Yanayojiri bungeni: Tarehe 20 Machi, 2014

Yanayojiri bungeni: Tarehe 20 Machi, 2014

Makangarawe

Senior Member
Joined
Nov 19, 2013
Posts
101
Reaction score
24
Bunge maalum la Katiba leo limepata mgeni kutoka Kenya mh. Amos Wako ambaye alikuwa mwanasheria wa Kenya na alishiriki katika mchakato wa kuandaa katiba.

Lengo la ujio wake ni kutoa fursa kwa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kujifunza jambo alilolifanya akiwa Mwanasheria wa Kenya aliyeshiriki Mchakato wa Kupata Rasimu ya Katiba ya Nchi hiyo hadi kupatikana kwa Katiba yake.

=== Updates ====

Kikwazo cha lugha aliyotumia Mh. Amos Wako

Wanajamvi.

Nimefanikiwa kushuhudia asilimia kubwa ya Wabunge wa Bunge la Katiba wakilalamika kuhusu matumizi ya lugha ya kiingereza kwenye uwasilishaji wa Mh. Amos Wacko.

Baada ya kuona ombi lao halikubaliwi kwa kigezo cha kuleta mtiririko mzuri wa kile anachokitoa Mh. Amos Wacko.
Wabunge wameingia mitini kiaina kwa kusinzia ama kutokujitokeza kupeleka majina ya kuomba kuuliza swali. Hadi muda huu ni wabunge kumi tu kati ya mia sita ndo wameomba kuuliza maswali au kuchangia.

Pia kimetolewa kisingizio cha kwa kuwa mjadala unaangaliwa na kusikilizwa na wananchi kupitia vyombo vya habari inabidi tafasiri itumike ili watu wengi waelewe.

Swali langu ni: Mbona kila siku muda wa saa mbili asubuhi TBC1 kituo cha Taifa kinaungana na CCTV na wanatangaza kwa kiingereza? Au matangazo hayo hayatuhusu wabongo?
Pia: Kwani wajumbe walikuwa hawajui kama Mh. Amos Wacko atakuja kushusha nondo kwa lugha ambayo siyo yao?

Mwenye uelewa anisaidie.

===
Nimefurahi kusikia kwamba kutoka kwa Mwanasheria Mstaafu wa Kenya, Amos Wakko kwamba Kenya nafasi nyingi mfano: Katibu Mkuu, Mwanasheria Mkuu, Jaji Mkuu, Wakuu wa Taasisi zote za Umma, wanaomba ajira kama wafanyakazi wengine wowote wale. Na Interview kwa nafasi muhimu mfano Jaji Mkuu hufanywa kwenye TV Live. Hii ni jambo muhimu sana, tunahitaji kuwa nalo maana rushwa na wizi wa rasilimali utapungua katika Ofisi za Umma. Kila mtu yuko huru kufanya kazi kwa utaalamu bila kuogopa aliyemteua...

====
Rev. Mtikila naye anena,
WanaJF,

Katika hali ya kushangaza bungeni, mch Mtikila ametokea kukurupuka na kuingizia mambo ambayo hayahusiki katika mjadala unao endelea bungeni kwa sasa ambao ni kuhusu semina ya uzoefu wa nchi ya Kenya katika kuandaa katiba yao.

Mchungaji Mtikila bila ya aibu ametokea kuingizia mijadala mingine kabisa ambayo haina mahusiano ya kile ambacho kinajadiliwa bungeni na kupelekea kutokea kwa hali ya taharuki miongoni mwa wajumbe wa bunge maalumu. Jambo ambalo limemdhalilisha sana Mtikila.

Kubwa ambalo Mtikila alikuwa anang'ang'ania ni kupigania Tanganyika bungeni eti akidai kuwa kuna vitisho kutoka kwa mhe Sitta vya kuwashughulikia wale watakao ipigania Tanganyika kama ambavyo Dr Ulimboka, Dr Mvungi na Kibanda walivyo shughulikiwa. Jambo ambalo limepingwa vikali na Mhe Sitta kwa kumwambia yeye kama Mwenyekiti atatumia kanuni za bunge na sio vinginevyo katika kushughulikia hoja.

