Pole mkuu,huyu dogo ni ndugu yake na Membe,amesoma Libya kama miaka minne,anaongea kiarabu vibaya sana,nilimjua mwaka 2008 tuliishi jirani maeneo ya Mwenge TRA,alikuwa akinifundisha kiarabu.,siku moja tulichelewa street mpaka saa 7 usiku, nilikuwa nakunywa yeye anywi tukipiga story,tukapitiwa na defender la polisi,tukapelekwa kituoni-mabatini,ndo nilijua jamaa sio wa kawaida,2 of alichenjia askari watatu kwa kungfu pale kituoni,mpaka akapigiwa simu mkuu wa kituo saa nane akaja,akamhoji zaidi ya nusu saa,dogo akampiga mkwara mkuu wa kituo kuwa akiamua wote kituoni hawamuwezi kwa mikono au silaha,mwishoni akampa namba mkuu wa kituo aipige apewe maelekezo,mpaka leo sijui ilikuwa namba ya nani,tukaachiwa palepale,baada ya muda tukapoteana,ghafla nakuja kumuona kwenye gazeti kadondoka na Chacha wangwe,Chacha ni.marehemu,gari nyang'anyang'a,yeye mzima hana hata kovu,ana bandeji ya kuzuga mkononi,niliogopa sana,huyu dogo sio.mtu mzuri yupo trained deeply,mpaka leo naamini ana backup ya serikali.Sielewi kwanini alitapeli baadhi ya watu,ila sio mtu mzuri.Story ni ndefu nimeifupisha,pole mkuu.