Yanayompata Lowassa liwe ni funzo kwa wanaompongeza Rais Magufuli

Kwa haraka haraka ukisikiliza hiyo hadithi ya upande mmoja unaweza kuamini kabisa kwamba cdm hawako tayari mtu kumuunga mkono rais Magufuli. Na iwapo utaamua kuishia na kufanya hitimisho basi utawaona cdm ni chama cha kijinga sana kwa hicho wanachofanya. Ni dhahiri cdm ni wapinzani wa ccm kisiasa, lakini aina ya siasa zinazoendeshwa na awamu hii ya tano kwao siasa ni uadui, na uadui wao uko dhidi ya cdm na hiki ni kitu kilichopandikizwa na rais mwenyewe.

Mh. Lema aliwekwa magereza kwa kile kilicho wazi kwamba ilikuwa maagizo toka juu, na juu panafahamika ni wapi. Wabunge wenzake walio katika kamati ya bunge toka ccm walitaka kwenda kumsalimia, walipata ujumbe toka huko huko juu kwamba kwenda kumsalimia Lema ni usaliti. Hayakuishia hapo, wapinzani hata huko bungeni imetoka amri ya nyuma ya pazia na mbele ya hadhara kwamba washughulikiwe ndani ya bunge na hata nje ya bunge. Na mtoa amri zote hizo anafahamika. Ikatokea Tundu Lissu kapigwa risasi, hakuna mbunge yoyote wa ccm aliyethubutu na aliyethubutu ambaye ni Nyalandu yakamkuta. Spika hajaenda wala wasaidizi wake. Leo kunaletwa maelezo ya upande mmoja ili kupotosha umma kwamba wapinzani wanazuia rais kusifiwa. Lakini ukiangalia sababu yote ya uhasama huu ni rais huyo huyo anayetetewa leo kwa utetezi wa upande mmoja.

Kilichofanyika jana kwa safari ya Lowassa imetajwa kama ya kibinafsi, lakini imetumika kutaka kuonyesha kwamba Lowassa alibeba ujumbe wa wapinzani kitu ambacho si kweli. Hakuna mpinzani anayepinga Lowassa kwenda ikulu, akitaka ahamie hata na familia yake hakuna mwenye shida, lakini mambo yake binafsi yasitumike kama muwakilishi wa wapinzani. Inafahamika wapinzani wana ajenda na malalamiko yao mengi dhidi ya rais huyu. Inasemekana Lowassa aliongea mambo mengi lakini hayajawekwa wazi bali ya kumsifia ndio yamewekwa wazi. Ifahamike Lowassa aliikuta cdm ikiwa taasisi imara, idadi ya wabunge na madiwani waliopatikana sio kwa juhudi za Lowassa maana cdm hakikuwa chama kipya alichoanzisha yeye. Pia naweza kusema Lowassa sio mpinzani bali alikuja upinzani akaelewana na viongozi wachache kwa vipande 30 vya fedha ili apate nafasi ya kugombea urais.

Wanacdm wengi tunaamini ujio wa Lowassa ulipunguza wingi wa kura, idadi ya madiwani na wabunge iliostahiki kupata kutokana na taswira yake mbaya mbele ya jamii. Na tunasema hata baada ya uchaguzi Lowassa hajawahi kutoa mchango wowote wa maana kwa chama. Kama kuna mtu anamtetea aonyeshe hata ofisi ya room 5 aliyojenga tujue kweli alikuja kuinyanyua cdm. Hakuna mwanacdm anayemtukana Lowassa, tunaomba upotoshwaji huo uachwe mara moja bali tunasema Lowassa alienda ikulu kwa mambo yake binafsi na sio ajenda za chama. Na pia tunapenda kusema kwamba Lowassa ndio alileta kura nyingi, wabunge na madiwani wengi sio kweli kwani cdm ilikuwa na mpango kazi wake wa 2010-2015 wa ondoa ccm, ambao Lowassa hakushiriki na matokea ya hiyo 2015 ilikuwa ni matunda ya operation hizo. Asipewe sifa ambazo sio zake.

