Klabu za Kitayosce na Fountain Gate zafungiwa kusajili wachezaji

Sildenafil Citrate

JF-Expert Member
Jan 29, 2021
573
2,554
IMG_7985.jpeg


Klabu za Kitayosce iliyoko Ligi Kuu ya NBC, na Fountain Gate inayocheza Ligi ya Championship zimefungiwa kusajili wachezaji.

Uamuzi huo umefanywa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) baada ya Kocha Ahmed El Faramawy Youse Mostafa Soliman kushinda kesi za madai dhidi ya klabu hizo.

Kocha huyo raia wa Misri ambaye alizifundisha timu hizo kwa nyakati tofauti alifungua kesi FIFA akipinga kuvunjiwa mikataba kinyume cha taratibu.

Baada ya Soliman kushinda kesi, klabu hizo zilitakiwa ziwe zimemlipa ndani ya siku 45 tangu uamuzi huo ulipotolewa, lakini hazikutekeleza hukumu hizo.

Wakati FIFA imezifungia klabu hizo kufanya uhamisho wa wachezaji kimataifa, Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limezifungia kufanya uhamisho wa ndani.

TFF inazikumbusha klabu kuheshimu mikataba ambayo zimeingia a wachezaji pamoja na makocha ili kuepuka adhabu mbalimbali ikiwemo kufungiwa kusajili.

Iwapo Klabu inataka kuvunja mkataba na mchezaji au kocha, inatakiwa kufanya hivyo kwa kuzingatia taratibu.
 
Hii ni taarifa mbaya kwa viongozi wa hizo timu lakini inaweza kuwa ni njema kwa wachezaji wa Tabora United (Kitayosce zamani).
Hizi timu zikipanda daraja wanaletwaga njemba hata hujui wametokea wapi wakati waliyoipandisha wakitelekezwa wasioneshe vipaji vyao,mpira wa bongo figisu kibao.
 
Yanga nao vipi? Wamelipa deni?
Yanga walishamalizana na yule kocha, so automatic adhabu inakuwa lifted. Hawa hawakumlipa ndani ya ule muda waliopewa, so inachukuliwa kama dharau kwa mamlaka na adhabu inabaki palepale...
 
Back
Top Bottom