Yajue makundi mawili ya TAHLISO

Yajue makundi mawili ya TAHLISO

Kahumbi Lumola

JF-Expert Member
Joined
Mar 3, 2012
Posts
359
Reaction score
2,569
Mimi ni Waziri Mkuu wa serikali ya wanafunzi DIT, Lumola Steven Maziku KAHUMBI. leo nataka nichangie maoni yangu kwa uchache kuhusu TAHLISO yetu, kisha nitaweka wazi mimi nipo katika kundi gani.
TAHLISO ina makundi mawili;
1. kundi la wanaojihusisha na siasa za nchi na 2. kundi ambalo siasa mwiko kwenye TAHLISO ila ni maslahi ya wanafunzi tu.

Nitaanza na kundi la pili ambalo mimi nipo katika kundi hilo. kundi hili hatuna agenda yoyote inayohusu siasa za kinchi NGUVU na AKILI zetu tumezielekeza kwenye eneo moja tu nalo si jingine ila ni la KUDAI MASLAHI ya wanafunzi wote wa TAASISI ZA ELIMU YA JUU nchini na hatupo tayari kuona maslahi rasmi ya wanafunzi yanachezewa iwe na serikali kuu kwa ujumla au iwe wizara fulani au bodi fulani au mtu yeyote yule. kazi yetu ni moja tu na agenda yetu ni wanafunzi.
MSIMAMO WETU WA KUNDI LETU. Kama serikali itatimiza mambo ya wanafunzi ndani ya muda kama taratibu zinavyoelekeza basi wataifanya TAHLISO iwe kama haipo kwasababu hatutakuwa na la kutufanya tutoke tuseme au tuandamane n.k. njia nzuri na njema ya kudhibiti kundi hili, serikali ikikaa kupanga mipango yake basi wanafunzi vyuo vikuu wawe ni wa kwanza.

KUNDI LA PILI. hili ni kundi la WASAKA TONGE, walafi ambao wanafikiri maisha mazuri yanapatikana kwa njia ya kujipendekeza kwa wenye nacho na wenye vyeo. kundi hili halijawahi na halitakuja kuwahi hata mara moja kutoka mbele kusimamia maslahi ya wanafunzi. ukiwaona wametoka basi ujue kuna mgombea urais ameongezeka wamekuja kumuunga mkono, hiyo ndio kazi yao. kwahiyo kwa MUHUTASARI kundi hili ni kundi linalojihusisha na siasa. Ninalichukia sana hilo kundi na MwenyeeziMUNGU atalilaani kundi hilo baya tena wao pamoja na washirika wao.

MATATIZO VYUO VIKUU.
hatukatazwi kufanya siasa lakini kuitumia TAHLISO kama mwavuli ni Dhambi isiyosameheka, mafikirio na ajenda za kisiasa tukazifanye vyama vyetu vya siasa tukumbuke sisi kama wasomi hatupaswi kuwa na haraka ya maisha hii nchi ni ya kwetu baina yetu leo ndio kuna Rais wa mwaka 2030 tena huenda nikawa ni mimi au mwingine yoyote pia baina yetu ndio kuna usalama wa taifa, maaskari, wakurugenzi, wabunge mawaziri n.k. hakuna atakayekuja kushika nafasi hizo ila ni sisi vijana wenzangu wasomi tusitumike ila tufanye kama sisi tujisaidie sisi na Taifa letu kwa ujumla.
 
Chadema zamani kwa sass ukawa wanawaharibu Sana maana wanawaletea yasiyofaa
 
Wataje hao wasomi wasaka tonge usije ukawa unaleta majungu humu kamanda!!

Kama kuna viongozi wa wasomi ambao ni waska tonge basi mambo si shwari!!!
 
Wewe Kahumbi si mmoja wa wale wanaoshikiliwa na Polisi kwa kufanya mikutano feki?
 
Wataje hao wasomi wasaka tonge usije ukawa unaleta majungu humu kamanda!!

Kama kuna viongozi wa wasomi ambao ni waska tonge basi mambo si shwari!!!
Mkuu, huyu mwenyewe ni msaka tonge sema anatumika na UKAWA
 
BTW:Makubdi yote yamechaguliwa na wanafunzi... Hawezi matatizo yakawa viongozi wenzako Bali wanafunzi waliowachagua!
 
BTW:Makubdi yote yamechaguliwa na wanafunzi... Hawezi matatizo yakawa viongozi wenzako Bali wanafunzi waliowachagua!
Mkuu, ni kweli kabisa. Ila ujue hata hao wanafunzi wapo kwenye makundi mawili. Pro CCM ambao ni wengi na Pro Opposition ambao ni wachache. Hawa wa opposition ndio wanaotumika kwenye maandamano na fujo. Hawa ndio wanaotandikwa virungu na mabomu ya michozi kutokana na ujinga wao
 
Kahumba,,, mie nataka utupe taarifa ya kuaminika na sio propaganga za siasa ni lini vyuo ambavyohawajapatiwa pesa zao watapewa???
 
Aya ya mwisho,imeharibu utangulizi na kukusogeza karibu kabisa na unaosema unawapinga na kuwalaani,na isitoshe ukajipingia na cross sasa ya 2030!

Ikiwa una ndoto kubwa za kisiasa na kuproject hadi mwaka,moral authority ya kuwalaani wenza unaipataje?! Sema tu mnapishana makundi na price tag!!!!
 
Mleta Mada Ni Msakatonge Mkuu Kama Hamjamgundua tena Ni Gamba linalotoa Moshi
 
Asante sana kamanda kahumbi watanzania ni wagumu sana kuelewa binafsi nimekusoma ila ukiangalia comments nyingi hapa hazina mantiki na huwezi amini ni wasomi hao.
Tusimamie kweli na kweli itatu vushawww
 
Last edited by a moderator:
kwa mujibu wa majibu ya afisa kutoka kanda maalumu alituambia suala hilo la malipo linashughulikiwa kwa ukaribu na wiki ijayo vyuo vyote vilivyosalia watapata. Don joshua
 
Last edited by a moderator:
kwa mujibu wa majibu ya afisa kutoka kanda maalumu alituambia suala hilo la malipo linashughulikiwa kwa ukaribu na wiki ijayo vyuo vyote vilivyosalia watapata. Don joshua

Wewe elimu bado haijakukomboa. Ningeamini wewe mwanaume endapo hizi shutuma zako ungezisema mbele ya wale walokuchagua. Na hao wachumia TUMBO wenzako ungewataja kwa majina. Ili ile dhana ya dalili za mnafiki ikutoke
 
Last edited by a moderator:
Mkuu, ni kweli kabisa. Ila ujue hata hao wanafunzi wapo kwenye makundi mawili. Pro CCM ambao ni wengi na Pro Opposition ambao ni wachache. Hawa wa opposition ndio wanaotumika kwenye maandamano na fujo. Hawa ndio wanaotandikwa virungu na mabomu ya michozi kutokana na ujinga wao

Acha kudanganya watu hakuna msomi mwenye akili timamu aliyepo CCM.
 
makamo mwenyekiti,anaetangaza kua mwenyekiti si halali,sijui anamanisha nn,na anatetea serikali kuhusu fedha za field kychelewa,hakika tulikosea,hakika hatufai
 
Ok ngoja tusubiri lkn mkuu
Tunaomba kuwe na mabadiliko TAHLISO kwa sasa ya uongozi na utendaji maana kutuambia kuna makundi mawili na kila kundi linatoa taarifa yake linavyoamua na sisi wanafunzi tunategemea chama chetu makini kama TaAHLISO hakina makundi kama ya CCM plzz over Plzz tunaomba tuwe kitu kimoja mtu akishindwa kuheshimu sheria za uongozi za TAHLISO naomba afukuzwe uongozi na sio kubaki na cheo bila masilahi ya wanafunzi..
 
Kila kitu sasa hivi kimeingiliwa na kuharibiwa na Siasa!
 
Back
Top Bottom