CC: msemajiukweli, misuli, thetallest, kipara kipya, jingalao
Tanzania imejaa watu wa ajabu sana. Haya mambo wanapotosha kwa faida ya nani? Hivi sisi tuna sifa tofauti na watu wengine ktk hii dunia? Tuna mawazo ya kimaskini ajabuuuu...
Rais wa maskini..
Wananchi wote maskini....
Mawazo yetu ya kimaskini... Kufikiri na kutenda kimaskini...
Kula na kulala kimaskini....
Kufanya kazi kimaskini....
Kutembea kimaskini...
Propaganda za kimaskini....
Uongo nao wa kimaskini....
Daaaaahhh, Eeehhh Mungu wangu....
 
Tu assume uliyoandika in sahihi.Je chadema nao ni ruksa kuwa na tabia chafu kama za ccm?Ni sahihi kufanya upumbavu kwa mgongo wa mbona naye Fulani anafanya?

Misuli kuweka rekodi sawa, aliyeleta uzi ni kama kataka kusadikisha umma kwamba cdm wanawazuia watu wao kumsifia rais. Na akaenda mbali zaidi kwamba yeyote atakayaamua kumsifia Magufuli akiwa cdm yatamkuta yanayomkuta Lowassa. Na ukiangalia kwa jicho la mbali ni kama anataka kuhalalisha haya manunuzi ya wapinzani yanayoitwa kumuunga mkono rais, kwamba kweli ndio sababu inabidi waondoke maana ni kosa kumuunga mkono rais ukiwa upinzani haswa cdm. Tuache upotoshaji, wapinzani hawapingi Lowassa kwenda ikulu, akitaka aenda hata na familia yake na ikiwezekana wakae huko mpaka Magufuli atakapotoka ikulu. Wapinzani wanachopinga ni safari hii kuonekana kama Lowassa ni muwakilishi wao wakati si kweli na aliyoenda kuongea hata yeye kasema ni yake binafsi.
 
Mkuu;
Vijana wa siku hizi nawasikia wana msemo usemao, ''umechanganya madesa''.

Masuala ya kura katika bunge au mabaraza ya madiwani huongozwa na party caucus.

Vyama hukubaliana masuala ya kupigia kura baada ya mjadala ndani ya caucus. Ndio maana unaweza kuona wabunge wa CCM wanaikosoa sana serikali lakini linapofika suala la kupiga kura, hupiga kura kulingana na maamuzi ya caucus.

Kama madiwani wa CCM walijadili na kufikia uamuzi wa kupeleka mgombea wao wa udiwani ili akapigiwe kura halafu kuna baadhi ya wengine hawakufanya hivyo, basi ni lazima waulizwe sababu ya kutopiga kura wakati walikubaliana wote. Hili ni suala la kawaida sana hata kwenye nchi zilizoendelea.

Hapo kwenye nyekundu, kawadanganye wazee wa vijijini wanaotumia simu za torch zile zenye button zilizofutika maandishi huku zimefungwa na rubber band.
 
Baadhi ya wananchi wamekuwa wakijiuliza bila kupata majibu sahihi kuhusu dhana ya baadhi ya madiwani na wabunge kuhama CHADEMA/upinzani na kujiunga CCM ili kuunga mkono juhudi za serikali ya Rais Magufuli au kumpongeza kwa juhudi zake.

Kinachompata Edward Lowassa kutoka kwa baadhi ya viongozi wa juu wa CHADEMA wakisaidiwa na manazi wake baada ya kupongeza juhudi za Rais Magufuli ni jibu linalojitoshereza kuhusu sababu za madiwani na wabunge kuhama kutoka CHADEMA/upinzani kabla ya kuunga juhudi za serikali ya Rais Magufuli.

Edward Lowassa ambaye baadhi ya viongozi wakuu wa CHADEMA/upinzani walikuwa wanatuambia amewasaidia kuwapatia wabunge zaidi ya 110 na maelfu ya madiwani ameshambuliwa kwa maneno ya kejeli na dharau huku wengine wakienda mbali zaidi na kudai aitwe kwenye Kikao cha juu cha CHADEMA ili ahojiwe. Kosa lake ni kuainisha mafanikio ya serikali ya awamu ya tano!

Jaribu kufikiria kama diwani au mbunge wa kawaida angefanya aliyoyafanya Edward Lowassa ya kukutana na Rais Magufuli na kupongeza kazi zake. Nina uhakika angefukuzwa uanachama mara moja na kupoteza udiwani au ubunge au angetengwa na kuitwa msaliti.

Kwa Lowassa hawataweza kutoa onyo au kumfukuza Lowassa mara moja kwa sababu ya pesa aliyowekeza kwa wenye CHADEMA na badala yake wanabaki kulalamika kwenye vyombo vya habari na mitandao kwa kutumia mawakala wao.

Wanachama wanaoifahamu vizuri CHADEMA wanajua kuwa ndani ya CHADEMA kuna wenye CHADEMA na watumishi wa CHADEMA wasio na mkataba.

Yaliyomtokea Diwani wa viti maalum CHADEMA jimbo la Tarime vijijini, Mh Philomena Tontora baada ya kuhudhuria maandamano ya kumpongeza Rais Magufuli ilikuwa ni ishara tosherezi kuwa kama unataka kufukuzwa uanachama wa CHADEMA toa pongezi kwa Rais Magufuli na serikali yake.

Kwa wale wasiofahamu yaliyompata Diwani wa Viti Maalum wa CHADEMA wanaweza kusoma hii thread;
LINK>>Kufilisika kisiasa kwa CHADEMA: Wanataka kumfukuza diwani aliyehudhuria maandamano ya kumpongeza Rais Magufuli

Yanayompata Edward Lowassa liwe ni funzo zuri kwa wale wanadhani wanaweza kupongeza juhudi za serikali au Rais Magufuli na kubaki salama ndani ya CHADEMA/upinzani.

Wanaomshambulia Lowassa ndio hawa hawa kila siku wanatuamisha kuwa wanapigania uhuru wa kutoa mawazo (Freedom of speech) hata kama hukubaliani nayo. Kwa haya wanayomfanyia Lowassa siwezi kuwatofautisha na simba ndani ya ngozi ya kondoo kwenye kelele zao za kutaka uhuru wa kutoa mawazo!
Kuna kitu hujakielewa, unaposifia kosoa pia mapungufu yaliyopo? Huyaoni? Kama yapo unachelea nini? Una mpango wa kuhujumu chama?
 
Kama hii ni hoja yako, kwa hiyo kwa macho ya baadhi ya viongozi wa juu CHADEMA ni kosa kutoa pongezi kwa serikali?
Tabia ya vyama vya siasa inafanana,iki mpiga kura ana haki ya kumpigia kura mtu yeyote anayemtaka kwa nini CCM inamtafuta diwani alieinyima kura?
Vipi kuhusu wabunge waliotaka kwenfa kumuona mbunge mwenzao mahabusu?
Unadhani wabunge wa CCM hawakutaka kwenda Nairobi kumuona Lisu, Ni nani katuletea tabia hii ya kiadui na kishetani kama sio CCM, Unachokiona leo ni makovu ya kilichoanzishwa chini ya utawala huu huwezi kuwachukia watu hadharani kisha utegemee wakupende!
 
Mzee Annael kwanza shikamoo, Makamu wa rais alienda kwenye sherehe za kuapishwa rais wa Kenya hiyo ndio iliyokuwa safari yake ya msingi na wala hakufunga safari ya kwenda kumuona Lissu. Alipokuwa kule, aidha aliguswa, au aliona aibu hili anajua yeye, ndio akaamua kwenda kumsalimu Tundu Lissu. CCM msitafute sifa kwa torch mchana wa jua kali. Kama kuna sifa zenye mashiko wala msingepata shida kuokoteza okoteza.
Marahabaa. Japo nilitaka kwanza kupata usingizi. Kwa namna ninavyokuheshimu imenibidi nijibu hoja yako hii.
Kwanza nakuomba tukubaliane kwa siasa siyo uadui. Sasa nirudi kwenye hoja yako.
Kabla ya kueleza maelezo mengi, ninaomba unipatie mtu mmoja amewahi kusifia utendaji kazi wa serikali ya CCM akiwa ni mwanachama wa CDM akabaki salama. Au uniambie ni nani amewahi kumkosoa Mwenyekiti wa CHADEMA akabaki salama.
Sifa ya CCM ni kukubali kukosolewa na kujirekebisha na kisha kusonga mbele.
Na ikumbukwe upinzani wa kweli umo ndani ya CCM na siyo nje ya CCM. Vilevile kukosoa ndani ya CCM ni njia moja wapo ya kukijenga chama.
mfano Mh Bashe, Mh Nape, Mhe Msukuma nk.
Jana tu Ole Sendeka kaandikiwa barua na Spika wa Bunge kwenda kujieleza kwenye kikao cha maadili.
Spika ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM vilevile na Ole Sendeka. Wote ni wana CCM. Huoni demokrasia na haki ikioneshwa kwa vitendo ndani ya CCM?
Naomba sasa kwa upande wako nioneshe mfano mmoja tu kwa yale niliyosema kutoka CHADEMA.
 
Misuli kuweka rekodi sawa, aliyeleta uzi ni kama kataka kusadikisha umma kwamba cdm wanawazuia watu wao kumsifia rais. Na akaenda mbali zaidi kwamba yeyote atakayaamua kumsifia Magufuli akiwa cdm yatamkuta yanayomkuta Lowassa. Na ukiangalia kwa jicho la mbali ni kama anataka kuhalalisha haya manunuzi ya wapinzani yanayoitwa kumuunga mkono rais, kwamba kweli ndio sababu inabidi waondoke maana ni kosa kumuunga mkono rais ukiwa upinzani haswa cdm. Tuache upotoshaji, wapinzani hawapingi Lowassa kwenda ikulu, akitaka aenda hata na familia yake na ikiwezekana wakae huko mpaka Magufuli atakapotoka ikulu. Wapinzani wanachopinga ni safari hii kuonekana kama Lowassa ni muwakilishi wao wakati si kweli na aliyoenda kuongea hata yeye kasema ni yake binafsi.
Kwa kuweka record vizuri. Lowassa hajasema kuwa ameenda Ikulu kuwakilisha chama. Lowassa kaenda kama yeye. Cha kushangaza kwanini mh. Mbowe anaanza kujitetea? Wakati Lowassa hajaliongelea swala la kuwakilisha chama?
Hapo utagundua mh. Mbowe hataki kabisa mwanachama wake amsifu mkuu wa nchi.
Vilevile kauli hiyo ya Mh. Mbowe imatupatia picha nyingine ya pili kwamba kumbe chama hakina msemaji. Kwamba chochote afanyacho mwanachadema anakuwa ametumwa na chama isipokuwa kumsifu mkuu wa nchi. Kwanini Mh. Mbowe huwa hakanushi taarifa zinazotolewa za matusi, dharau, kejeri, uzushi nk? Inamaana taarifa hizo huwa zimebarikiwa na chama?
 
Marahabaa. Japo nilitaka kwanza kupata usingizi. Kwa namna ninavyokuheshimu imenibidi nijibu hoja yako hii.
Kwanza nakuomba tukubaliane kwa siasa siyo uadui. Sasa nirudi kwenye hoja yako.
Kabla ya kueleza maelezo mengi, ninaomba unipatie mtu mmoja amewahi kusifia utendaji kazi wa serikali ya CCM akiwa ni mwanachama wa CDM akabaki salama. Au uniambie ni nani amewahi kumkosoa Mwenyekiti wa CHADEMA akabaki salama.
Sifa ya CCM ni kukubali kukosolewa na kujirekebisha na kisha kusonga mbele.
Na ikumbukwe upinzani wa kweli umo ndani ya CCM na siyo nje ya CCM. Vilevile kukosoa ndani ya CCM ni njia moja wapo ya kukijenga chama.
mfano Mh Bashe, Mh Nape, Mhe Msukuma nk.
Jana tu Ole Sendeka kaandikiwa barua na Spika wa Bunge kwenda kujieleza kwenye kikao cha maadili.
Spika ni mjumbe wa mkutano mkuu wa CCM vilevile na Ole Sendeka. Wote ni wana CCM. Huoni demokrasia na haki ikioneshwa kwa vitendo ndani ya CCM?
Naomba sasa kwa upande wako nioneshe mfano mmoja tu kwa yale niliyosema kutoka CHADEMA.

Kwanza nikushukuru kwa kuchukua dakika zako chache kunijibu mimi mtu mdogo ambaye sistahili hata kufunga kamba za viatu vyako. Shida ninayoiona kwako ni kufanya kazi moja kwa moja na propaganda za huku mitandaoni kisha kugeuza ndio sehemu ya kujengea hoja zako. Kama ni kutaja naweza kukutajia mtu lakini napaswa kuvuka sifa ya mtu mmoja mmoja. Mfano wa watu hao waliosifia na wanaosifia kisha wakabaki kubaki ndani ya cdm ni Mh. Nassary, Meya wa jiji la Arusha nk. Halafu nikuambie kitu mzee Annael, wapinzani sio juu yao kusifia, hata wakikaa kimya bila kukosoa jambo zuri ni sifa pia. Kwa tabia zetu sisi watanzania hatuna uwezo wa kumsifia mpinzani wako na mara nyingi hufanyika kinafiki.

Umejaribu kuweka sifa nyingi kwamba ccm inajirekebisha na kukubali kukosolewa, hizo sifa umezitoa kama kasuku, Huyo Bashe na Nape michango yao ya kukosoa ndani ya bunge rais alimtuma waziri Mpango kwa ujumbe ulioonyeshwa kukerwa na michango yao bungeni. Labda unapoteza kumbukumbu. Muheshimiwa msukuma huwa hakosoi serekali bali huwa anawakejeli mawaziri anaohitilifiana nao. Jijengee utaratibu wa kuelewa tabia ya mtu kabla ya kudhani ni mkosoaji.

Halafu hilo la Sendeka naona kama umejichanga muktadha wake. Ole Sendeka anaitwa sio kwasababu ccm inakubali kukosolewa, ila anaenda kuhojiwa ni kwanini amekosoa kwa kuliponda bunge. Ilibidi kama ccm inakubali kukosolewa wakiri kuupata ujumbe wa Sendeka na kumwambia kama kuna mapungufu watafanyia kazi. Kumuita ni kwenda kumpa vitisho. Naomba nisiibe muda wako wa kupumzika, tutaendelea kesho, nakutakia usiku mwema.
 
Kwanza nikushukuru kwa kuchukua dakika zako chache kunijibu mimi mtu mdogo ambaye sistahili hata kufunga kamba za viatu vyako. Shida ninayoiona kwako ni kufanya kazi moja kwa moja na propaganda za huku mitandaoni kisha kugeuza ndio sehemu ya kujengea hoja zako. Kama ni kutaja naweza kukutajia mtu lakini napaswa kuvuka sifa ya mtu mmoja mmoja. Mfano wa watu hao waliosifia na wanaosifia kisha wakabaki kubaki ndani ya cdm ni Mh. Nassary, Meya wa jiji la Arusha nk. Halafu nikuambie kitu mzee Annael, wapinzani sio juu yao kusifia, hata wakikaa kimya bila kukosoa jambo zuri ni sifa pia. Kwa tabia zetu sisi watanzania hatuna uwezo wa kumsifia mpinzani wako na mara nyingi hufanyika kinafiki.

Umejaribu kuweka sifa nyingi kwamba ccm inajirekebisha na kukubali kukosolewa, hizo sifa umezitoa kama kasuku, Huyo Bashe na Nape michango yao ya kukosoa ndani ya bunge rais alimtuma waziri Mpango kwa ujumbe ulioonyeshwa kukerwa na michango yao bungeni. Labda unapoteza kumbukumbu. Muheshimiwa msukuma huwa hakosoi serekali bali huwa anawakejeli mawaziri anaohitilifiana nao. Jijengee utaratibu wa kuelewa tabia ya mtu kabla ya kudhani ni mkosoaji.

Halafu hilo la Sendeka naona kama umejichanga muktadha wake. Ole Sendeka anaitwa sio kwasababu ccm inakubali kukosolewa, ila anaenda kuhojiwa ni kwanini amekosoa kwa kuliponda bunge. Ilibidi kama ccm inakubali kukosolewa wakiri kuupata ujumbe wa Sendeka na kumwambia kama kuna mapungufu watafanyia kazi. Kumuita ni kwenda kumpa vitisho. Naomba nisiibe muda wako wa kupumzika, tutaendelea kesho, nakutakia usiku mwema.
Na wewe pia. Kesho nayo siku. Japo mimi siyo mpiga propaganda wa kwenye mitandao ni mtu ninayeongea facts tupu. Kesho jioni baada ya kazi suala hili tulijadili kwa kina. Aliyeanzisha mada ailete na atuite tuidadavue pasipo matusi na vijembe.
 
Kwa kuweka record vizuri. Lowassa hajasema kuwa ameenda Ikulu kuwakilisha chama. Lowassa kaenda kama yeye. Cha kushangaza kwanini mh. Mbowe anaanza kujitetea? Wakati Lowassa hajaliongelea swala la kuwakilisha chama?
Hapo utagundua mh. Mbowe hataki kabisa mwanachama wake amsifu mkuu wa nchi.
Vilevile kauli hiyo ya Mh. Mbowe imatupatia picha nyingine ya pili kwamba kumbe chama hakina msemaji. Kwamba chochote afanyacho mwanachadema anakuwa ametumwa na chama isipokuwa kumsifu mkuu wa nchi. Kwanini Mh. Mbowe huwa hakanushi taarifa zinazotolewa za matusi, dharau, kejeri, uzushi nk? Inamaana taarifa hizo huwa zimebarikiwa na chama?

Samahani mzee Annael, napenda uchangiaji wako lakini naona unaelewa kwa kukengeuka ama itikadi yako inakufanya kuangalia kwa makengeza. Ni kweli Mbowe alipaswa kutokuonyesha tahamaki hadharani kwa hiyo safari ya Lowassa ndani ya Ikulu kwani jana yake walikuwa pamoja walipoenda kumtembelea Kingunge hospital. Katika mazingira ya kawaida na aina ya mtu Lowassa aliyeenda kuonana naye alipaswa hata kumbrief kwamba kesho nitamuona jamaa ila kwa suala la kibinafsi.

Kumbuka Lowassa ni mjumbe wa kamati kuu cdm na ndiye alipewa nafasi ya kugombea urais tena kwa upendeleo kupitia Mbowe, wangalau alipaswa kujua kwamba anabeba status ya chama haswa wakati huu vyama hivi na rais mwenyewe akitazamwa kwa jicho la shaka dhidi ya wainzani hususani cdm. Kumsifu Magufuli haikuwa kosa hilo nikiri na wala kwa Mbowe haikuwa shida, ila Mbowa alichosema safari ya Lowassa ikulu ilikuwa ya kificho, lakini inatumika kama msimamo wa chama hasa ukizingatia kilichopolekwa kwa jamii ni sifa wakati wapinzani na Lowassa akiwepo wanaugulia maumivu na kutotendewa haki. Basi wangalau ingeonyeshwa mbali ya sifa kwa rais, pia kwenye mazungumzo hayo kuna mambo ya kilio cha upinzani yatafanyiwa kazi. Tuwe wakweli tu ndugu yangu Annael, mimi naishi na wewe nyumba moja ama hata kufanya kazi na wewe, inatokea unaenda kumuona rais kesho yake lakini usiniambie, au ndio hizo surprise? Kwa safari nyeti hivyo na hali halisi ilivyo ilikuwa ni vyema kwenda bila kumuambia mkuu wako wa chama? Nikupe mfano mrahisi, hivi leo ikitokea PM Majaliwa yuko na Rais, halafu kesho yake rais anasikia waziri mkuu kakutana na Mbowe na kamsifia jinsi chama chake kinavyokuwa rais atamueleweje?
 