My take,

Mhe rais Kikwete amefanya makosa sana kuteua watu ambao vichwani mwao haijulikani kama ni wazima ama lah.

Hivi huyu Mtikila anashindwa kuelewa kuwa kuna mjadala wa semina na pia kuna mgeni!? Tanganyika nani anaitaka? Kama sio yeye na CHADEMA tu?
 
^^
Anasema "You cannot need a new constitution, if you don't have a constitution crisis"
^^
 
Wakati bwana Okao kutoka Kenya akiendelea kuelezea uzoefu wake kuhusu katiba ya Kenya na kutaka watanzania wajifunze kupitia Kenya, mtaalam huyu amekuwa akitoa maelezo hayo kwa njia ya kimombo na baadae kutafsiriwa, baadhi ya wajumbe wamemuomba M/Kiti ili mtaalamu huyo endelee tu kwa lugha ya kimombo kwa vile wengi wanafahamu. wakati Mwenyekiti akihoji kuwa endelee kwa lugha ya kimombo Mh Seif Ali Iddi amepeleka kichwa chake kushoto na kulia akiungana na baadhi ya wajumbe kutaka iendelee kutafsiriwa.,
 
Fafanua basi mkuu na uandike habari iliyojitosheleza.
 
hii kitu wamechemsha sana huyu Amos wenu anaongea kingereza tupu.eti amesema kiswahili kwao ni kigumu. sasa wamekuja na mkalimani hapa akiongea paragraph mbili anastop mkalimani anaelezea. baadae sita akaona ni kupoteza muda akamwambia aongee tu moja kwa moja kwani watanzania wengi wanajua kingereza. baada ya kuongea muda mrefu Sita anamkatisha tena anasema amepata msg kutoka kwa watu wengi eti lazima mkalimani atafsiri,lakini kwa sasa anatakiwa kutafsiri eneo kubwa yaani Wako aongee muda mrefuhalafu ndio atafsiri
 
katika kumchagua huyu msemaji kutoka Kenya kutokujua tu kiswahili ilikuwa inam-disqualify.
 
Sasa mbona hawakumwambia atumie kiswahili wakakurupuka na kiingereza lol, tz tunakurupuka jamani
 
Swala la shule za kina Kayumba/kata inabidi ubora wake usiisitizwe kwenye hii katiba. La sivyo hata wakalimani tutashindwa kuwazalisha.
 
Kwani lugha yetu ya taifa ni Kifaransa au Kiingereza?
Wajumbe wengi wa CCM ndio mbumbumbu, wanatuaibisha, Afadhali wamwachie Amos wako ashushe material moja kwa moja watatafasiri baadaye. Hawa wanatuaibisha sana maana Elimu imeshushwa na utawala wa CCM sasa wanamptotezea muda Mh. Wako na mpangilo wa mawazo yake. Utasikia magazeti ya Kenya watakavyotuchamba.
 
Yaani bunge letu lingekuwa linaendeshwa kwa Kiingereza kama Kenya ,mijadala ingekuwa inachukua muda mfupi sana,mambo ya ''Muongozo wa spika n.k ''yangepungua ama kuisha kabisa,wachangiajia wangekuwa wachache sana na utoro Bungeni ungeongezeka.
 
Sasa mbona hawakumwambia atumie kiswahili wakakurupuka na kiingereza lol, tz tunakurupuka jamani


Tumia akili ya kawaida tu! Kupitia almashauri ya kichwa chako, hakuna aliye kurupuka mgeni hakuweza kutumia lugha yetu kutoa mtililiko sahihi wa mawazo yake, hivyo utaratibu unaotumika ni sahihi
 
Kwani wakenya walijifunza kwa nani? Mi naona ilikuwa bora asiitwe huyo jamaa badala yake tungeangalia tu kwa uhalisia mahitaji na maoni ya watz yanataka nn na kuyafanyia kazi. Usije kushangaa huyo jamaa kulipa si chini ya tsh. 50,000,000 kwa hayo madudu tu
 
Back
Top Bottom