Yanayojiri Bungeni Dodoma: Jumanne, Trh 22 Aprili 2014 - Majadiliano ya bunge zima kwa sura ya 1 & 6

Hawa wabunge wanaosema wanaunga mkono maoni ya walio wengi ya serikali2, ni yepi hayo! Ni yale yaliyotolewa na wananchi kupitia Tume ya Mzee Warioba au ya Kamati zao ambayo kwa idadi hayalingani na yale yaliyotolewa na wananchi elfu 17!
 
Bunge maalumu la katiba (BMK) limejifia rasmi wiki hii baada ya kuanza kujadili rasimu mpya ya katiba badala ya rasimu mbili za kwanza kufeli.
Rasimu ya kwanza ilikuwa ni ile iliyoletwa na tume ya Jaji Warioba; ya pili ni ile iliyoletwa na JK na ya tatu ni ya samweli Sitta ambayo sasa wanajadili maisha, makabila, miradi na dini za watu wote wanaoongoza UKAWA. Ukimtukana memba wa UKAWA wewe una akili.. utashangiliwa saana... gusa kabila lake; dini yake n.k.

BUNGE ni tupu hata wale mashabiki wa serikali mbili wamekimbia aibu ya kujadili watu na maisha yao.. Katiba hii ya tatu imejaa vitisho vya vita vya kidini na kikabila; mapinduzi ya serikali; vurugu za kisiasa n.k.

HOJA ZILIZOPO:

Paul Makonda: Jusa na Lipumba ni mashetani kwa mujibu wa biblia;
Sheik Kombo: Hata koran inakubali Wapinzani ni mashetani na tena wasirudi tena bungeni.
Mch. Rwakatare: Washindwe kwa jina la Yesu
 
Nilikuwa namuona tu mtuta kumbe naye anauwezo wa kujenga hoja nimezipenda sana hoja zake yuko vizuri kujenga hoja zake na kuzielewa ameendelea kusisitiza kuwa katiba inatungwa bungeni siyo mitaani huku akiwataka chadema,cuf, na nccr mageuzi warudi bungeni make katiba haitungwi mitaani.
Anataka warudi ili baadae aseme walikuepo wakati interahamwe wakijipanga kwa mauaji?
 
Nami nakuunga mkono Tetyy ni bora hao wana CCM waliobaki mjengoni wakapitisha hivyo vifungu badala ya kupoteza muda kuwapiga vijembe UKAWA ambao hawapo huko bungeni. Ni upuuzi wa hali ya juu kumsema mtu asiyekuwepo bali tungetegemea wajenge hoja za kuridhisha ili kutetea mfumo wa Serikali 2. Hilo halifanyiki bali ni lugha zile zile zizilizo watoa UKAWA bungeni. CCM hawana hoja za maana ndio maana wanaishia kuongea ujinga mtupu matusi na kejeli kwa wapinzani. Ninawaasa wajue kuwa wakipitisha hivyo vifungu na hio Katiba ya Serikali 2 ni yao wao CCM lakini sisi Watanzania tulio wengi tunasubiri katiba yetu ya Serikali 3 kama ilivyopendekezwa na Tume ya Jaji Warioba. CCM wajue kuwa mabadiliko hayazuiliki ila yanacheleweshwa tu. Wanapigania masilahi yao kwa nguvu zote hata ikiwezekana kwa kuua (ndio maana wanachukia kuitwa Intarahamwe) wala si masilahi ya nchi na kwa ujinga wao huo wajue kila mtu amewajua na hivyo wajiandae kwa mabadiliko na wengine yatawapeleka jela kwa uchafu wao huo.


Siyo CCM pekee,nimeona nchi nyingi za Afrika zinapinga sana mabadiliko,mpaka inapotokea vita vya wenyewe kwa wenyewe ndipo wanastuka.
 
Wanajamvi nini kimetokea mbona hali imwbadilika bunge.nilitegemea kushangilia na makofi vizidi bungeni kwa sababu wote wanafanana.sidhani kama kuna mpinzani wao.sasa mbona wanapiga makofi kwa woga! Au wamegundua kuwa walifanya Unafiki? Au yalikuwa makofi ya kuoneshana uwezo wa usemaji na uungwaji mkono?
Tatizo nini au nini kimewarudisha nyuma ktk kupiga makofi na kushangilia?
 
