Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,505
- 911,249
Hicho ni kitanda chako, hakistahili kupeana migongo, lol
Mlipoanzana sisi hatukuwepo kabisa!
Mlipotongozana siye hamkutualika!
Mlipokuwa mkibipiana ilikuwa siri yenu!
Mlipokuwa mkikonyezana mlikuwa pweke!
Mlipoanzana kufukuziana hamkutujuza hata!
Yawaje sasa mwapeana migongo,, imekuwaje?
Mlipowekana sawa sote mlitualika!
Mlipovalishana pete ilikuwa karamu!
Mlipovikana vilemba vya ukoka...........
Mlipotumiana posa si mliniita mshenga?
Mlipomiminiana mizawadi mbona furaha?
Yawaje sasa mwapeana migongo,, imekuwaje?
Miaka kweli haina subira, hupeperuka tu!
Miaka kweli imesonga tangia uushike ufyagio!
Miaka kweli imetupa kisogo tangia uuteme ukapera!
Miaka kweli imeishia tangia ufue na kusuuza kufuli zako!
Miaka kweli haichelei tangia uunguze kidole gumba jikoni!
Yawaje sasa mwapeana migongo,, imekuwaje?
Yaelekea sasa umemchoka na humtaki tena!
Yaelekea sasa umegundua kumbe ni chongo tu!
Yaelekea sasa umetambua havielei hivi hata!
Yaelekea sasa umefumbuka macho, hakuna chenga!
Yaelekea sasa mtaani umeonjeshwa asali na manenge!
Yawaje sasa mwapeana migongo,, imekuwaje?
Zile ahadi na mapochopocho kweli hukumbuki?
Kama kazeeka na wewe je ungali mbichi?
Kama hawaki je na wewe nawe wawaka?
Kama kajiachia na wewe kweli hujioni?
Mbona hivyo walakini wawaka tamaa hivyo?
Yawaje sasa mwapeana migongo,, imekuwaje?