K A B U R U
JF-Expert Member
- Nov 24, 2011
- 818
- 1,067
Una uhakika kilichokuuzi ni hicho ulichoandika au ukweli wa matokeo ya uchaguzi Kenya?Kwenu Uongozi wa JamiiForums huyu Mtu hajaanza leo kuwa na tabia ya Kunichokoza na kupenda kwa Makusudi Kuharibu Mtiririko wa ama Threads zangu au Posts zangu hapa JamiiForums.
Yeye anachojua ni Kunidhihaki na kwa Makusudi kabisa Kunichokoza ili nihamaki na nijibizane nae kwa Lugha ya Ukali ili Moderators wenu wakiona wanipe BAN kitu ambacho Yeye na Watu wa Kundi lake wenye Chuki zisizo na Kichwa wala Miguu na Mimi ndicho wanakitaka Kutwa.
Na kinachonishangaza hasa ni Kitendo cha Members hapa Kumchekea na Kufurahia Uchokozi wake na Dhihaka zake za kila mara dhidi yangu kwa Kumnyamazia ila GENTAMYCINE nikiamua tu Kupambana nae kwa Lugha niijuayo Mimi ambayo inaumiza zaidi ndipo utawaona Wao ( Members ) wengi Wanafiki wakiongozwa na Tate Mkuu wanajitokeza Kunilaumu na Kuhoji kwanini namjibu Kiukali ila ninapokuwa Nachokozwa na Nadhihakiwa nae huwa hawasemi Kitu na wala hawamsemi.
Kilichonishangaza zaidi na ambacho kila Siku nasema hapa kuwa huyu LIKUD ni Mmoja wa Moderators na pia anasapotiwa na baadhi yao ni kwamba Juzi tu tumetoka Kujibizana nae kwa Maneno Makali na siyo ya Kupendeza na nina uhakika Moderators waliona hilo Tukio na walijua kabisa kuwa Yeye ni Mchokozi na amekuwa na tabia ya kufanya hivyo Kwangu kila Siku hapa JamiiForums walichokifanya Moderators ni Kufuta zile Posts zetu za Majibizano yetu Makali na Kumuachia hadi Leo tena ameibuka na Utamaduni wake ule ule wa Kunichokoza.
Narudia tena na nina uhakika kuwa kuna Kikundi cha Watu ( Members ) hapa tena huenda wanasaidiwa ( Wanasapotiwa ) na Moderators ( baadhi ) kwa Roho zao Mbaya na Chuki Kwangu kutokana na Uwasilishaji wangu wa Kipekee wa Mada, Mvuto na Umaarufu wangu umekuwa ni Chukizo Kuu Kwangu GENTAMYCINE hivyo waneanzisha Mkakati Maalum wa Kunichokoza na Kunidhihaki kwa Makusudi ili Nihamaki ( kwa kujua nina Hasira za Karibu ) na Kuwajibu kwa Maneno yangu Makali ili Mada zangu ziwe zinaharibika Kimaudhui na ziwe Chafu ( kwa kujaa Majibizano yetu ya Lugha Kali ) na haraka sana GENTAMYCINE nipigwe BAN jambo ambalo ndilo wanalitaka liwe linanyika ( linafanywa ) dhidi yangu Kutwa hapa Jamiiforums.
Hata katika hii Post ambayo Mimi nimechangia tu kwa Mtazamo wangu kama walivyofanya Wengine ila amekuja tena Kunichokoza na Kunidhihaki ili nihamaki na tujibizane kwa Maneno Makali ili Lengo lake litimie na ninyi Moderators mkasirishwe nami kisha haraka mnipe BAN za Mwezi au Miezi Mitatu Mitatu kama ambavyo mmekuwa mkinipa na Mkakati wao Maalum dhidi yangu Utimie.
MImi ni Mvumilivu sana na mno halafu sina Unafiki wala Uoga na mpaka leo ( Usiku ) huu mnaona nimeandika hiki ( hivi ) jua nimechoka. Na asidhani kuwa kwa Kunichokoza na Kunidhihaki Kwake hivi anaweza Kushindana nami kwa Vita ya Maneno Makali ila nimeamua tu kuwa Mstaarabu kwa Kutomjibu vile anavyotaka na Kukusudia kwa Kuwaheshimu Members na kwa Heshima ya huu Mtandao ambao wengine umetusaidia Kutupa Maarifa na Kutukomaza zaidi Kifikra japo kwa Wengine umewasaidia Kuwaonyesha jinsi walivyo Majuha na Wendawazimu kwa Kuwekeza zaidi muda wao kwa Kunishambulia, Kunichokoza na Kunidhihaki GENTAMYCINE utadhani kuna chao chochote nilichokula au nina Deni nao.
Na namalizia kwa kusema huyu huyu Mtu hana tu hii ID Moja tu bali nina ID's zake zaidi ya Nne ( 4 ) ninazozijua ambazo kutokana na Upumbavu wake huwa ananishambulia, ananichokoza na kunidhihaki kwa Lugha hii hii Moja inayofanana. Na kuna Siku alinichoko:a Kimakusudi na nilipomjibu Vikali akaniambia ( narudia akaniambia ) atanipiga BAN na kweli ndani ya muda mchache tu nikapigwa hiyo BAN.
Mwisho naomba hii Post yangu ya Malalamiko kumhusu huyu Member isifutwe kwani kumekuwa na tabia ya pale tu GENTAMYCINE nikilalamikia Jambo hapa na nikimtagi ( Tag ) JamiiForums Founder Maxence Melo na huyu Cookie upesi sana hiyo post yangu inafutwa na sijui huwa ni kwanini inafutwa.
Posts za huyu Member LIKUD na Wengine wanaonichokoza, Wanaonidhihaki na Wanaonishambulia Kutwa hapa huwa zinaachwa na hazifutwi, ila nikiwa najibu Mapigo kwa Maneno yangu Makali au nawataja hawa akina Maxence Melo na Cookie haraka unaona post yangu inafutwa.
Na kila mara nasisitiza hapa JamiiForums kuwa kama unaona HUNIPENDI au HUNIKUBALI kwa namna yoyote ile GENTAMYCINE na Kwako Mimi sina THAMANI yoyote ya Kiuwasilishaji basi cha kufanya ni rahisi sana cha Wewe kuamua tu KUNIBLOKU ( IGNORE ) ila cha Kushangaa ni kwamba 99% ya Wanaojinasibu Kutwa hapa Jamiiforums kuwa WANANICHUKIA na HAWANIPENDI ndiyo hao hao Wanaoongoza kwa KUNIFUATILIA, KUNISOMA na hata baadhi yao ni 'FOLLOWERS' wangu Jambo ambalo huwa sielewi ni kwanini. Hivi Logically Yule unayemchukia unaweza ukapoteza muda wako 24/7 Kumfuatilia? Hili kama siyo tatizo Kubwa la Akili linalowakabili litakuwa ni nini tena? Wao wameshaona Mimi nikihangaika nao au hata kupoteza muda wangu Kuwasoma na hata tu Kuwafuatilia?
Kama mnamtuma semeni tu nijue.
Inakera.
Cc:. Moderator, Active, JamiiForums, Paw, Cookie and JamiiForums Founder Maxence Melo
Kama Kawaida yenu na nilikitegemea Jana Usiku baada ya Kuandika post hii hii haraka sana mkawahi Kuifuta na Kufuta comment yake LIKUD na najua hata hii nayo mtaifuta muda si mrefu ili Kumlinda na Kuonyesha Kufurahia Kwenu anavyonichokoza, anavyonidhihaki na anavyonishambulia Kutwa hapa Jamiiforums. Na kamwe sitochoka Kuwalaumu na Kuwalalamikieni juu ya hili na huyu Member.