa
Soma sehemu ya saba hapa
Soma sehemu ya nane hapa
Soma sehemu ya tisa hapa
YANGA SIYO MABINGWA MARA 29 NA SIMBA SIYO MABINGWA MARA 22
Hii ni changamoto kwa wadau wote wa soka nchini Tanzania; wachambuzi, waandishi wa habari, mamlaka za soka na serikali kwa maana ya wizara ya michezo na baraza la michezo.
Fanyeni utafiti na mje na majibu sahihi maana siku zinavyozidi kwenda, uongo unakuwa ukweli kwa sababu watu wanaamini yasiyo sahihi.
Ligi ya Tanzania ilianza mwaka 1965 ikiitwa Klabu Bingwa ya Taifa. Hadi mwaka huu, 2023, ni miaka 58. Maana yake kuna mabingwa 58 wanatakiwa kuwepo.
Sasa kama Yanga ni mabingwa mara 29, Simba mara 22 maana yake hawa wawili peke yao wamechukua ubingwa mara 51.
Katika misimu 58, imebaki misimu 7 pekee ambayo wamechukua wengine.
Hao wengine ni wafuatao.
Cosmopolitan -1 (1967)
Mseto -1 (1975)
Pan African - 1 (1982)
KMKM - 1 (1984)
Majimaji - 3 (1985, 1986 na 1998)
African Sports - 1 (1988)
Malindi - 2 (1989 na 1992)
Pamba - 1 (1990)
TZ Prisons - 1 (1999)
Azam FC - 1 (2014)
Jumla 13
Ukijumlisha na zile 51 za Yanga na Simba, unapata 64...inawezekanaje?
Ligi iliyochezwa miaka 58 inakuwaje na mabingwa 64...hesabu za wapi hizo?
Timu zilizotajwa hapo ndiyo mabingwa wa Tanzania wanaotambuliwa na CAF na FIFA, na ndiyo walioshiriki Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika katika miaka husika.
Ndiyo maana nilianza kwa kutoa changamoto kwa wadau.
Tembeleeni tovuti za CAF na FIFA muone ni timu zipi ziliiwakilisha Tanzania kwenye Klabu Bingwa/Ligi ya Mabingwa Afrika kuanzia 1965.
UKWELI
Yanga ni mabingwa mara 22 na Simba mara 21.
22+21= 43 - Yanga na Simba
43+13=56 - Jumla (kati ya 58)
NB: Kuna misimu miwili (1970 na 2003) Tanzania hakukuwa na bingwa.
Ndiyo maana unapata mabingwa 56 katika misimu 58.
Itaendelea...
Soma sehemu ya pili hapa
Soma sehemu ya tatu hapa
Soma sehemu ya nne hapa
Soma sehemu ya tano hapa
Soma sehemu ya sita hapa
Soma sehemu ya saba hapa
Soma sehemu ya nane hapa
Soma sehemu ya tisa hapa