Yahusu kampuni ya uuzaji viwanja mkoani Dodoma, Land Netwotk

Bususwa

JF-Expert Member
Sep 30, 2021
429
1,011
Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pole na majukumu mazito ya ujenzi wa taifa letu! Mh Rais wetu kwanza nakupa hongera sana kwamba hua unapita pita hapa Jamii Forum kusoma maoni ya wananchi wako,yale mazuri hua unayafanyia kazi na mengine hua unayaboresha na huo ndiyo uongozi thabiti!

Mh Rais wetu mimi nikijana mdogo sana mwenye malengo makubwa mbele ya safari zangu za utafutaji wa maisha!

Mh Rais wetu, mwaka 2021 nilinunua kiwanja hapa Dodoma eneo la Nala Chihoni kwa hawa jamaa wanaoitwa Land Network, sababu ni kampuni kubwa niliwaamini sana, nililipa pesa bila ya kwenda kuangalia viwanja vikoje!

Kumbe vile viwanja kwanza havijafanyiwa usafi, ni kwamba hawa jamaa walinunua pori kubwa,wakaanza kulipima kwa kukata viwanja vipande vipande, lakini hawajafanya chochote hadi leo hii ukienda huko huwezi kukiona kiwanja chako zaidi yakuona pori tu

Mh Rais wetu, nikaenda ofisini kwao kuomba wanipeleke kwenye kiwanja changu, nilipofika nikakuta ni pori kweli unaweza kuta hata kuna Simba au tembo kabisa kwenye hilo pori, huo ni mwaka 2021 kipindi hicho nimemaliza kulipa gharama za kiwanja na mambo mengine, nikauliza mtakuja lini kufanya usafi yaani kufyeka hili pori ili niweze kukijua kiwanja changu?? Wakasema mitambo kama Motor Grader wameagiza kutoka Nje ya Tanzania,kwa hiyo ikifika tu watafanya usafi na mimi nitaonyweshwa kiwanja changu sehemu kilipo!

Mh Rais wetu tangu kipindi hicho cha mwaka 2021, mitambo imekuja mwaka 2022 mwishoni, nikaenda tena pale, nilikutana na wenzangu na wenyewe kero ni kama yangu, wamelipa pesa kwenye viwanja,lakini hadi leo hawajui hata viwanja vyao viko wapi! Mitambo yakufanya usafi imekuja lakini nasikia wanakodisha kwa wakandarasi wa ujenzi wa barabara na sisi hawaendi tena kufanyia kazi yetu

Mh Rais wetu kila mtu hua anamipango yake, toka 2021 hadi leo, kama ningekua najua kiwanja kiko wapi,ningekua nishaanza na ujenzi lakini hadi leo nipo nipo tu, hadi nawaza nijipange tu upya ninunue kiwanja kingine tu!

Mh Rais wetu hawa jamaa wamekua wahuni, na wanatoa majibu mepesi sana kwenye jambo la msingi!

Ombi langu kwako,kama utapita hapa au wasaidizi wako watapita hapa! Basi naomba Waziri wa Ardhi,Mkurugenzi wa Jiji Dodoma na Land Network wape amri ili waweze kulifanyia kazk ombi letu! Wanatukwamisha pakubwa sana hawa jamaa

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Pole kwa kuuziwa mbuzi katika gunia?je wameshakupa hata hati yako au document yoyote ya kuthibitisha umiliki wa hilo eneo?usije ukawa unasubiri dodo chini ya mnazi.
 
Pole kwa kuuziwa mbuzi katika gunia?je wameshakupa hata hati yako au document yoyote ya kuthibitisha umiliki wa hilo eneo?usije ukawa unasubiri dodo chini ya mnazi.
Documents zipo na eneo lipo! Shida ni kwamba hawajatuonyesha tu eneo letu, hilo ni pori aieeee
 
Yani ufanyaji wa usafi wa viwanja vyetu tulivyonunua kwa makampuni binafsi, mh. Rais aingilie kati?

Kwa nini tusingeanzia kwa viongozi hapo Mkoaji au jiji?....wakizingua toa ka laki mbili kaka safisha eneo lako ndg yangu.
 
Pole sana Mkuu, shida kama hii siyo ya kwenda kwa Mh Rais aisee ana mambo mengi mno,
Ungeweza hata kwa mkurugenzi wa halmashauri tuu au naibu waziri angetosha kingine kama wamekupatia documents maana yake Kuna coordinate ambazo ukiwa na GPS unaweza kupafahamu bila shida...
Hivyo chukua hizo coordinate mpatie surveyor yeyote hapo manispaa mpoze 50, 000/- utaweza kuliona eneo lako
 
Yani ufanyaji wa usafi wa viwanja vyetu tulivyonunua kwa makampuni binafsi, mh. Rais aingilie kati?

Kwa nini tusingeanzia kwa viongozi hapo Mkoaji au jiji?....wakizingua toa ka laki mbili kaka safisha eneo lako ndg yangu.
Utasafishaje eneo bila yakujua unaanzia wapi na unaishia wapi?? Hujui hata B corn zako ziko wapi?? Kweli???

Sent from my SM-A032F using JamiiForums mobile app
 
Nyie sasa mnataka kufanya mheshimiwa Rais aache kuingia JF.

Hizi ishu ni za kuripoti kwa Rais, hebu acheni utoto asee. Kudeka gani kwa hovyo huku

By the way unasema ulishapelekwa kuoneshwa kiwanja chako na documents zipo yaani unashindwa kuanza kujenga kwa sababu kampuni iliyokuuzia kiwanja haijasafisha eneo?

Kwanza Nani kakwambia viwanja vinapimwa vikiwa visafi? Yanapimwaga mapori ndio vinageuka viwanja. Kama unashindwa kusafisha kiwanja chako utaweza kujenga wewe jamaa?
 
Huu nao ni ujinga Wa hali ya juu Sasa unatoaje pesa ata kiwanjani ujafika ujapaona mipaka ujaijua kwaiyo ulionyeshwa kwenye picha au mchoro au kwa mbali kwamba ni palee dah aisee pole sana ndugu yangu
 
Muanzisha Uzi pole sana,na ilikuaje ukaenda kununua kiwanja Chihoni mbali kule wakati hapa Nala Mizani mpaka Nala ya Kwanza kuna Viwanja vingi tu vizuri tena kwa Bei rafiki?njoo inbox nikuuzie kiwanja kizuri,kisafi na ambacho utaanza kujenga moja kwa moja bila ya kuingia gharama ya kusafisha nk
 
Nyie sasa mnataka kufanya mheshimiwa Rais aache kuingia JF.

Hizi ishu ni za kuripoti kwa Rais, hebu acheni utoto asee. Kudeka gani kwa hovyo huku

By the way unasema ulishapelekwa kuoneshwa kiwanja chako na documents zipo yaani unashindwa kuanza kujenga kwa sababu kampuni iliyokuuzia kiwanja haijasafisha eneo?

Kwanza Nani kakwambia viwanja vinapimwa vikiwa visafi? Yanapimwaga mapori ndio vinageuka viwanja. Kama unashindwa kusafisha kiwanja chako utaweza kujenga wewe jamaa?
Huyu anadeka sana. Pale Nala Dodoma kuna pori gani la Simba na Tembo?
 
Yani ufanyaji wa usafi wa viwanja vyetu tulivyonunua kwa makampuni binafsi, mh. Rais aingilie kati?

Kwa nini tusingeanzia kwa viongozi hapo Mkoaji au jiji?....wakizingua toa ka laki mbili kaka safisha eneo lako ndg yangu.
Unajichanganya. Umesema ulienda kuoneshwa kiwanja kilipo, kwamba hukuoneshwa mipaka walikuonesha pori?

Acha kulialia. Safisha kiwanja chako achana na matapeli hao as long as umeona mipaka na eneo lako.
 
Yani ufanyaji wa usafi wa viwanja vyetu tulivyonunua kwa makampuni binafsi, mh. Rais aingilie kati?

Kwa nini tusingeanzia kwa viongozi hapo Mkoaji au jiji?....wakizingua toa ka laki mbili kaka safisha eneo lako ndg yangu.
Walifanya hilo kwa ubia na Dodoma Jiji.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom