Nilifungua biashara ya chakula mbali kidogo na ninapo ishi. Miezi minne ya kwanza biashara ilikuwa ikienda vizuri, hivyo nikajiwekea mipango kadhaa ya kupanua biashara yangu.
Baada ya miezi kama sita hivi akaja mama mmoja kufungua biashara jirani na kwangu, yani frem ya pembeni yangu kabisa. Tukaanza kugawana wateja, hivyo biashara ikawa inasua sua si kama mwanzo.
Baada kama ya miezi miwili toka yule mama afike kila nikifika asubuhi nakuta friji imejizima; vyakula vimeharika, juisi na maziwa vimeharibika pia.
Ile friji nilinunua mpya kabisa, ilibidi nimuite fundi aikague lakini akasema ipo sawa. Cha ajabu, kuanzia asubuhi mpaka jioni tunapokuwepo tukiwasha friji haijizimi, nikasema tujaribu tusiwashe siku nzima kisha usiku tu ndio iwake lakini bado tukirudi friji imezima na vitu vimeharibika.
Kwa bahati mbaya si kil ulichopika watu watanunua na kitaisha, hivyo ilibidi nibadilishe friji lakini hali ikawa ile ile. Nikaweka jenereta lakini wapi
Kipindi hicho wateja sipati kabisa mpaka nikaamua kufunga ile biashara.
Wewe mama wa kimakonde ulichonifanya pale Kawe sokoni sitakusahau, SITAKUSAHAU MILELE.
Sent using
Jamii Forums mobile app