Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,502
- 911,254
kuna watu wana ndoa haina miaka sita lakini kila mtu analala chumba chake, kisa mama keshampata mfanyakazi mwenziwe na anampa vizuri kamjia juu jamaa kila siku ugomvi mwisho jamaa kaona ampishe shetani bora alale chumba cha nje, kwa hiyo unaweza kuona hata mzungu wa nne ni afadhali zaidi.
Ndio maana yake, kaka. Nimeshuhudia. Wapendanao wanashindwana wenyewe, lawama anatupiwa jirani..ooh fulani ananivunjia nyumba... Ukimuuliza huyo fulani, hana hata habari kwamba anavunja nyumba za watu na pengine hata hao wanaovunjiwa nyumba hawafahamu ni kina nani.
Point is, kama una tatizo na mkeo/mumeo jaribuni kujitizama nyie wenyewe na kutambua mapungufu yenu kisha omba msaada utasaidiwa..
Baba mkwe unanipiga sana vita ila kaa ukijua nitakapomsugua binti yako akaniuliza swali ndo itakuwa mwanzo na mwisho wa kukusikiliza wewe. Atajua ulikuwa unamkatazia utamu, utaona kama hata wajukuu zako utaruhusiwa kuwaona.
Sometimes people who are thousands of miles away from u can make u feel better than people right beside you...........Tafakari
Inasikitisha sana, nyumba nzuri, kitanda safi, ukikutana nao mchana unasema hawa wana furaha sana kwenye ndoa yao maana nyuso zina tabasamu utafikiri kweli: ikifika wakati wa kulala kila mtu ana geuka kwakwe!
Asante Rutashubanyuma huu ni ujumbe mzuri!
mkuu Rutashubanyuma mapenzi kizunguzungu mwanzo mnakuwa kwenye dunia nyingine kadri miaka inavyokwenda yanabadilika taratibu hadi kuhama chumba na majina ya kila aina yasiopendeza yale matamu mliokuwa mnaitana hutayasikia lakini sio wote wapo waliobahatika yakaendelea
Inasikitisha sana, nyumba nzuri, kitanda safi, ukikutana nao mchana unasema hawa wana furaha sana kwenye ndoa yao maana nyuso zina tabasamu utafikiri kweli: ikifika wakati wa kulala kila mtu ana geuka kwakwe!
Asante Rutashubanyuma huu ni ujumbe mzuri!