John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Ndiyo maana ‘treatment’ ya viongozi wa Serikali huwa ni tofauti na raia wa kawaida lakini tofauti inapozidi na kuonekana haki haijatendeka ndipo shida inapoanzia.
Tanzania inajua Kocha wa Mbeya Kwanza, Mbwana Makata na Meneja David Naftali wa timu yake wamefungiwa kwa kipindi cha miaka mitano kutojihusisha na soka kwa kosa la kushawishi/kuamuru wachezaji wasiingie uwanjani.
Tukio lilitokea katika mchezo dhidi ya Namungo FC mwisho mchezo haukufanyika, Bodi ya Ligi wanasema uchafua taswira ya Ligi na kusababisha hasara kwa wadhamini wa Ligi.
Ukifuatilia hoja za Makata na timu yake zilikuwa za msingi, hata kama kuna makosa walifanya basi labda chanzo ni makosa ya waandaaji wa mchezo pia.
Sababu ilikuwa ni kutokuwepo kwa Ambulance, Bodi ya Ligi wanadai hata wakati gari hilo halipo, kulikuwa na gari lingine la akiba, inachekesha lakini ndio mazingira ya soka letu yalivyo.
Wanasema Ambulance ilirejea uwanjani saa 10:23, Uwanja wanaotumia hauna taa za kumulika usiku ili mchezo uendelee, Bodi ya Ligi walilifikiria hilo? Wamechukua hatua gani kuhusu waratibu wa mechi?
Kuna maswali kadhaa, lakini fuatilia hata wachambuzi wengi wa soka Bongo, habari hiyo kwao imepita kama habari ya matokeo kisha ni wengi wamechana nayo kwa kuwa haina maslahi ya moja kwa moja kwao.
Ni hivi karibuni tu katika mchezo wa Simba na Yanga, kulitokea sintofahamu, Yanga waligomea kucheza katika muda ambao Bodi ya Ligi waliubadilisha muda mfupi kabla ya mechi kutokana na kile walichosema ni sababu ya dharura.
Naamini gharama zilizotumika kwa mchezo huo ni kubwa mara 1000 zaidi ya zile zilizotumika kwa Namungo FC Vs Mbeya Kwanza, lakini Yanga na Simba hakuna hatua zilizochukuliwa za maana, mwisho ni kama TFF na Bodi ya Ligi wao ndio wakapiga magoti mchezo ukapangwa siku nyingine maisha yakaendelea, lakini kina Makata wanapewa adhabu za kumaliza maisha yao ya soka.