Tunapiga makofi kwny point....
Hatuwez kusupport hoja zczo na upya.
Kila mtu anaongea kitu kimoja sasa tutapiga makofi kwny hoja moja kila saa hee!! Nikujichosha.
 
akuna utumwa hatari duniani kama utumwa wa kichumi umlazimisha mtumwa kutokumpinga bepari na ukiongezea utumwa wa kifikra hivyo watumishi ndani ya serekali awawezi kuupinga mtazamo wa rais na serekali yake atafukuzwa kazi na kukosa kula
 
Jamani bunge la Interahamwe vipi?hakuna updates,naona Mwanri ananyesha mvua tu hapa,kuna mama mzenji kaleta mambo ya ndoa ya mwanae hapa.hana hoja
 
Yupo live anazungumza kuwa watu wasipotoshe ukweli ya kwamba MAANA ya RASIMU ni mapendekezo na Mapendekezo yanaweza kukubaliwa au kukataliwa. Anasisitiza kuwa sheria inaruhusu kubadili lile linaloonekana sio zuri na kuwa wasishangae kuona wajumbe wa KATIBA wakiamua kuondoa baadhi ya vifungu. Anataja idadi ya watu waliochangia maoni kwa tume kuwa WARIOBA alitoa takwimu ambazo ni tofauti na hotuba aliyoitoa Bungeni.

Amtaka Warioba azibe mdomo kuwa anapoendelea kusemasema kwenye vyombo vya habari kuwa serikali tatu haziepukiki ni ajabu wakati tume halkkuwa yeye peke yake wenzake wako kimya lakini yeye kila siku kwenye vyombo vya habari tutakuwa na wasiwasi naye kuwa ni maoni yake sio ya wananchi. Anasema GHASIA HAWA. Ametaja idadi ya watanzania akataja waliochangia maoni kwa tume akasema Warioba alidanganya kuwa WENGI walipendekeza serikali TATU.

Asema kuongeza serikali ya tatu sio njia ya kuondoa changamoto zilizopo ila ni kuongeza nafasi za madaraka ambao ni vyeo wanavyovitaka wanaotaka serikali tatu. Anaongeza kusema wajumbe wa kundi la wachache walihusika na taarifa za kashfa, matusi na kejeli kibao ndio maana walikataa kusoma maoni yao kutoka kamati aliyokuwamo. Asema walio wachache waliwatukana hata marehemu. Mwisho anasema, mwanaume hakimbii vita ukawa warudi bungeni hiyo ni aibu hata wanawake hawakimbi vita warudi bungeni tubanane. Kamaliza.
 
Mie nashangaa wanajisifu kwa heshima na kuwalaumu wengine kwa kuwakashifu viongozi wetu.....Hivi wenyewe kwa kumkashifu na kumdhihaki Warioba wanaona wako sawa? Kumdhihaki Warioba ni Kumdhihaki Nyerere....tunaojua tunajua!
 
Hivi na ile miwani aliyovaa sijamuelewa? Je mule ukumbini kuna high light intensity?.
 
Tena kasema a msisitizo, mh.Lissu inaelekea hajaenda jandoni, na kama alibahatika kwenda then inabidi arudishwe tena. Maana alimtaja marehemu kwa mabaya. Kumbe Bunge letu licha ya kuongozwa na KANUNI, pia linaongozwa kwa mila na desturi za baadhi ya makabila.
 
Huyu bibi anakula lwa mwisho mwisho akiingia rais Lowasa anae subiri kuapishwa hata mchukua
 
katiba inaandaliwa na watawaliwa kuwaelekeza watawala n kwa namna gan wanatakiwa kutawala, hoja ya ghasia haina mashiko. na haiwezekani watawala waamue n namna gan wanataka watutawale haiwezekan
 
Mie nashangaa wanajisifu
kwa heshima na kuwalaumu wengine kwa kuwakashifu viongozi wetu.....Hivi
wenyewe kwa kumkashifu na kumdhihaki Warioba wanaona wako sawa?
Kumdhihaki Warioba ni Kumdhihaki Nyerere....tunaojua tunajua!

Wrioba SIYO sawa na Nyerere kwani mwl hakuwahi kukataliwa popote na kwa nafasi yoyote,,,,kumbuka warioba hakukubarika/alikataliwa kwao mwaka 1995 Pale wasira alipo mpiga chini kwa udomo zege,,,,,so Warioba < Nyerere.
 
Back
Top Bottom