Naam,
Unafikiri Kafulila akiambiwa na Rais huyu Adani ni mtu wetu, atatupa mpunga wa kutusaidia kufanyia uchaguzi, Kafulila anaweza kukataa deal?
Unafikiri Kafulila akiambiwa anatakiwa achangishe kiasi fulani kwenye kampeni ya CCM atazitoa mfukoni mwake?
Hivi mnajua CCM huwa inazunguka kwenye taasisi za umma kuchangisha pesa za uchaguzi?
Ataanzia wapi kukataa, Kupewa nafasi tu ndani ya CCM ni msaada kwake. Tunafahamu miaka yote CCM hutumia pesa za umma kufanya kampeni na uchaguzi, kununua wapinzani wao na uchafu kama huo. Ndio maana unakuta wateuliwa wa Taasisi za Umma wako very Royal kwa CCM na viongozi wa Serikali kwasababu ya kulinda matumbo yao na familia zao.
Ndio maana watu wanapoimba KATIBA mpya CCM wanaona kama kelele za mbu, wanaingia ndani ya vyandarua wana mute.
Kikwete Alipojaribu akapelekewa Rasimu iliyopitishwa na Bunge la katiba, aliwadanganya wananchi kwamba sasa wataenda kuipitisha Bunge la JMT, mpaka leo, licha ya wao kuichakachua still wanaiogopa kuileta hivyo hivyo. Kwasababu ilikuwa inawapora silaha zao za kukaa madarakani.
Rais anateuwa kila mtu serikalini, hata wajumbe wa bodi ambao huteuliwa na Mawaziri bado hawapiti bila kuangaliwa na Rais, kwasababu Rais ndiye huteuwa mawaziri, ndio maana wajumbe wa tume ya mawasiliano alio wateuwa Nape akiwa waziri, alipopigwa chini, nawao wakapigwa chini na Rais.
Kafulila akiambiwa achangishe anawafuata wadau wote walioko chini ya ofisi yake, Ukumbuki Nape alivyokuwa Bukoba alisema " Naweza kuyafuata makampuni ya simu yakanipa pesa, kwasababu yako chini ya wizara yangu", the same applied kwa watawala wote walioko Serikalini na ndani ya CCM, na hakuna atakaye kataa.
Zamaani walikwa wakiwakamua Wahindi, siyo kwamba wameacha lakini, wao ndio walikuwa wanajulikana wanapesa, lakini siku hizi wafanya biashara wote ndio mtaji wao, ukikataa TRA, Brela, NIDA na taka taka zote wanakufuata kama kifaranga anavyo shukiwa na mwewe au kipanga.