Rutashubanyuma, naomba nikushauri kwa roho safi tu, ingawa mimi sina taaluma ya ushairi lakini kuna maeneo ambayo kwa uelewa kiasi nadhani unahutaji kuyafanyia kazi. Huwa nasikia kwenye mashairi kuna kitu wanaita vina na mizani, mimi sijui hivi ni vitu gani, maana kama nilivyosema mimi sio mtaalamu wa tasnia hii. lakinnadhani huwa ni ile hali ya sauti kufanana fanana hasa kwenye maneno ya mwisho wa kila mstari nitatoa mfano ili nieleweke:
Yako majina ya vitu, mengine yasiyotajwa,
Yashangaza kuna watu, wenye uovu kujawa,
Waona kuwa si kitu, ni kama wanaolipwa,
Thawabu yako motoni, sikia mwenye matusi.
Mtu sio hayawani, anatumia akili,
Kuboboka hadharani, huwa ni kwake katili,
Matusi siwe kinywani, kama lusu tafadhali,
Thawabu yako motoni, sikia mwenye matusi.
Mdomo wako ni moto, wewe mja nakwambiya,
Wanena mambo mazito, hutaki kuyawaziya,
Ulimi wako ufito, mwilini wateketeya,
Thawabu yako motoni, sikia mwenye matusi.
Haya sasa angalia shairi lako hapa chini:
Mlipoanzana sisi, hatukuwepo kabisa!
Mlipotongozana siye hamkutualika!
Mlipokuwa mkibipiana ilikuwa siri yenu!
Mlipokuwa mkikonyezana mlikuwa pweke!
Mlipoanzana kufukuziana hamkutujuza hata!
Yawaje sasa mwapeana migongo,, imekuwaje?
Mlipowekana sawa sote mlitualika!
Mlipovalishana pete ilikuwa karamu!
Mlipovikana vilemba vya ukoka...........
Mlipotumiana posa si mliniita mshenga?
Mlipomiminiana mizawadi mbona furaha?
Yawaje sasa mwapeana migongo,, imekuwaje?
Miaka kweli haina subira, hupeperuka tu!
Miaka kweli imesonga tangia uushike ufyagio!
Miaka kweli imetupa kisogo tangia uuteme ukapera!
Miaka kweli imeishia tangia ufue na kusuuza kufuli zako!
Miaka kweli haichelei tangia uunguze kidole gumba jikoni!
Yawaje sasa mwapeana migongo,, imekuwaje?
Ukiangalia tofauti ya mashairi hayo hapo juu utagundua kuwa la kwako lina mistari mitano katika kila beti wakati hilo lingine lina mistari minne, ambayo nadhani ndio sahihi, yaani inakuwa rahisi kuliimba kishairishairi. ukitaka kujua kama shairi lako linaimbika jaribu kuliimba kwa kutumia sauti ya lile shairi maarufu la sungura la sizitaki mbichi hizi.
Sasa hebu ngoja nijaribu kuli editi shairi lako bila kubadili maana yake japo ubeti mmoja tu:
Mlipoanzana sisi, hatukuwepo kabisa!
Mlipotongozana siye hamkutualika!
Mlipokuwa mkibipiana ilikuwa siri yenu!
Mlipokuwa mkikonyezana mlikuwa pweke!
Mlipoanzana kufukuziana hamkutujuza hata!
Yawaje sasa mwapeana migongo,, imekuwaje?
Wakati mkianzana, peke yenu mlikuwa
Ukope mlipigana, penzi lenu likakuwa
Mahaba mlipeana, taarifa hatukupewa
Ya kupeana migongo, ni wapi yametokea
Nawakilisha.