Na wewe pia. Kesho nayo siku. Japo mimi siyo mpiga propaganda wa kwenye mitandao ni mtu ninayeongea facts tupu. Kesho jioni baada ya kazi suala hili tulijadili kwa kina. Aliyeanzisha mada ailete na atuite tuidadavue pasipo matusi na vijembe.

Amen
 
Lowassa bado ni kiongozi kwenye taifa hili hivyo kwenda Ikulu ni jambo la kawaida. Pia kupongeza kwa mazuri sio vibaya.
Kuna baadhi ya watu hawataki kuelewa angalizo lako lakini hata kama Lowassa angekuwa sio kiongozi kitaifa angekuwa na haki ya kutoa mawazi yake kuhusu serikali.
 
Samahani mzee Annael, napenda uchangiaji wako lakini naona unaelewa kwa kukengeuka ama itikadi yako inakufanya kuangalia kwa makengeza. Ni kweli Mbowe alipaswa kutokuonyesha tahamaki hadharani kwa hiyo safari ya Lowassa ndani ya Ikulu kwani jana yake walikuwa pamoja walipoenda kumtembelea Kingunge hospital. Katika mazingira ya kawaida na aina ya mtu Lowassa aliyeenda kuonana naye alipaswa hata kumbrief kwamba kesho nitamuona jamaa ila kwa suala la kibinafsi.

Kumbuka Lowassa ni mjumbe wa kamati kuu cdm na ndiye alipewa nafasi ya kugombea urais tena kwa upendeleo kupitia Mbowe, wangalau alipaswa kujua kwamba anabeba status ya chama haswa wakati huu vyama hivi na rais mwenyewe akitazamwa kwa jicho la shaka dhidi ya wainzani hususani cdm. Kumsifu Magufuli haikuwa kosa hilo nikiri na wala kwa Mbowe haikuwa shida, ila Mbowa alichosema safari ya Lowassa ikulu ilikuwa ya kificho, lakini inatumika kama msimamo wa chama hasa ukizingatia kilichopolekwa kwa jamii ni sifa wakati wapinzani na Lowassa akiwepo wanaugulia maumivu na kutotendewa haki. Basi wangalau ingeonyeshwa mbali ya sifa kwa rais, pia kwenye mazungumzo hayo kuna mambo ya kilio cha upinzani yatafanyiwa kazi. Tuwe wakweli tu ndugu yangu Annael, mimi naishi na wewe nyumba moja ama hata kufanya kazi na wewe, inatokea unaenda kumuona rais kesho yake lakini usiniambie, au ndio hizo surprise? Kwa safari nyeti hivyo na hali halisi ilivyo ilikuwa ni vyema kwenda bila kumuambia mkuu wako wa chama? Nikupe mfano mrahisi, hivi leo ikitokea PM Majaliwa yuko na Rais, halafu kesho yake rais anasikia waziri mkuu kakutana na Mbowe na kamsifia jinsi chama chake kinavyokuwa rais atamueleweje?
Japo natamani kuijibu hii comment, nasita kidogo. Ngoja nijibu tu kidogo kwa ufupi.
Mh. Mbowe alikuwa na haraka gani kujibu kwenye public? Kwanini asisubiri akutane na Lowassa kwanza? Hapa inajenga picha kwamba Mbowe hana uwezo wa kubeba mambo kifuani, yaani ni mwepesi sana. Na kwa namna hiyo tunaweza kukubaliana mimi na wewe kwamba Mbowe alikuwa anajificha kwenye mgongo wa Dr. Slaa, kwamba Dr. Slaa amewahi kuwa kiongozi wa dini anakifua cha kutunza mambo kusubiri wakati mwafaka. Hapo inabidi mimi na wewe tukubaliane kuwa hiyo ndiyo true color ya Mbowe.
Hayo mambo ya kwamba mlikuwa pamoja jana ni ya kwenu ndani haitakiwi kuyaweka kwenye public, ni udhaifu mkubwa sana wa kisiasa. Mbowe anauwezo wa kuitisha kikao na kuyazungumza ndani ya chama. Je, yale aliyoyaongea mbowe ni makubaliano ya chama? Chama ni taasisi inaongozwa kwa vikao. Hii inaonesha kuwa Mh. Mbowe hana kifua cha kubeba mambo. Na ukichimba zaidi utaona jamaa anabeba mambo personal.
Hakukuwa na ulazima wa Mwenyekiti wa chama kutolea maelezo jambo hilo. Kwahiyo Mbowe ameonesha udhaifu wa hali ya juu wa kiuongozi. Mbowe anahitaji mshauri mwenye utashi na siyo Lema.
 
