BRBR unakosea!Huyu jamaa aliahidiwa unaibu katibu mkuu CHADEMA kwani walitaka kumtosa bwana Zitto ili apewe yeye,lakini Zitto alipogundua hilo ndipo akaanza harakati za kuwania uenyekiti.Wazee wa CHADEMA walipoketi na Zitto kumshawishi aachane na kugombea uenyekiti yeye akawajibu mbona swala la kuenguliwa unaibu katibu mkuu na kubandikwa Lwakatare hamlizungumzii!?Hapo mzee Bob Makani akatoa amri kuwa Lwakatare awe mwamasishaji chama Kagera na Zitto aendelee na nafasi yake ya unaibu katibu mkuu.Yaliyotokea wote mmeyaona au kuyasikia sitaki kuyarudia tena,ila kwa taarifa ya jana tuu bwana Lwakatare amekutana na captain Chiligati ktk ukumbi wa Blue Pearl Hotel pale Ubungo plaza kwa mazungumzo yaliyochukua takribani masaa 2,sasa kilichozungumziwa huko ni siri yao ila tutege masikio yetu kwani hawa sisieeemu siwaaamini sana,maana Akwilombe,Tambwe,Atiki,Ngawaiya,Lamwai,Mtemvu,mswanzigwanko...n.k wote walikuwa katika upinzani!