Yanayojiri Bungeni Dodoma: Jumanne, Trh 15 Aprili 2014 - Majadiliano ya bunge zima kwa sura ya 1 & 6

Hivi serikali ya Muungano inapata wapi hela sasa hivi na itaacha vipi kuendelea pata hela?
 
Ni mtazamo wangu tu!!
Siku zote huwa nawaza na kufikiri kwakina kuhusu muungano nakujiuliza maswali yafuatayo
1; Inawezekana kupata vitu viwili katika kimoja? I mean serikali mbili zenye mamlaka katika nchi 1!????
2; Inawezekanaje nchi mbili zikaungana alafu moja kati ya hzo zilizo ungana ikawa inamiliki national identities like bendera, wimbo wa taifa, na vinginevyo!??????
3; Ni sehem gani ya katiba ya muungano wa jamhuri ya TANZANIA inawaruhusu Zanzibar kua na katiba yao ya nchi?????
Hivyo basi kwa KWA MTAZAMO WANGU NAONA MUNGANO UNGEKUA MUUNGANO WA KWELI KAMA TUNGEKUA NA SERIKALI 1 , MUUNGANO UNGEKUA MUUNGANO KAMA INGEKUEPO MSINGI MMOJA WA UTAWALA UNAOENDESHWA NA KATIBA MOJA YA NCHI "
naomba kuwasilisha hoja yangu wakuu pia karibu kwa mawazo mengine/ yatofauti na mtazamo wangu
 
Huu urais wa Muungano ni kiiini macho. Rais wa nchi ni lazima awe Rais mahali popote na kwa mambo yote
 
Watanzania ktk suala la Uchumi tuko nyuma GDP yetu ni ndogo sana ukilinganisha na Mauritius, Libya,Israel Nchi hizo zinaongozwa na Rais 1 na Waziri Mkuu hatuna ubavu wa kuendesha Serikali 3 kama tutaruhusu ziwepo ujue tutatumia pesa ambayo tungeweza kuwapa wachimba madini mtaji au mama ntilie,pembejeo za kilimo ,mkopo kwa wanavyuo wetu serikali 3 ni mzigo kwetu wananchi.
 
Watanzania ktk suala la Uchumi tuko nyuma GDP yetu ni ndogo sana ukilinganisha na Mauritius, Libya,Israel Nchi hizo zinaongozwa na Rais 1 na Waziri Mkuu hatuna ubavu wa kuendesha Serikali 3 kama tutaruhusu ziwepo ujue tutatumia pesa ambayo tungeweza kuwapa wachimba madini mtaji au mama ntilie,pembejeo za kilimo ,mkopo kwa wanavyuo wetu serikali 3 ni mzigo kwetu wananchi.

usipotoshe. serikali kuu itakuwa ndogo sana kwa hiyo hakuna litakalobadilika.rasimu inaonesha serikali 3 garama zitapungua. na kama utanganyika ni mbaya mbona uzanzibar hamsem ni ubaya una garama?kuweni makini
 
Tanganyika lazima irudi na uchapa kazi wa serikali kama ilivyokuwa hapo mwanzo.Tanganyika haikuwahi kuwa na viongozi wasiotekeleza wajibu wao ipasavyo kama wa Tanzania.
Hivi kwa mfano ukiacha kuongelea usimamizi wa rasimali usivyoridhisha,unajua mpango wa kupata vazi la taifa umeishia wapi??Au kama umesahau kuhusu vazi la taifa,je vitambulisho vya taifa??
Kama vitu vidogo kama hivi vinaishinda Tanzania si bora ipunguziwe kazi na Tanganyika ili ibaki na kazi chache yenye kuzimudu?
 
Watanzania ktk suala la Uchumi tuko nyuma GDP yetu ni ndogo sana ukilinganisha na Mauritius, Libya,Israel Nchi hizo zinaongozwa na Rais 1 na Waziri Mkuu hatuna ubavu wa kuendesha Serikali 3 kama tutaruhusu ziwepo ujue tutatumia pesa ambayo tungeweza kuwapa wachimba madini mtaji au mama ntilie,pembejeo za kilimo ,mkopo kwa wanavyuo wetu serikali 3 ni mzigo kwetu wananchi.
Kwani CCM hela yote waliyoiba inaweza endesha serikali ngapi?
 
Katika majadiliano yanayoendelea inaonekana wazi kwamba wazanzibar sasa wanaamsha hisia za utengano zilizokuwepo zamani. Weusi wamekuwa wanawatukana na kuwabagua wenye asili ya kiarabu kaisi kwamba unashindwa kuelewa muafaka kule zanzibar utabaki kweli baadaya katiba hii? Nimependa mbunge mmoja amemuonya kingwangala aliyesema kwamba katiba hii ikipitishwa itawalazimu zanzibar kubadili katiba yao na kumwambia hizo ni ndoto za mchana na halitokaa litokee zanzibar. Huu ubaguzi wa rangi ambao Sitta amekuwa anaulea bila kuukemea haliwezi kuleta ufa mkubwa zanzibar?


Hata tukipitisha serikali tatu katiba ya Zanzibar razima ifumuliwe tena, katiba inayotungwa dodoma ndio katiba mama. Huwezi kutunga katiba mama kwa kuogopa kabadili katiba ya Zanzibar, kwenye rasimu ya Katiba aridhi imekua ya shiliklisho wakati katiba ya Zanzibar haisemi hivyo inamaana aridhi ya tanganyika tu ndo itakayokua ya shilikisho?
 
Mbarouk mzima kweli eti anasema mfumo wa serikali mbili utainufaisha Zanzibar itakuwa half london my God! Kwa miaka 50 hamjakuwa half london kwa mfumo huu sasa ndo utawanufaisha? And this and the Rages r the one to decide our fate. R.I.P TANZANIA

Wewe unacheza na njaa?
 
Sasa serikali mbili utasemaje hakuna upande ambao haujaweka mamlaka yote kwenye serikali ya muungano? Tanganyika mamlaka yao yanakaa wapi?


Mkuu hata hiki kitendo cha kukaa kujadili muundo wa muungano wakati upande mmoja tayari ushakua na katiba ni aina fulani ya wizi. Kuna vitu vingi ambavyo hata Tanganyika ikija leo tutashindwa kuviweka kwenye katiba yetu kwa kubanwa na katiba ya jamhuri wakati wenzetu walipokua wanatunga katiba yao walikua huru. Kwa sasa hivi katiba ya Zanzibar inawaongelea wazanzibari, katiba ya Tanganyika haipo inamaana Tanganyika haiwakilishwi humo ndani chochote kitakachopatikana humo ndani huko mbele ya safari kitakua haramu.
 
kuna mbunge mmoja wa znz kaniacha hoi kweli eti yeye anaunga mkono serikali mbili eti anasema serikali tatu zitavunja muungano na mimi nina kaya zangu mbili tatu lushoto nitamuachia nani. Yaani yevaangalia lake si la wananchi.ndivyo wajumbe wa ccm wote walivyo. Hawana hoja ya msingi ya kupinga serikali tatu
 
Hivi Dodoma kuna baridi kali sana? namuona Mwigulu amejitanda ile mitandio inayovaliwa nchi zenye baridi kali hasa na mashabiki wa mpira.

Mshamba tuu yule,ila kwa fikra zake anadhani yeye mjuaji.


Sent from my iPad using JamiiForums
 
Ni dhahiri hakuna uwezekano wa kuwa na katiba mpya kutokana na msimamo wa wajumbe wa chama Tawala. HAKUNA MJUMBE ALIYETAYARI KUSHAWISHIKA KWA HOJA YEYOTE KUTOKA UPANDE ASIOUSHABIKIA HATA INGEKUWA BORA NAMNA GANI. Tegemeo la wajumbe kubadili mIsimamo kutokana na ubora wa hoja za mwenye mawazo tofauti halipo kamwe. kukijaribu kulazimisha maamuzi yeyote bila marithiano hatutapata katiba bora. Aidha nakubali kuwa hatua tuliyofikia sasa ya bunge la katiba kujadili rasimu ya katiba iliyowasilishwa na Jaji Joseph Warioba ni nzuri. Sasa Rasimu ipo bado kuijadili tu kwa maana ya kuifanyia marekebisho.

Mawazo yangu yananituma kusitisha kazi ya kujadili katiba kwa sasa, na tuende kushughulika na Tume ya uchaguzi pamoja na kuboresha daftari la wapiga kura. Hii nikwasababu yawezekana kukatakiwa kura ya maoni kuhusu muundo wa muungano kabla ya kupigia kura ya maoni ya katiba mpya. Vilevile yawezekana mjadala wa bunge la katiba ukaendelea mpaka baada ya uchaguzi mkuu wa 2015.

Yatupasa kukataa kuendelea na mfumo wa uendeshaji wa uchaguzi uliopo sasa. athari zake tumeziona katika bunge linaloendelea sasa. Tunahitaji tume huru ya uchaguzi na kila raia mwenye sifa ya kupiga kura atumie haki yake ya kupiga kura, hapo ndipo katiba tuitakayo itaweza kupatikana.

Tukikubali kuendeleza marumbano ya mipasho yaliyopo sasa na hatimaye wanaojiita wengi wakafanikiwa kupenyeza serikali zao mbili, hatutokaa tusahau fursa hii maana mabadiliko yeyote yanayofuata yatakuwa na shinikizo kubwa sana ambalo huenda likasababisha muundo mbovu wa muungano na katiba mbovu au hata kuvunja muungano.

Kutokana na mjadala unaoendelea bungeni, nimejifunza kwamba Zanzibar hakuko salama, na waliopendekeza serikali nne huenda wanahoja kwa mazingira yalivyo zanzibar. Wazanzibar hawaaminiani kabisaaaaaa! hivyo huenda serikali ya Pemba, Serikali ya Unguja, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Muungano vikawa ndio suluhisho la migogoro tunayoiona.

Wananchi tuelekeze nguvu zetu katika kuhakikisha tunakuwa na tume huru ya uchaguzi na daftari la wapiga kura linaboreshwa haraka. Tujipange kwa lolote linaloweza kutokea.

Lakini pia nawashauri Ukawa wakati wa kuchangia hoja jiandaeni kwa takwimu na vielelezo:
Mfano: Naunga hoja muundo wa serikali iliyopendekezwa ktk rasimu ya katiba sababu:
1. kuondoa kero : orodhesha kero na njiaambazo serikali mbili zilijaribu kuzitatua na zilishindwa kivipi.
onyesha jinsi serikali tatu itakavyoziondoa
Gharama za uendeshaji wa serikali tatu: orodhesha namba ya wizara zote za sasa, onyesha wizara zitakazo baki ktk serikali ya muungano baada ya kuingia katika serikali tatu, onyesha wizara unodhanina zinafaa kusimamiwa na serikali washirika, hapo sasa onyesha tofauti ya gharama kama utavyoweza kujenga hoja. Onyesha jinsi bunge la muungano litakavyo kuwa dogo na laweza kutumia ukumbi wa karimjee DSM, onyesha jinsi bunge la Tanganyika litavyo kuwa na litakuwa likiendeshwa wapi shughuli zake wapi, bila shaka ni Dodoma Onyesha Kiongozi wa Tanganyika atakapoendeshea shughuli zake kuwa ni ofisi ya sasa ya Waziri mkuu Dodoma. Onyesha Kuwa ofisi ya Raisi wa Muungano iendelee kuwa pale Magogoni, hivyo hoja kuwa hakuna ardhi ya ofisi ya rais wa muungano haipo. Zungumzia suala la Urai mmoja kwa wananchi wote washirika kwamba wote ni raia wa Jamuhuri za Tanganyika na Zanzibar. Onyesha wepesi utakaokuwepo kwa nchi washirika kuhudumia wananchi wake na jinsi serikali ya muungano itakavyowajibika kwa nchi washirika.

