Asanteni nyote.
Hii ni moja wapo ya kazi nzuri sana kuipenda hapa jf.nikishindwa kushukuru sitakuwa na utu.
Safi sana kaka.
Asanteni nyote.
Juzyta khyrnMueke chura kwenye kiti cha dhahabu utamuona ataruka aende kwenye tope hivi ndio baadhi ya watu walivyo, namna utakavyomuenua atarudi mahala anapotoka....
Usimhuzunikie mtu aliyekubadilikia ghafla, huenda ikawa ameacha kujifanyisha.. (pretend)
Mwenyezi Mungu amewaumba malaika wana akili bila ya matamanio, na akawaumba wanyama wana matamanio bila akili, na akamuumba mwanadamu akampa akili na matamanio, basi ambaye akili yake itashinda matamanio yake anaungana na malaika, na ambaye matamanio yake yatashinda akili yake anaungana na wanyama.
Mwanadamu maishani ni kama kalamu (pencil), anachongwa na makosa ili aandike kwa khati nzuri..anaendelea hivi mpaka kalamu iishe na kunabaki mazuri aloyaandika.
Usililie kila kitu kilichopita na iwe ni funzo kwako, hakuna kitu kinakufanya mkubwa isipokuwa maumivu makubwa, na sio kila kuanguka ndio mwisho kwani kuanguka kwa mvua ni mwanzo mwema.
Uslubu wako ni fani: kutangamana na wengine ndio cheo chako, kila uslubu wako ukipanda cheo chako kinapanda.
Wanamsifu mbwa mwitu naye ni hatari kwao, na wanamdharau mbwa naye ni mlinzi wao...watu wengi wanawadharau wanaowahudumia na wanawaheshimu wenye kuwadharau.
Kuwa na mnyama rafiki ni bora kuliko kuwa na rafiki mnyama!!
Nilitabasamu nilipokosa ninachokitaka nikafahamu kuwa Mungu anataka nipate zaidi ya ninachotaka nikatabasamu tena upya...
Ukiumia kwa maumivu ya mwengine basi wewe ni mwema, na ukishiriki katika matibabu yake, basi wewe ni mtukufu...
Juzyta khyran
Mkuu ulichoandika hapa ni chenye thamani kubwa sana,binafsi sina namna ya kuonesha jinsi gani nimeguswa kwa mtizamo chanya na hili bandiko,itoshe tu kukushukuru na kukutakia kila lililo heri katika mambo yako!be blessed!
Mueke chura kwenye kiti cha dhahabu utamuona ataruka aende kwenye tope hivi ndio baadhi ya watu walivyo, namna utakavyomuenua atarudi mahala anapotoka....
Usimhuzunikie mtu aliyekubadilikia ghafla, huenda ikawa ameacha kujifanyisha.. (pretend)
Mwenyezi Mungu amewaumba malaika wana akili bila ya matamanio, na akawaumba wanyama wana matamanio bila akili, na akamuumba mwanadamu akampa akili na matamanio, basi ambaye akili yake itashinda matamanio yake anaungana na malaika, na ambaye matamanio yake yatashinda akili yake anaungana na wanyama.
Mwanadamu maishani ni kama kalamu (pencil), anachongwa na makosa ili aandike kwa khati nzuri..anaendelea hivi mpaka kalamu iishe na kunabaki mazuri aloyaandika.
Usililie kila kitu kilichopita na iwe ni funzo kwako, hakuna kitu kinakufanya mkubwa isipokuwa maumivu makubwa, na sio kila kuanguka ndio mwisho kwani kuanguka kwa mvua ni mwanzo mwema.
Uslubu wako ni fani: kutangamana na wengine ndio cheo chako, kila uslubu wako ukipanda cheo chako kinapanda.
Wanamsifu mbwa mwitu naye ni hatari kwao, na wanamdharau mbwa naye ni mlinzi wao...watu wengi wanawadharau wanaowahudumia na wanawaheshimu wenye kuwadharau.
Kuwa na mnyama rafiki ni bora kuliko kuwa na rafiki mnyama!!
Nilitabasamu nilipokosa ninachokitaka nikafahamu kuwa Mungu anataka nipate zaidi ya ninachotaka nikatabasamu tena upya...
Ukiumia kwa maumivu ya mwengine basi wewe ni mwema, na ukishiriki katika matibabu yake, basi wewe ni mtukufu...