Smt016
JF-Expert Member
- Jan 11, 2016
- 2,288
- 3,019
Kiukweli ukiangalia namna GSM na viongozi wa Yanga wanavyoendesha timu kiukweli inashangaza sana. Nilitoa uzi hapa nikiziomba timu zetu zinazowakilisha nchi zijikite kwenye maandalizi ya uhakika kwa kucheza walau mechi zisizopungua nne ili kuimarisha vikosi na pia kuwaweka wachezaji katika fitness, lakini naona Simba, Azam na biashara ndiyo mpaka sasa ndio walionesha kuwekeza kwenye performance ya timu na huku Yanga ikionesha nguvu kubwa kuwekeza kwenye kupiga domo. Una mechi ya klabu bingwa mapema kabisa mwezi wa tisa lakini Cha ajabu hata haujacheza mechi yoyote ya kirafiki unaenda kuweka kambi Morocco kambi ambayo haina impact yoyote zaidi ya kupoteza muda.
Mechi ya wiki ya mwananchi haitokuwa na msaada wowote kiufundi kwasababu wachezaji wengi wa kikosi cha kwanza watakuwa kwenye mataifa yao kucheza mechi za kimataifa. Na la pili hata yakionekana mapungufu una muda mchache sana kurekebisha kabla ya kucheza na Rivers United. Na hauwezi kujua kama imerekebishika pasipo kucheza tena mechi ya kirafiki kuona hali ya kikosi. Kwa upande wa maandalizi ya timu, GSM na viongozi wa Yanga wamefeli. Mimi binafsi ikitokea Yanga imeshindwa kuingia hatua ya makundi klabu bingwa sitolaumu mchezaji yeyote wala benchi la ufundi bali uendeshaji mbovu wa timu hakuna usiriazi kwenye uwekezaji wa uwanjani zaidi ya propaganda tu.
Kituko kingine ni hili la kumkaribisha Haji Manara ndani ya Yanga. Hili binafsi ni moja ya tukio lililonipa mashaka juu ya uwezo wa kufikiria kwa hawa watu wanaoionhoza Yanga. Yaani Manara katoa kila aina ya kejeli, kila aina ya tusi na hao hao Wana Yanga walikuwa wanapiga kelele kuwacheka Simba kuwa wanamsemaji mswahili sana lakini leo kageuka keki Yanga. GSM kawaza kibiashara zaidi lakini atambue kuwa hata Manara alivyokuwa yupo Simba, alifanikiwa kuujaza watu kwasababu ya mpira unaoonekana na matokeo yanayoonekana uwanjani na sio kwamba kupiga domo huku timu ikiwa haifanyi vyema.
Hivyo GSM na uongozi wa Yanga mpira sio kupiga domo na propaganda bali wekeni nguvu kwenye maandalizi ya timu, wekeni nguvu kwenye mpira mzuri na matokeo mazuri hata muhamasishaji hatotumia nguvu nyingi kujaza watu. Ila kama matokeo yatakuwa mabaya uwanjani huyo Manara hatoweza kuwafunga kamba watu wakajaze uwanja.
Mimi binafsi safari hii kama timu haitofika hatua ya makundi klabu bingwa, basi sina budi nikae pembeni ushabiki kwenye timu hii itakuwa basi tena nitarejea baada ya mfumo mpya wa uwekezaji.
Mechi ya wiki ya mwananchi haitokuwa na msaada wowote kiufundi kwasababu wachezaji wengi wa kikosi cha kwanza watakuwa kwenye mataifa yao kucheza mechi za kimataifa. Na la pili hata yakionekana mapungufu una muda mchache sana kurekebisha kabla ya kucheza na Rivers United. Na hauwezi kujua kama imerekebishika pasipo kucheza tena mechi ya kirafiki kuona hali ya kikosi. Kwa upande wa maandalizi ya timu, GSM na viongozi wa Yanga wamefeli. Mimi binafsi ikitokea Yanga imeshindwa kuingia hatua ya makundi klabu bingwa sitolaumu mchezaji yeyote wala benchi la ufundi bali uendeshaji mbovu wa timu hakuna usiriazi kwenye uwekezaji wa uwanjani zaidi ya propaganda tu.
Kituko kingine ni hili la kumkaribisha Haji Manara ndani ya Yanga. Hili binafsi ni moja ya tukio lililonipa mashaka juu ya uwezo wa kufikiria kwa hawa watu wanaoionhoza Yanga. Yaani Manara katoa kila aina ya kejeli, kila aina ya tusi na hao hao Wana Yanga walikuwa wanapiga kelele kuwacheka Simba kuwa wanamsemaji mswahili sana lakini leo kageuka keki Yanga. GSM kawaza kibiashara zaidi lakini atambue kuwa hata Manara alivyokuwa yupo Simba, alifanikiwa kuujaza watu kwasababu ya mpira unaoonekana na matokeo yanayoonekana uwanjani na sio kwamba kupiga domo huku timu ikiwa haifanyi vyema.
Hivyo GSM na uongozi wa Yanga mpira sio kupiga domo na propaganda bali wekeni nguvu kwenye maandalizi ya timu, wekeni nguvu kwenye mpira mzuri na matokeo mazuri hata muhamasishaji hatotumia nguvu nyingi kujaza watu. Ila kama matokeo yatakuwa mabaya uwanjani huyo Manara hatoweza kuwafunga kamba watu wakajaze uwanja.
Mimi binafsi safari hii kama timu haitofika hatua ya makundi klabu bingwa, basi sina budi nikae pembeni ushabiki kwenye timu hii itakuwa basi tena nitarejea baada ya mfumo mpya wa uwekezaji.