Ndugu zangu pambana, hakuna kulala, jini la Katiba limeishachomoka katika chupa, halitarudi mpaka katiba mpya ipatikane.
 
Wenyeji waliokandamizwa walihisi hawawezi kustahamili zaidi dhiki na udhalimu waliogubikwa nao na wakaamua kutafuta kujikomboa. Kulifikia lengo hili waliupeleka ujumbe wa siri Oman. Walipofika walitoa malalamiko yao kwa Imam juu ya unyama na udhalimu wa Kireno, na mabaya yote yaliyofanywa dhidi yao. Zaidi ya wananchi mia mbili walikatwa vichwa au kuuliwa kwa panga kwa jina la Mungu. Wareno waliwaingiliya kwenye nyumba zao, na kuwafukuza wenyewe na kuwanajisi wanawake wao. Wale waliokwenda kuomba msaada kabla walihukumiwa kifo.6
Oman ilikuwa ni dola ya kwanza ya Mashariki kuishinda dola kubwa ya kibeberu kutoka Magharibi. Ilifanikiwa kuwaondowa Wareno kutoka Mutrah baada ya Sultan bin Saif Al-Ya’rubi (1649–1668) kupewa taarifa muhimu na Muhindi aliyekuwa na Wareno lakini akiiunga mkono kadhia ya Waomani na “Baada ya Wareno kufukuzwa kutoka fukwe za Oman…walilipiza kisasi kwa kuwaadhibu Waswahili na Waarabu wa Kiomani wa Mombasa na sehemu nyengine za Afrika Mashariki kwa ukali mkubwa zaidi.”7
Dola ya Zanzibar ilikuwa imetanda Afrika Mashariki na Kati kabla ya kuingiya wakoloni wa Kizungu ambao walianza kunyanganyiana mpaka mwisho wake vikabakiya visiwa vya Unguja na Pemba. Pamoja na kuwa ilipofikiya Agosti 1961 iliamuliwa kuwa tarehe ya uhuru wa Zanzibar “isingeliwezekana kuwa kabla sana au baada sana ya [uhuru] wa Kenya na sababu kubwa ya hili ni mara Kenya itakapopata uhuru, uwezo wa ufalme wa Kiingereza wa kuilinda Zanzibar kwa nguvu za kijeshi utapunguwa kwa kiasi kikubwa sana.”8
Dhihaka ya kihistoria ni Zanzibar pamoja na historia ya Waarabu wa Kiomani waliyopigana na kuwashinda wakoloni wa Kireno kupotoshwa kutoka mtazamo wa kiukombozi na kuangaliwa kipropaganda kuwa ilikuwa ni kiti cha mwanzo
34 Mlango wa Tatu
cha ubeberu Afrika Mashariki. Nyerere alikuwa ameshatiya niya ya kuindowa Dola ya Zanzibar kwa kukitumiya kisingiziyo cha ubeberu na aliiyona fursa ya kuweza kufanya hivyo baada ya Tanganyika kupata uhuru na kwa kukosekana kwa uwezo wa Kiingereza wa kuilinda Zanzibar kwa nguvu za kijeshi kutoka Kenya. Na serikali ya ZNP-ZPPP ilimpa Nyerere fursa aliyokuwa akiisubiri ilipotaradadi baina ya kuipeleka Zanzibar kwenye njia ya siasa kali ya kizalendo ya Kiarabu ya Raisi Gamal Abdel Nasser, na kuwaomba Waingereza wabaki kuisaidiya Zanzibar kiulinzi baada ya uhuru wa Zanzibar wa tarehe 10 Disemba 1963. Matokeo yake ulinzi wa dola na uhuru wa Zanzibar ukapoteya.9
Tarehe 21 Novemba 1963, Balozi wa Kiingereza wa Zanzibar, Sir George Mooring alipeleka barua kwa Secretary of State for the Colonies yenye kusema:
Waziri Mkuu amenijiya na ombi la kutaka kutimiza Mkataba wa Kijeshi baina ya Zanzibar na Serikali ya Malkiya (H.M.G.). Serikali ya Zanzibar makhsusi inaomba kuwa Serikali ya Malkiya iombwe ikubali kutowa nguvu kwa ajili ya usalama wa ndani na wanataka kujuwa kama vikosi vya Kiingereza vitaweza kupatikana vyenye nguvu za kijeshi. Makadiriyo ya Serikali ya Zanzibar ni kuwa kutakuwa na tishio la usalama wakati na mara tu baada ya Siku ya Uhuru. Nitashukuru kama nitaelekezwa nitowe majibu gani, na kama Gavana wa Kenya ambaye namnukuu ujumbe huu atashauri kama Serikali ya Kenya itakuwa na upinzani wowote wa kuvitumiya vikosi vya Kiingereza viliyoko Kenya kwa ajili ya kuweka usalama Zanzibar ikiwa itahitajikana.10
Ujumbe wa hapo juu wa Sir George Mooring ulipelekwa kwa Secretary of State for the Colonies tarehe 21 Novemba 1963 saa kumi na mbili na nusu za magharibi. Siku hiyohiyo na wakati huohuo Sir George Mooring alimpelekeya Secretary of the Colonies ujumbe mwengine ambao uliongezewa hadhi ya kuwa ni siri na wa binafsi (secret and personal):
 
kubadilisha mawazo yake juu ya Zanzibar na waliendeleya kutizama maslahi yao na kumuunga mkono Mwalimu Nyerere katika jitihada zake mpya za kuimeza Zanzibar. Kisingiziyo kipya kilikuwa ni Ukoministi hata kama alifahamu kuwa Makomred walikuwa ni "kikundi cha watu wachache [Waarabu?] na kibanzi cha wachache."24
Kwenye mahojiano mbele ya televisheni aliyofanyiwa marehemu Mzee Karume, John Okello, na Abdulrahman Babu, na mwandishi wa habari wa Kiingereza, Babu alitamka wazi kuwa yeye na kikundi chake hawakusaidiwa na nchi za Kikoministi katika kufanikisha Mapinduzi na kuwa Balozi wa Cuba aliyekuwepo Dar es Salaam alikuwa hajui kitu kuhusu Mapinduzi kama alivyokuwa yeye hakujuwa chochote kuhusu mipango ya Mapinduzi ya Zanzibar. Okello alisema kuwa alisaidiwa na "Mungu wa Waafrika" kuyafanikisha Mapinduzi hayo Zanzibar na Babu aliyarudia kikasuku maneno ya Okello kwa kusema "tulisaidiwa na Mungu wa Waafrika."
Mara tu baada ya kutokea Mapinduzi ya Zanzibar, "Jorge Serguera Balozi wa Cuba nchini Algeria aliruka kwa ndege kwenda Zanzibar kuitathmini hali ilivyokuwa. Baada ya siku chache aliruka akenda Moscow kuonana na Fidel Castro ambaye alikuwa anautembelea Muungano wa Kisovieti kuanzia Januari 13 mpaka 23. Castro alifadhaishwa kabisa na habari za Mapinduzi [ya Zanzibar]. ‘Fidel aliniuliza,' anakumbuka Serguera, ‘Ni kweli [viongozi wa Mapinduzi Zanzibar] wanazungumza Kispaniola?' Nikasema: ‘Ni kweli Fidel.' Halafu akauliza: ‘Ni kweli wanasema "Patria o muerte. Venceremos!" ' Nikasema: ‘ni kweli Fidel.' Halafu akauliza: ‘Ni kweli tuliwapa mafunzo [ya kijeshi]?' Nikasema: ‘Ni kweli, Fidel.' Akasema: ‘Nilifikiri ni propaganda ya Kimarekani!' "25
Ingawa Babu na Makomred walikuwa na mipango yao ambayo ikiongozwa na fikra za kisoshalisti na zaidi za Mao Tse-Tung, isingeliwezekana kuungwa mkono na Cuba kwa wakati ule kufanya mapinduzi Zanzibar wakati Cuba ilikuwa na uhusiano mzuri na Urusi na ilikuwa haisikilizani na Uchina. Pia, ilikuwa ni kwa faida ya wahusika khasa wa Mapinduzi ya Zanzibar kuwatupiya mpira Makomred au Kamati ya Watu 14 kwa sababu kwa kufanya hivyo walikuwa wanajipa himaya ya bure.
Waliokuwa hawakijuwi kiini cha Mapinduzi wakipita wakitamba kuwa wao ndio wao wanamapinduzi wenyewe! Na ndio maana mpaka hii leo hakuna maelezo kutoka kwa Komred yoyote aliye hai au aliyekufa yenye kuthibitisha mchango wao kabla ya Jumapili tarehe 12 Januari 1964. Walikubali kuyatumiya na kutumiliwa na Mapinduzi kama walivyokubali wengineo katika chama cha Afro-Shirazi wakati Babu alitambuwa kuwa:
Waingereza waliiendeleza hii sera ya kuigawa Afrika Mashariki na Kati kutoka Afrika ya Kaskazini kwa nguvu ambazo hazijapata kuonekana. Walifikia kupandikiza chuki za migongano ya kikabila baina ya "Waarabu" na "Waafrika"
 
