Yahusu kufuta kauli

Mshana Jr

Platinum Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
360,449
Reaction score
829,819
Mjadala wa BILIONI 1500 unazidi kushika kasi... Sasa watu wanaulizwa ni kweli zimepotea... Wanasema hapana hazijapotea.

Na ni kweli hakuna panaposema zimepotea ila zimeingizwa kwenye matumizi yasiyoonekana kwenye makaratasi ya kumbukumbu. Sasa baada ya hapo kila mtu anaweza kuchanganya na za kwake.

Mbunge mmoja kule Afrika kusini wakiwa bungeni akasema nusu ya wabunge wote humu ndani ni wapumbavu. Kauli hii ikawakera wengi mpaka supika akamwamuru jamaa afute kauli yake.

Hakubisha! Akakubali kufuta kauli yake kwa kusema nusu ya wabunge wote humu ndani sio wapumbavu!!

Hivi tofauti ya kupotea na kutojulikana kilipo kitu ni ipi!?

Tunaishi nchi ya wanoni... Ni nani akamfunge paka kengele!? Ili akija wote tumsikie?
 
Ni kweli hazijapotea ila zimetumika ndivyo sivyo
 
Taifa la ajabu sana hili huu ujinga duniani unapatikana hapa!!! Ashakum si matusi si ajabu kiongozi wa Taifa fulani alimwambia mtawala fulani anaongoza maiti hii kauli ya miaka ya 70's huko hadi leo inaishi.
 
Taifa la ajabu sana hili huu ujinga duniani unapatikana hapa!!! Ashakum si matusi si ajabu kiongozi wa Taifa fulani alimwambia mtawala fulani anaongoza maiti hii kauli ya miaka ya 70's huko hadi leo inaishi.
Lile roho mpaka leo linaishi halafu limekuwa jitu zima sasa
 
Nusu yawabunge humu ndani niwapumbavu, nafuta kauli Nusu yawabunge humu ndani sio wapumbavu aisee bado maana inabaki ileile yakwanza
Kupotea na kutojulikana ๐Ÿ˜€ ๐Ÿ˜€ ๐Ÿ˜€
 
Yetu majicho na ma midomo na mashikio.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