mzee wa kasumba
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 1,440
- 2,963
Maishani kuna mengi ya kukumbukwa, ila kuna mengine ya kukumbukwa zaidi. Hii ni kutokana na uzito wake
Mke wa mtu sumu
Dada huyu alikuwa na duka jirani na ambapo nilikuwa naishi. SIkuwa na mazoea naye kabisa awali. Lakini kadiri siku zilivokwenda alianza kuleta mazoea kidogo kidogo.
Muda wote sikuwa najua kama dada yule alikuwa na mume, nami sikuuliza kwa sababu hakunivutia kumtongoza.
Mazoea yalizidi kiasi kwamba siku nikibadili njia hulalamika sana na kuwa huwa anamiss kuniona na lile tabasamu langu uchwara.
Watoto wa mtaa wataungana nami kwani wanajua, demu akishaanza kusema kuna muda huwa anakumiss basi moja kwa moja unaona hapa ushakubalika. Basi hata kama mwanamke hukua na mpango wa kumpelekea moto utatafuta njia yoyote ile. Basi nami nikaona hapa bila shaka nimeshaeleweka ngoja nianze kucheba cheba.
Siku hiyo nikamwambia "siter ee",
akaitika "bee"
Nikamwambia kuna kitu natamani sana kukwambia ila najikuta roho inasita, ila usijali siku moja ntakwambia tu wala usijali. Kama utapata muda (siku flani) nitafute nikwambie.
Akasema sasa ntakutafutaje wakati wee namba yako sina? Akasema nipe namba yako. Nikambwia namba tuu hiyo mamy. Akasogeza simu yake nikaandika nambari kisha nikapotea.
Kabla sijafika (kazini) ambako nilikuwa naelekea nikatangamana na ujumbe usemao Namba yangu hiyo MIMI MAMA.....
Nikamwambia ooh asante, kumbe umeolewa? Mh basi sawa.
Akasema mbona umeguna? Nikamwambia basi hata ambacho nilitaka kukwambia nimegairi maana nilijua hujaolewa.
Akasema Ongea tuu kaka, we mtu mzima bana.
Mpaka hapa nikahisi kama mdudu anataka kupasua zizi, maana alivimba ghafla. Nikasema eeebwana mchuchu amejileta mwenyewe. Hapa ni kumaliza tuu
Nikamwambia "bana sister samahani, mimi nakupenda. Afu nimekuelewa sana ujue, lakini nilikuwa naogopa kukwambia kwasababu sikutaka kuingilia mahusiano yako ila nafsi imenishinda nami ni mwanadamu. Kama nimekosea nisamehe bure mpendwa. Lakini mpaka hapa roho yangu ni nyeupeeee kwa kutua mzigo niliokua nimeubeba".
Jibu alilolitoa liliniacha mdomo wazi
Alisema "Hayo mbona ni mambo ya kawaida tu, sasa hilo ndo unaogopa? ha ha ha haaa, usijali. Sasa umenipendea nini mimi labda"
Nilishukuru kuona nimevua samaki bila chambo, basi nikajikuta kiduuuuume.
**************
Siku ziliendelea, lakini mdada yule alikuwa anamjua mwanamke ambaye nilikuwa na mahusiano naye kwa wakati ule. Alikuliza vipi yule ninayekuona naye ni demu wako? NIkamwambia ndio. Sikuona haja ya kumficha kwa sababu naye alisema kuwa ana bwana japo hajamuoa.
Siku moja aliomba tuonane mahala tuzungumze
Siku hiyo tukakutana sehemu tu ya kawaida tukapata kiyepe safi, huku tukipata mawili matatu (mazungumzo). Sikua na amani sana kwa sababu hapakuwa mbali na mtaani maana simjui mumewe anafananaje.
Kumbe mda wote ule jamaa ameshitukia ishu za mke wake kuna mabadiliko flani ameyaona akaanza kufuatilia kimya kimya
ITAENDELEA....................................
Mke wa mtu sumu
Dada huyu alikuwa na duka jirani na ambapo nilikuwa naishi. SIkuwa na mazoea naye kabisa awali. Lakini kadiri siku zilivokwenda alianza kuleta mazoea kidogo kidogo.
Muda wote sikuwa najua kama dada yule alikuwa na mume, nami sikuuliza kwa sababu hakunivutia kumtongoza.
Mazoea yalizidi kiasi kwamba siku nikibadili njia hulalamika sana na kuwa huwa anamiss kuniona na lile tabasamu langu uchwara.
Watoto wa mtaa wataungana nami kwani wanajua, demu akishaanza kusema kuna muda huwa anakumiss basi moja kwa moja unaona hapa ushakubalika. Basi hata kama mwanamke hukua na mpango wa kumpelekea moto utatafuta njia yoyote ile. Basi nami nikaona hapa bila shaka nimeshaeleweka ngoja nianze kucheba cheba.
Siku hiyo nikamwambia "siter ee",
akaitika "bee"
Nikamwambia kuna kitu natamani sana kukwambia ila najikuta roho inasita, ila usijali siku moja ntakwambia tu wala usijali. Kama utapata muda (siku flani) nitafute nikwambie.
Akasema sasa ntakutafutaje wakati wee namba yako sina? Akasema nipe namba yako. Nikambwia namba tuu hiyo mamy. Akasogeza simu yake nikaandika nambari kisha nikapotea.
Kabla sijafika (kazini) ambako nilikuwa naelekea nikatangamana na ujumbe usemao Namba yangu hiyo MIMI MAMA.....
Nikamwambia ooh asante, kumbe umeolewa? Mh basi sawa.
Akasema mbona umeguna? Nikamwambia basi hata ambacho nilitaka kukwambia nimegairi maana nilijua hujaolewa.
Akasema Ongea tuu kaka, we mtu mzima bana.
Mpaka hapa nikahisi kama mdudu anataka kupasua zizi, maana alivimba ghafla. Nikasema eeebwana mchuchu amejileta mwenyewe. Hapa ni kumaliza tuu
Nikamwambia "bana sister samahani, mimi nakupenda. Afu nimekuelewa sana ujue, lakini nilikuwa naogopa kukwambia kwasababu sikutaka kuingilia mahusiano yako ila nafsi imenishinda nami ni mwanadamu. Kama nimekosea nisamehe bure mpendwa. Lakini mpaka hapa roho yangu ni nyeupeeee kwa kutua mzigo niliokua nimeubeba".
Jibu alilolitoa liliniacha mdomo wazi
Alisema "Hayo mbona ni mambo ya kawaida tu, sasa hilo ndo unaogopa? ha ha ha haaa, usijali. Sasa umenipendea nini mimi labda"
Nilishukuru kuona nimevua samaki bila chambo, basi nikajikuta kiduuuuume.
**************
Siku ziliendelea, lakini mdada yule alikuwa anamjua mwanamke ambaye nilikuwa na mahusiano naye kwa wakati ule. Alikuliza vipi yule ninayekuona naye ni demu wako? NIkamwambia ndio. Sikuona haja ya kumficha kwa sababu naye alisema kuwa ana bwana japo hajamuoa.
Siku moja aliomba tuonane mahala tuzungumze
Siku hiyo tukakutana sehemu tu ya kawaida tukapata kiyepe safi, huku tukipata mawili matatu (mazungumzo). Sikua na amani sana kwa sababu hapakuwa mbali na mtaani maana simjui mumewe anafananaje.
Kumbe mda wote ule jamaa ameshitukia ishu za mke wake kuna mabadiliko flani ameyaona akaanza kufuatilia kimya kimya
ITAENDELEA....................................