Ni dhahiri hakuna uwezekano wa kuwa na katiba mpya kutokana na msimamo wa wajumbe wa chama Tawala. HAKUNA MJUMBE ALIYETAYARI KUSHAWISHIKA KWA HOJA YEYOTE KUTOKA UPANDE ASIOUSHABIKIA HATA INGEKUWA BORA NAMNA GANI. Tegemeo la wajumbe kubadili mIsimamo kutokana na ubora wa hoja za mwenye mawazo tofauti halipo kamwe. kukijaribu kulazimisha maamuzi yeyote bila marithiano hatutapata katiba bora. Aidha nakubali kuwa hatua tuliyofikia sasa ya bunge la katiba kujadili rasimu ya katiba iliyowasilishwa na Jaji Joseph Warioba ni nzuri. Sasa Rasimu ipo bado kuijadili tu kwa maana ya kuifanyia marekebisho.

Mawazo yangu yananituma kusitisha kazi ya kujadili katiba kwa sasa, na tuende kushughulika na Tume ya uchaguzi pamoja na kuboresha daftari la wapiga kura. Hii nikwasababu yawezekana kukatakiwa kura ya maoni kuhusu muundo wa muungano kabla ya kupigia kura ya maoni ya katiba mpya. Vilevile yawezekana mjadala wa bunge la katiba ukaendelea mpaka baada ya uchaguzi mkuu wa 2015.

Yatupasa kukataa kuendelea na mfumo wa uendeshaji wa uchaguzi uliopo sasa. athari zake tumeziona katika bunge linaloendelea sasa. Tunahitaji tume huru ya uchaguzi na kila raia mwenye sifa ya kupiga kura atumie haki yake ya kupiga kura, hapo ndipo katiba tuitakayo itaweza kupatikana.

Tukikubali kuendeleza marumbano ya mipasho yaliyopo sasa na hatimaye wanaojiita wengi wakafanikiwa kupenyeza serikali zao mbili, hatutokaa tusahau fursa hii maana mabadiliko yeyote yanayofuata yatakuwa na shinikizo kubwa sana ambalo huenda likasababisha muundo mbovu wa muungano na katiba mbovu au hata kuvunja muungano.

Kutokana na mjadala unaoendelea bungeni, nimejifunza kwamba Zanzibar hakuko salama, na waliopendekeza serikali nne huenda wanahoja kwa mazingira yalivyo zanzibar. Wazanzibar hawaaminiani kabisaaaaaa! hivyo huenda serikali ya Pemba, Serikali ya Unguja, Serikali ya Tanganyika na Serikali ya Muungano vikawa ndio suluhisho la migogoro tunayoiona.

Wananchi tuelekeze nguvu zetu katika kuhakikisha tunakuwa na tume huru ya uchaguzi na daftari la wapiga kura linaboreshwa haraka. Tujipange kwa lolote linaloweza kutokea.

Lakini pia nawashauri Ukawa wakati wa kuchangia hoja jiandaeni kwa takwimu na vielelezo:
Mfano: Naunga hoja muundo wa serikali iliyopendekezwa ktk rasimu ya katiba sababu:
1. kuondoa kero : orodhesha kero na njiaambazo serikali mbili zilijaribu kuzitatua na zilishindwa kivipi.
onyesha jinsi serikali tatu itakavyoziondoa
Gharama za uendeshaji wa serikali tatu: orodhesha namba ya wizara zote za sasa, onyesha wizara zitakazo baki ktk serikali ya muungano baada ya kuingia katika serikali tatu, onyesha wizara unodhanina zinafaa kusimamiwa na serikali washirika, hapo sasa onyesha tofauti ya gharama kama utavyoweza kujenga hoja. Onyesha jinsi bunge la muungano litakavyo kuwa dogo na laweza kutumia ukumbi wa karimjee DSM, onyesha jinsi bunge la Tanganyika litavyo kuwa na litakuwa likiendeshwa wapi shughuli zake wapi, bila shaka ni Dodoma Onyesha Kiongozi wa Tanganyika atakapoendeshea shughuli zake kuwa ni ofisi ya sasa ya Waziri mkuu Dodoma. Onyesha Kuwa ofisi ya Raisi wa Muungano iendelee kuwa pale Magogoni, hivyo hoja kuwa hakuna ardhi ya ofisi ya rais wa muungano haipo. Zungumzia suala la Urai mmoja kwa wananchi wote washirika kwamba wote ni raia wa Jamuhuri za Tanganyika na Zanzibar. Onyesha wepesi utakaokuwepo kwa nchi washirika kuhudumia wananchi wake na jinsi serikali ya muungano itakavyowajibika kwa nchi washirika.

Ndugu zangu pambana, hakuna kulala, jini la Katiba limeishachomoka katika chupa, halitarudi mpaka katiba mpya ipatikane.





Warudishe kwetu wanainchi tuamue


Na hapa tuko kama rasimu ya Mzee Warioba tu Tatu tatu tatu tu we need Tanganyika yetu sasa
 
usipotoshe. serikali kuu itakuwa ndogo sana kwa hiyo hakuna litakalobadilika.rasimu inaonesha serikali 3 garama zitapungua. na kama utanganyika ni mbaya mbona uzanzibar hamsem ni ubaya una garama?kuweni makini
Bunge la Muungano limefikia hatua ambayo ni ile ama lako au langu.naona tushauri jinsi ya kutoka hapo kwa kuanda katiba ya sote.Naona katiba iwe ya win win kwa kuweka vipengele vifuatavo;
1 Pawepo na nchi moja na serekali moja ya Muungano
2 Kila upande wa Muungano uwe na serekali ndani ya nchi moja kwa mambo ambayo si ya muungano
3Tunu za katiba ya muungano viheshimiwe ktk katiba za kila upande
4Upande waTanganyika na ule wa Zanzibar viwe na katiba ambazo hazipingani na Tunu/katiba ya muungano.kura za maoni zitawaandaa watu kwa lengo hili
5 TRA iwe ya Muungano na wawajibike kwa mfumo maalum kwa Rais wa Muungano na viongozi wa kila upande.Hii ni kuhakikisha viongozi wa TRA wanaheshimu sheria kwa hali ya juu.
5Sehemu ya VAT iende kwenye Muungano
 
Wajumbe wa bunge la katiba, haswa wenye mlengo wa serikali 3! mnapaswa kuwa makini wakati mnapojibu hoja za upande wa pili kwa kuwa ccm wanaingiza suala la ubaguzi katika mjadala ili baadae litumike kama turufu ya kuwaogopesha watu. TAFAKARINI.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom