Nyamsusa JB
JF-Expert Member
- Jul 9, 2015
- 567
- 1,565
Uchaguzi huu unanikumbusha mbali sana,
Unanikumbusha hadithi moja nzuri sana ya Kobe na Ndege Mjanja.
Ilitokea siku moja ndege wenye mabawa walikua na sherehe (Kalamu), walikubaliana waluke mbali kwenye Mti moja mkubwa sana.
Sasa ndege huyu mjanja alimdanganya Kobe nae aende kwenye hiyo sherehe, lakini Kobe alihoji akasema nitaendaje wakati mimi sina Mabawa. Ndege huyo mjanja alimwambia Kobe usijari rafiki angu nitakutengenezea mabawa ya bandia. Siku ilipowadia kweli ndege huyu mjanja alimbandika Kobe mabawa ya bandia kwa gundi.
Baada ya Kobe kubandikwa mabawa ya bandia alifurahi sana na safari ikaanza, wakaungana na ndege wengine akaruka wakafurah na kuimba, wakati wanaendelea kuimba na kufurahia Jua nalo liliendelea kuchomoza na kuongeza makali, hii hali ilianza kumpa hofu Kobe huyo lakini hakujali sana na akaendelea kuruka juu zaidi, Jua nalo likaongeza makali na manyoya ya Kobe yakaanza kunyonyoka, wakati sherehe inaendelea kunoga ndivyo manyoya ya Kobe yalizidi kunyonyoka akaanza kulia ya wengine yananyonyoka, ya wengine yananyonyoka, ndege hao hawakujali waligundua kua Kobe hakua mwenzao hata yule ndege mjanja hukujali pia na mwisho wa siku Manyoya yaliisha na akaanza kuanguka chini kwa spidi ya ajabu akaangukia pua akafa.
Sasa tuangalie mfanano wa hadithi hii katika Uchaguzi wetu.
Magufuli ni kama Kobe kwenye hadithi yetu, sio mwanasisa mwenye kuaminiwa na CCM kupewa nafasi ya kugombea uraisi, imelazimishwa na amelazimishwa tu kama Kobe alivyolazimishwa kushiriki Sherehe ya ndege walukao sasa kadri muda unavyokwenda ndivyo Magufuli anaonekana tofauti na wenzake kama vile kobe alivyotofautiana na Ndege walukao, manyoya yakaisha Kobe akaanguka akafa na ndivyo itakavyokua kwa Magufuli.
Asanteni
Unanikumbusha hadithi moja nzuri sana ya Kobe na Ndege Mjanja.
Ilitokea siku moja ndege wenye mabawa walikua na sherehe (Kalamu), walikubaliana waluke mbali kwenye Mti moja mkubwa sana.
Sasa ndege huyu mjanja alimdanganya Kobe nae aende kwenye hiyo sherehe, lakini Kobe alihoji akasema nitaendaje wakati mimi sina Mabawa. Ndege huyo mjanja alimwambia Kobe usijari rafiki angu nitakutengenezea mabawa ya bandia. Siku ilipowadia kweli ndege huyu mjanja alimbandika Kobe mabawa ya bandia kwa gundi.
Baada ya Kobe kubandikwa mabawa ya bandia alifurahi sana na safari ikaanza, wakaungana na ndege wengine akaruka wakafurah na kuimba, wakati wanaendelea kuimba na kufurahia Jua nalo liliendelea kuchomoza na kuongeza makali, hii hali ilianza kumpa hofu Kobe huyo lakini hakujali sana na akaendelea kuruka juu zaidi, Jua nalo likaongeza makali na manyoya ya Kobe yakaanza kunyonyoka, wakati sherehe inaendelea kunoga ndivyo manyoya ya Kobe yalizidi kunyonyoka akaanza kulia ya wengine yananyonyoka, ya wengine yananyonyoka, ndege hao hawakujali waligundua kua Kobe hakua mwenzao hata yule ndege mjanja hukujali pia na mwisho wa siku Manyoya yaliisha na akaanza kuanguka chini kwa spidi ya ajabu akaangukia pua akafa.
Sasa tuangalie mfanano wa hadithi hii katika Uchaguzi wetu.
Magufuli ni kama Kobe kwenye hadithi yetu, sio mwanasisa mwenye kuaminiwa na CCM kupewa nafasi ya kugombea uraisi, imelazimishwa na amelazimishwa tu kama Kobe alivyolazimishwa kushiriki Sherehe ya ndege walukao sasa kadri muda unavyokwenda ndivyo Magufuli anaonekana tofauti na wenzake kama vile kobe alivyotofautiana na Ndege walukao, manyoya yakaisha Kobe akaanguka akafa na ndivyo itakavyokua kwa Magufuli.
Asanteni