Chillah
JF-Expert Member
- Oct 12, 2016
- 8,293
- 8,847
Kiungo nyota wa Atletico Madrid na timu ya taifa ya Hispania, Jorge Resurrección Merodio maarufu kama Koke, ameonyesha kushangazwa na Simba wa mbuga za wanyama za Ngorongoro.
Koke na baby wake, wako nchini Tanzania wakila raha.
Kiungo huyo anaonekana akiwa amepiga picha na Simba huyo ambaye amepumzika pembeni yake.
Koke ameongozana na mpenzi wake kwa ajili ya mapumziko na wako kwenye mbuga za wanyama za Manyara mkoani Manyara.
Kiungo hiyo aliyekuwa Urusi na Hispania kabla haijatolewa, ametembelea Ngorongoro na picha zinaonyesha akiwa ni mwenye furaha pamoja na mpenzi wake.