Yesu ni muongo au wapambe ndo waongo?

Yesu ni muongo au wapambe ndo waongo?

Munch wa Annabelle

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2019
Posts
6,290
Reaction score
10,870
Shalom shalom


Je, Kuna Uthibitisho wa Kihistoria au Kisayansi kwamba Yesu Alijaribiwa na Shetani?

Simulizi la Yesu kujaribiwa na Shetani jangwani ni moja ya hadithi maarufu katika Ukristo. Linaonekana katika vitabu vya Mathayo, Marko, na Luka ndani ya Biblia. Hata hivyo, tukilitazama tukio hili kwa jicho la historia na sayansi, tunakuta changamoto kubwa kuhusu uthibitisho wake.

Kwanza, hakuna rekodi za kihistoria kutoka kwa vyanzo huru kama Warumi au wanahistoria wa wakati huo zinazoelezea tukio hili. Wanahistoria kama Josephus na Tacitus wanamtaja Yesu, lakini hawazungumzii jaribu hilo. Hii inaonyesha kuwa taarifa zote zinazohusu tukio hili zinatoka kwenye maandiko ya kidini pekee.

Pili, tukio lenyewe linasemekana lilitokea faraghani jangwani bila mashahidi wa kibinadamu. Hali hii inafanya iwe vigumu, au hata haiwezekani, kulithibitisha kwa njia ya kihistoria au ushahidi wa moja kwa moja.

Tatu, sayansi hushughulika na mambo yanayoweza kuonekana, kupimwa, au kujaribiwa. Madai ya kiumbe wa kiroho kama Shetani kumjaribu mtu hayawezi kuthibitishwa kwa mbinu za kisayansi. Kwa hiyo, simulizi hili linabaki kuwa suala la imani, si la majaribio au ushahidi wa kisayansi.

Kwa msingi huu, inaweza kusemwa kwamba hakuna uthibitisho wa kihistoria wala wa kisayansi unaounga mkono dai hilo; kilichopo ni maandiko ya imani tu. Hivyo, kulikubali au kulikataa kunategemea zaidi msimamo wa kidini wa mtu binafsi kuliko ushahidi wa kitaaluma.

Nawasubir wala nguruwe
 
Dhana nzima tu ya uwepo wa Yesu ina loopholes nyingi kiasi ukifanya analysis utaona hazikufikishi kwenye jibu la uhakika kwasababu zimegubikwa na hearsay.

Na ile sehemu tata ambayo inaweza kuwa shauku ya wengi kutaka kuyapata majibu, utakuta imewekewa defense ya miujiza ili kurahisisha au itawekewa zuio la "kufuru" kwamba tambua mipaka yako ya kuhoji sio kila swali linaweza kujibika.

Na ndio maana ukiwa mtu wa imani zaidi unakatazwa hata kuhoji chanzo cha Mungu. Unaambiwa ukifanya hivyo hata kwa bahati mbaya unatakiwa ukaungame.

Kwa hiyo ukianza tu ku question ni upi ushahidi ambao ni vivid, testable and undeniable upo unathitisha Yesu yupo/alikuwepo. Ushahidi wao mkubwa wa kwanza utapewa Biblia.

And guess what? In the first place Biblia imewekewa kinga (self-defense) kwamba ili uisome Bible na uielewe kwanza unatakiwa uongozwe na roho mtakatifu na pia uwe na imani.

Hiyo ndio motto yao, wanakwambia vinginevyo hapo utakuwa unasoma Bible kama gazeti.

Nini matokeo yake kwenye hii self defense?

Ni kwamba chochote ambacho utasoma ukaona hii kwa akili za kawaida hai make sense: Utaambiwa haukuwa na imani ambayo ingepelekea uongozwe na roho mtakatifu ambaye angekusaidia ku decipher hizo scriptures.

Hii ni self-defense ambayo inakilinda kitabu na matokeo yeyote yatayokuja always kitabu kipo upande salama so ni either msomaji hajawa guided na holly spirit au ni mpotoshaji tu.

Self-defense hii haitoi room ya kuonekana makosa kwenye kitabu.

Ni mfano na mimi niseme nina uwezo wa kipekee wa kujua taarifa za mtu bila kuambiwa na mtu as long as nitatajiwa jina tu.

Ukanitajia jina, then hapo hapo nikakuambia moja ya sifa yako wewe ni ubishi na haukubali ukiambiwa vitu vya kweli.

Nikaanza kusimulia jinsi migogoro yako ya ndoa wewe na mkeo ilivyoshamiri na namna unavyokosa amani kwenye nyumba yako.

Then wewe ukanikatisha na kupinga huu unabii wangu kwa kusema mimi ni muongo kwasababu haujaoa na sio kweli kuwa una nyumba.

Audience inaweza kuniamini mimi kuwa ni mtabiri wa kweli kuliko wewe, kwasababu nilisha declare mwanzoni kuwa moja ya sifa yako ni ubishi wa kutokubali ukweli so kadri unavyozidi kunipinga unazidi kunifanya nizidi kuaminika kwa watu.

So hiyo ndio trick.
 
Back
Top Bottom