Umewahi kuona hata kwa bahati mbaya lowasa amevaa sare ya cdm yeyote huyo bado ni ccm damu muda wowote anarejea nymbni
 
Japo natamani kuijibu hii comment, nasita kidogo. Ngoja nijibu tu kidogo kwa ufupi.
Mh. Mbowe alikuwa na haraka gani kujibu kwenye public? Kwanini asisubiri akutane na Lowassa kwanza? Hapa inajenga picha kwamba Mbowe hana uwezo wa kubeba mambo kifuani, yaani ni mwepesi sana. Na kwa namna hiyo tunaweza kukubaliana mimi na wewe kwamba Mbowe alikuwa anajificha kwenye mgongo wa Dr. Slaa, kwamba Dr. Slaa amewahi kuwa kiongozi wa dini anakifua cha kutunza mambo kusubiri wakati mwafaka. Hapo inabidi mimi na wewe tukubaliane kuwa hiyo ndiyo true color ya Mbowe.
Hayo mambo ya kwamba mlikuwa pamoja jana ni ya kwenu ndani haitakiwi kuyaweka kwenye public, ni udhaifu mkubwa sana wa kisiasa. Mbowe anauwezo wa kuitisha kikao na kuyazungumza ndani ya chama. Je, yale aliyoyaongea mbowe ni makubaliano ya chama? Chama ni taasisi inaongozwa kwa vikao. Hii inaonesha kuwa Mh. Mbowe hana kifua cha kubeba mambo. Na ukichimba zaidi utaona jamaa anabeba mambo personal.
Hakukuwa na ulazima wa Mwenyekiti wa chama kutolea maelezo jambo hilo. Kwahiyo Mbowe ameonesha udhaifu wa hali ya juu wa kiuongozi. Mbowe anahitaji mshauri mwenye utashi na siyo Lema.

Mzee Annael si ulishaaga, kumbe na ww ni mbishi!! Au kitanda kimejaa kunguni? Nenda kalale, saa hii utaishia kuleta malumbano na uwezo wako wa kujenga hoja utapungua. Subiri kesho tuachie sisi ambao hakuna kulala. Hapa utazidiwa hoja maana umeshachoka. Set alarm hata uamke saa 12 asubuhi umelizie viporo vya huku jf kabla ya kwenda kazini.
 
Mzee Annael si ulishaaga, kumbe na ww ni mbishi!! Au kitanda kimejaa kunguni? Nenda kalale, saa hii utaishia kuleta malumbano na uwezo wako wa kujenga hoja utapungua. Subiri kesho tuachie sisi ambao hakuna kulala. Hapa utazidiwa hoja maana umeshachoka. Set alarm hata uamke saa 12 asubuhi umelizie viporo vya huku jf kabla ya kwenda kazini.
Asante ndugu yangu. Usiku mwema.
 
Upande gani unaosema?

Kumbuka pia two wrongs don't make a right

Kampumzike tu, umeanzisha hoja, umepewa ukweli wako ambao ulikuwa hujafanya utafiti kabla ya kuanzisha mada, saa hizi umebaki kuleta misemo ya kiingereza tu humu ndani. Huwezi kuichafua cdm kwa vipost vyepesi vya kiwango hiki.
 
Back
Top Bottom