Yaliyojiri Jijini Arusha: Mkutano wa Mgombea wa CCM, Dk. Magufuli – Oktoba 6, 2015

Hakuna mtu aliyetegemea kama siku ya leo Dr. Magufuli angepata watu katika uwanja wa Sheik Amri Abeid Arusha. Hata yeye mwenyewe Magufuli hakuamini alichokiona leo. Watu walikuwa wengi sana hasa ikizingatiwa kuwa Arusha ni ngome ya CHADEMA. Mbaya zaidi, vijana waliokuwa wamevalia sare za CCM walikuwa wengi mno. Mimi mwenyewe leo nilikuwa Arusha na nikasema lazima niende nikashuhudie nini kitatokea huko. Sikuamini kabisa!

Kumekuwa na upotoshaji mkubwa sana kuhusu wana CCM wa Arusha. Tumewasikia Mara nyingi sana UKAWA wakisema eti Arusha CCM imekufa, hapana, Arusha CCM iko hai tena iko imara sana. Nilichogundua WanaCCM wa Arusha sio watu wa kupiga kelele na kujionesha barabarani. Leo vijana wa CHADEMA walipigwa na butwaa hasa walipoona vijana wenzao kwa maelfu wakiwa wamevalia mavazi ya CCM.

Mimi ni mwanaCCM ambae sikai Arusha lakini leo nilifurahi sana tena sana kwa nilichokiona. Kuna kila dalili, jimbo la Arusha mjini linarudi mikononi mwa CCM. Nilikuwa nimekaa na wenyeji wa mji huu pale uwanjani, na wengi wao walisema CHADEMA ilishinda Ubunge Arusha sababu wazee wengi wa CCM walichukizwa na aina ya mtu waliyepewa wakati ule ndio maana wengi wao hawakupiga kura. Sasa hivi wanasema wamechukizwa zaidi na Lema sababu ameifanya Arusha kuwa ni ya maandamano na vurugu na mabomu kitu ambacho wanajuta. Wakazi wengi wa Arusha wameapa kumchagua Philemon Molel {MONABAN} kuwa Mbunge wao.

Nafahamu fika kuwa mshindi wa urais anapatikana kwa kupigiwa kura, lakini ukweli utabakia pale pale kuwa Magufuli ana nafasi kubwa sana ya kuingia Ikulu na ninaweza kusema mpaka sasa ni kama Magufuli amemaliza Kampeni na leo amefunga kazi Arusha mjini. Hata yeye mwenyewe leo baada ya kuona umati uliojaa uwanjani alisema sasa basi, yeye ameshakuwa rais tayari. Mimi pia nasema nikiwa kama mwana CCM kwa nilichokiona leo Arusha ambayo ni ngome ya CHADEMA, basi hakuna ubishi, Magufuli ndio rais mpya wa Tanzania.

#HapaKaziTu CHAGUA MAGUFULI.

Thubutu yako, sisi ndiyo A Towners wazee wa Dili.Nani hapendi kula na vipofu?

Hakunaga CCM huku A Town kwa taarifa yako chaliangu, ukitaka kuamini muulize Batillda na Felix Mrema wanatujua vema, wewe waja leo na kurudi kesho huwezi pata ukweli.Zaidi njoo kijiwe utatukuta tunepeana mrejesho wa kazi.
 
Thubutu yako, sisi ndiyo A Towners wazee wa Dili.Nani hapendi kula na vipofu?

Hakunaga CCM huku A Town kwa taarifa yako chaliangu, ukitaka kuamini muulize Batillda na Felix Mrema wanatujua vema, wewe waja leo na kurudi kesho huwezi pata ukweli.Zaidi njoo kijiwe utatukuta tunepeana mrejesho wa kazi.

Batilda na Felix hawakuwahi kukusanya mafuriko ya namna hii
 
Kila sehemu mukisha bebelea watu, basi mumeshinda. Amakweli mumeishiwa kweli. Mwakahuu mumeshikwa pabaya kweli.
 
Sasa kama unajua kuna mungu kwa nini mnaingilia kazi ya mungu na kiwaombea binadamu wenzenu matatizo...........wakipasuka wote atatawala wafu......
 
Piga hesabu 15000 mara idadi ya watu waliofika, kisha zidisha na wengine mikoa mingine ambayo inasemekana watu walinunuliwa, kisha shirikisha ubongo wako! Je inawezekana?

mkuuu ukawa watakuchoshaa bureee kuleee wengi shulee hawajaenda wakijitaidi Sana ni form four leavers tu.ivooo akiri zao hazijui kuchuja ilaaa zunajua kuropoka tuuu pasipo Ku meditate kwanza
 
Katibuni kesho tarehe 7/10 viwanja vya shule ya msingi mringa na tar 8/10 maeneo ya unga ltd Arusha ukutane na mh raisi ea awamu ya tano E.Lowasa atawanadi wagombea wa ukawa.karibuni sana.
 
Arusha wamekubali kazi na wanataka kazi tu!

Karibia robotatu ya waliohudhuria walitoka nje ya jiji la Arusha na ushahidi ni pale watu kama ni wenyeje wa Arusha kwa nn waulize maeneo haya hapa chakula kinapatikana wapi! pia wengine walienda Fiesta!
 
Pipoooooooooooooooooz ✌✌✌✌✌✌✌✌✌✌
hapa kazi tu. utabiri wa kuhani mkuu wa chadema gwajima et al ni mizungu tu oct 25 tunachagua mtu muadilifu na mchapa kazi magufuli. hapa ni kazi tuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuiuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuuu.
 
Sina maana kuwa mimi ni mshabiki wa Chama chochote ila kujaa kwa watu kwenye majukwaa ya kisiasa siku hizi ushindi wa chama husika ila watanzania wameelimika kwa kusiliza Sela za wagombea husika.......ushindi bado ni changamoto tu kukipa asilimia mia chama huko ni kujifariji.
 
Watu kweli mnashangaza na ni wepesi wa kusahau kweli kweli. Magufuli alipozindua kampeni Jangwani Dar mkapagawa mara oh kwa tulichokiona Jangwani leo Magufuli ni Raisi. Hazikupita siku saba Lowassa akatinga Jangwani na loo mkanyamazishwa kama vile mmemwagiwa maji baridi.

Magufuli akafika Mbeya na kwa mhemuko mkasahau ya Dar es Salaam hadi siku Lowassa alipotua Mbeya mkawa kimyaaa!
Magufuli akafika Tanga mkapagawa tena hadi Lowassa alipotua huko na kuwanyamazisha. Kama vile hamna kumbukumbu leo mmeanza tena baada ta Magufuli kufika Arusha...

Mmeshindwa kabisa kuona tofauti iliyopo kati ya mafuriko na gharika, unazi umewapofua; mnayo macho lakini hamuoni, mnayo masikio lakini hamsikii. Basi hamna tena namna, subirini kipigo cha Oktoba 25!

Mage3 katika ubora wake. Mkuu uko vizuri. I trust you
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom